Giro
JF-Expert Member
- Feb 9, 2009
- 359
- 22
Katika mahojiano yake yaliochapishwa katika gazeti la RAI alhamisi iliyopita,Waziri wa fedha wa zamani katika serilikali ya awamu ya tatu,Profesa Simoni Mbilinyi amejitosa katika mjadala unaomhusisha rais mstaafu Benjamini Mkapa,
Profesa Mbilinyi anasema aneyestahili kuchunguzwa ni Anna Mkapa wala si mumewe Benjamini Mkapa.Mbilinyi anasema hatua ya kumpeleka Mkapa mahakamani inaweza kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.
***************************************************************
Wakati hayo yakijiri,serikali imebanwa na Bunge kiasi cha kulazimika kuanza kufikiria uamuzi wa kisheria na hata kutafakari fursa ya kumwondolea kinga Raisi Mkapa, au kumuhoji kuhusu mgodi wa makaa ya mawe kupitia kampuni ya ANBEN.Habari za kuaminika zina sema umiliki wa mgodi huo ulifanyia mabadiliko kutokana na mwenendo wa mambo na hasa baada ya suala hilo kuonekana kumuweka pabaya kisiasa na kisheria Mkapa.Katika mabadiliko hayo nyaraka za sasa zinabainisha kuwa mgodi huo unamilikiwa na kampuni ya Tanpower Resource Ltd,ambayo ni muungano wa kampuni nne tofauti
(1)Fosnick Ltd..ambayo wanahisa wake ni Nick Mkapa,Foster Mkapa na mwingine anayetambulika kama B.Mahembe
(2)Choice Industries--ambayo wanahisa wake ni Joe Mbuna na Goodyear Francis
(3)Devconsult Ltd--wanahisa wake ni D.Yona na Dan Yona jr
(4)Technologies Ltd--wanahisa wake ni Wilfred Malekia na Evans Mapundi
Habari za kuaminika zinasema tayari nyaraka za awali (original) zenye kuonyesha kuwa mgodi wa Kiwira unamilikiwa na kampuni ya ANBEN ambayo ni ya Mkapa,zimefikishwa katika uongozi wa juu wa Bunge nyaraka hizo zimejitosheleza kiushahidi kwamba Mkapa ni mmiliki wa ANBEN.
Mkapa si msafi ana kutu hivyo hata kama kina Mbilinyi na wenzake watamuogesha na kumsugua na sabuni ya mbuni mara tano kwa siku.Mkapa katu hato kuwa msafi ,labda tumpake rangi(afikishwe mahakani akajibu)
Profesa Mbilinyi anasema aneyestahili kuchunguzwa ni Anna Mkapa wala si mumewe Benjamini Mkapa.Mbilinyi anasema hatua ya kumpeleka Mkapa mahakamani inaweza kurudisha nyuma maendeleo ya Taifa.
***************************************************************
Wakati hayo yakijiri,serikali imebanwa na Bunge kiasi cha kulazimika kuanza kufikiria uamuzi wa kisheria na hata kutafakari fursa ya kumwondolea kinga Raisi Mkapa, au kumuhoji kuhusu mgodi wa makaa ya mawe kupitia kampuni ya ANBEN.Habari za kuaminika zina sema umiliki wa mgodi huo ulifanyia mabadiliko kutokana na mwenendo wa mambo na hasa baada ya suala hilo kuonekana kumuweka pabaya kisiasa na kisheria Mkapa.Katika mabadiliko hayo nyaraka za sasa zinabainisha kuwa mgodi huo unamilikiwa na kampuni ya Tanpower Resource Ltd,ambayo ni muungano wa kampuni nne tofauti
(1)Fosnick Ltd..ambayo wanahisa wake ni Nick Mkapa,Foster Mkapa na mwingine anayetambulika kama B.Mahembe
(2)Choice Industries--ambayo wanahisa wake ni Joe Mbuna na Goodyear Francis
(3)Devconsult Ltd--wanahisa wake ni D.Yona na Dan Yona jr
(4)Technologies Ltd--wanahisa wake ni Wilfred Malekia na Evans Mapundi
Habari za kuaminika zinasema tayari nyaraka za awali (original) zenye kuonyesha kuwa mgodi wa Kiwira unamilikiwa na kampuni ya ANBEN ambayo ni ya Mkapa,zimefikishwa katika uongozi wa juu wa Bunge nyaraka hizo zimejitosheleza kiushahidi kwamba Mkapa ni mmiliki wa ANBEN.
Mkapa si msafi ana kutu hivyo hata kama kina Mbilinyi na wenzake watamuogesha na kumsugua na sabuni ya mbuni mara tano kwa siku.Mkapa katu hato kuwa msafi ,labda tumpake rangi(afikishwe mahakani akajibu)