Aliyeenda JPM kuanzisha bwawa la mwl Nyerere lilikuwa la kuupa msukumo SGR. Sasa mmekuja na longolongo nyingine.Hiyo tofauti ya ujenzi kati ya reli za China na Korea na hii reli yetu ya SGR ni ipi?
Nina wasiwasi Mbarawa asijekutumia udhaifu wao wa kununua vichwa chakavu vya treni ya SGR, vilivyosababisha spidi iwe ndogo, akahamishia kwenye ujenzi wa reli.
Maana naona siku hizi ni kama kuna mchezo huko serikalini wa kumtupia lawama The late Magufuli kwenye kila kitu.
Wajanja wamekula pesa kwenye ununuzi wa vichwa vya treni, wameachwa hawafanywi chochote na bosi wao, wapo tu wanatamba kwa ukwasi..
Leo malengo ya utengenezaji wa reli ya SGR ili kurahisisha usafiri yameshindwa kufikiwa, lawama inatupiwa njia ya treni!.
Mbona hili jambo halikuwahi kusemwa kabla? sasa kuna maana gani ya kuwa na hiyo reli ya SGR?
Prof. Mbarawa ameonesha incompetence muda mrefu sana kwenye hiyo wizara, ajabu anaachwa tu, na haya ndio matokeo yake.
Kwa kauli hii ya Prof. Mbarawa, sasa hata ujenzi wa JNHPP nao hauna maana, lile bwawa sasa limegeuzwa la kutuondolea ile migao yao ya umeme wanayoitengeneza, yale malengo mahususi ya kuzalisha umeme wa kuendesha treni ya SGR yamekufa.
I doubt kama yupo atakayekuwa tayari kupoteza muda wake atoke Dsm kwenda Morogoro kwa masaa matatu, wamechezea pesa nyingi, wamepoteza muda, wameshindwa kufikia malengo.
Majuzi mmewaambia wanaoishi ukanda wa Rufiji na Kilwa eti Wahame kutokana na athari za maji mliyoyafungulia wenyewe ya bwawa .
Kama sio mwanzo wa kuhujumu hili bwawa ni nini!
Mwisho wa siku hakutakuwepo na maji!
Hao wananchi mliowafungulia hayo maji waende wapi na je mko tayari kuwalipa fidia kwa uzembe huo?
WaTanzania msiwafanye wajinga.
Katiba mpya Katiba .