Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 10,394
- 17,984
Prof Peter Erlinder ambaye ni wakili anayewatetea watuhumiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. Ameomba kuwasilisha utetezi wake kwa wateja anaowawakilisha kwenye mahakama ya kimataifa ya Rwanda kwa kupitia picha za video yaani 'video conference'. Anasema usalama wake uko mashakani kama atakuwapo mahakamani Arusha kimwili kwa kuwa Serikali ya Rwanda inatekeleza mpango wa kuwaua watetezi wote wa watuhumiwa wa mauaji ya kimbari. Profesa Peter ambaye ni mwanasheria wa Kimarekani anasema hataki yampate yaliyompata mwanasheria mwenzie Profesa Juani Mwaikusa wa UDSM aliyeuawa kikatili nje ya nyumba yake mwaka jana. Ingawa sitaki kuingilia mchakato wa DCI na mahakama lakini nataka mdau mwenye details zaidi atujuze!