Prof Lipumba aenda World Bank

mimi sijawahi kuskia rais profesa duniani

hata mmoja sijawahi kuskia

thirsty.jpg


Angela Merkel, Gordon Brown and Yule wa Chile anaitwa hasa Professor Sibastian Pinera unataka wengine?
 
Wasomi Tanzania huwa hawakubaliki hata siku moja, utashangaa mtu kama Prof. Majimarefu anakubalika kuzidi Prof. Lipumba.
Wewe nenda zako kafanye kazi na wazungu, huku tuache kama tulivyo Miafrika ndivyo ilivyo
 
Wasomi Tanzania huwa hawakubaliki hata siku moja, utashangaa mtu kama Prof. Majimarefu anakubalika kuzidi Prof. Lipumba.
Wewe nenda zako kafanye kazi na wazungu, huku tuache kama tulivyo Miafrika ndivyo ilivyo

Mkuu umenena. Prof. Maji Marefu anakubalika kuliko Prof. Lipumba sasa hapo si ndio inaonyesha jinsi akili zetu zinavyorudi nyuma
 
mimi sijawahi kuskia rais profesa duniani

hata mmoja sijawahi kuskia

thirsty.jpg

Rais wa awamu ya kwanza Nyerere na rais wa awamu ya pili Mzee Ruksa walikuwa walimu, si lazima tuende mbali kutafuta mataifa mengine, ila historia ya nchi yetu tu inajieleza. Au wewe mgeni wa historia tukusaidie?

Mwalimu au mkufunzi ni kazi ile ile iwe shule ya kawaida au elimu ya juu wote wako katika category moja yakhe.
 
Nduka original jaribu kupitia na thread za wenzako.umejibiwa kuwa Nabii hakubaliki kwake. Kikwe na serikali yake hawajakubali kuwa ana kitu special huyu jamaa.
 
Affirmative action.

Kuna nafasi nyingine huwa zinatengwa kujazia jazia Waafrika ili kumbi za mikutano zipendeze na rangi mbali mbali, hailazimu kwamba huyu ndio mkali kwa sana katika level za kidunia. Wewe mchumi, nchi yako masikini wa kutupwa na kukanyagwa unaenda Ulaya kushauri uchumi, kumshauri nani?
 
Haendi kufanya kazi amepata fellowship anakwenda kusoma/ kufunzwa, Fungueni hiyo link muone. Watu wa cuf mnampa ujiko bure eti anakwenda world Bank!!!

Fellowship hii sio ya kusoma au kufunzwa wewe ndugu hii unafanya utafiti au kwa jina jengine inaitwa research fellowship hivyo hawajakosea anaenda kufanya kazi kwani fellowship hizo unalipwa na mshahara na marupurupu mengineyo kama mtafiti wa kuajiriwa World Bank. Hio sio post ya kuandaa matamasha yenu ya World Economic Forum ambapo mshauri wenu anaenda kule.
 
Haendi kufanya kazi amepata fellowship anakwenda kusoma/ kufunzwa, Fungueni hiyo link muone. Watu wa cuf mnampa ujiko bure eti anakwenda world Bank!!!
Mkuu wangu, napata tabu kidogo naomba uniweke sawa anakwenda kusoma halafu World Bank wanamlipa pesa kwa kusoma tu?
 
Kuna nafasi nyingine huwa zinatengwa kujazia jazia Waafrika ili kumbi za mikutano zipendeze na rangi mbali mbali, hailazimu kwamba huyu ndio mkali kwa sana katika level za kidunia. Wewe mchumi, nchi yako masikini wa kutupwa na kukanyagwa unaenda Ulaya kushauri uchumi, kumshauri nani?
Mkuu wangu, basi hao wazungu wa World Bank watakuwa wajinga sana.
Kila siku wae wanamuita huyo Prof Lipumba, wanawaacha kina Chiligati, Prof Maji Marefu, Mrema, Makamba, Tambwe Hizza, Dovutwa Faham Dovutwa
 
Mkuu wangu, napata tabu kidogo naomba uniweke sawa anakwenda kusoma halafu World Bank wanamlipa pesa kwa kusoma tu?

Mkuu,

Ndinani bado hana exposure anafikiria fellowship za World Bank ni kama zile fullbright fellowship za watu kwenda kusoma. Hizi zinaitwa research fellowship mtu anakuwa anaajiriwa kwa muda maalum afanye kazi ya utafiti amalize. Wanakuwa wanamlipa mshahara, na marupurupu mengineyo kama staff member wa kitengo husika.

La kuchekesha mtu tayari ana PhD ya Economics kuna kitu gani cha zaidi anaenda kusomeshwa World Bank? Isitoshe World Bank navyojua mie ni Taasisi ya benki ya maendeleo ya kidunia sijui walibadilisha hiyo hali na kuwa chuo kikuu.
 
Mkuu,
Ndinani bado hana exposure anafikiria fellowship za World Bank ni kama zile fullbright fellowship za watu kwenda kusoma. Hizi zinaitwa research fellowship mtu anakuwa anaajiriwa kwa muda maalum afanye kazi ya utafiti amalize. Wanakuwa wanamlipa mshahara, na marupurupu mengineyo kama staff member wa kitengo husika.
La kuchekesha mtu tayari ana PhD ya Economics kuna kitu gani cha zaidi anaenda kusomeshwa World Bank? Isitoshe World Bank navyojua mie ni Taasisi ya benki ya maendeleo ya kidunia sijui walibadilisha hiyo hali na kuwa chuo kikuu.
Mkuu Mdondoaji,
Ha ha ha ha ha!! Inabidi wakati mwingine nicheke halafu huwa namkumbuka sana Mwalimu Nyerere!
 
Back
Top Bottom