Mohammed Hamad
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 3,988
- 1,304
Mkuu matumizi mabaya ya rasilimali za umma yamekita mizizi hata ndani ya bunge.
Si bunge lililopita tu bali mabunge yote tokea mfumo wa vyama vingi uanze na kabla ya hapo. Hoja ya kutetea masilahi yao ndiyo pekee uwaunganisha bila kujali wapinzani na ccm.
Kwanza walishajinoneshea malipo na bado hata leo wanasema hawalipwi vizuri inavyotakiwa. Bila aibu utasikia wanajilinganisha na wabunge wenzao wa nchi nyingine. Hii tabia ya kujilinganisha na wa nchi nyingine ni ujinga mkubwa kwa sababu kama nyie (wabunge) mnajilinganisha na wabunge wa nchi nyingine katika masilahi yenu mbona hamtulinganishi nasi wananchi katika huduma za msingi tunazopata kutoka serikalin na huduma za msingi wanazopata wananchi wa uko ulaya! This is unfair
Ebu ajitokeze mbunge yeyote aeleze ni kwanini wanalipwa Tsh. 2500/= kwa lita ya mafuta wakati mafuta siku zote mafuta uuzwa chini ya 2500/=. Kama hiyo ni haki mbona idara za serikali hawapangiwe flat rate kama hiyo. HUU NI UFISADI MKUBWA, na kudhihirisha hilo utaona kwa sasa mafuta yakifika 2500 watasema hela iongezeke manake haitoshi.
Wabunge tuelezenin kwanini msilipwe kwa gharama halisi namtoe risti za manunuzi? Wa DSM anunuae mafuta kwa 1700/= na Kigoma anunue kwa 2100/=
Je tumesahau walivyomshambulia Dr. Slaa kwa pamoja pale alipotaka marupurupu ya wabunge yapunguzwe? Huenda ndiyo maana wananchi walionekana kumshabikia sana Dr. Slaa!
MWISHO;
Inapokuja kwenye ufisadi watanzania karibia wote nguo iliyokatwa kwenye kitambaa kimoja!
TAFAKARI!