Polisi wauaji kasulu hatimaye watoroka

mwandiga

JF-Expert Member
Dec 5, 2011
1,506
661
Hii habari niliisikia kama tetesi siku ya ijumaa tarehe 2/3/2012 kwa kuwa nilikuwa nadai vihela vyangu huko Kasulu na niliahidiwa kuzipata Jumatatu nilifunga safari Ijumaa na kufika jioni na kufanya ufukunyunyu wa kujua ukweli wa hii habari. niliyobaini ni kama ifuatavyo.
Wale askari kama tisa hivi walioua mwananchi maeneo ya Rungwe Mpya mwaka jana walitoka lock up na kuwa mtaani, baadaye walipata uhamisho wa kwenda Kigoma na Kibondo lakini baada ya Mbunge wa Kasulu Mjini mwalimu Machari na Mhe. Mkosamali kukomalia hawa wauaji wachukuliwe hatua na sio kuhamishwa, uhamisho wao ukasitishwa mara moja ila waliohama kituo cha kasulu ni OCD, OCID NA OCS na tayari wengine wapya wamekuja wawili kati yao nilikuwa nao hapa town kigoma. Baada ya uhamisho huo kusitishwa hawa polisi wakawa mtaani tu ila wakapata habari kutoka Kigoma kuwa wanatakiwa wakamatwe. Kilichotokea ni wote kutoroka usiku wa manane wengine wakiondoka na wake zao na wengine wakiwaacha. Wake zao nimeonyeshwa walipo sehemu zao za biashara kwa wale waliobaki.
Hivi kweli hapa kulikuwa na dhamira ya dhati kuwaadhibu hawa polisi? Ndio maana kila siku wanaua raia na hawachukuliwi hatua wanachofanya ni kulindana tu. Hongera polisi Tabora kwa kuonyesha mfano mzuri wa kuwafunza tabia polisi wenye tabia za kuua ovyo raia
 
Ndugu yangu hii ndiyo Tanzania.

Kulindana kila sehemu kwani hapa aliyeua ni Polisi na anayekwenda kumkamata mhalifu ni Polisi. Hapa haki haiwezi kupatikana.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Ndugu yangu hii ndiyo Tanzania.

Kulindana kila sehemu kwani hapa aliyeua ni Polisi na anayekwenda kumkamata mhalifu ni Polisi. Hapa haki haiwezi kupatikana.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Inauma? nini inauma? Mnakaa kama maboga mnasema inauma? Na itawawauma kwelikweli japo haina meno. Mmezidi undondocha enyi watanzania. Nafuu ya pundamilia kule manyara wanapigania haki zao kuliko watanzania. Mpaka mtakapojua umuhimu wa kuwafurumusha Kikwete Pinda na genge lao, hata kwa mawe ikipidi, mtaendelea kukiona kilichomnyoa kanga manyoya ya shingo
 
Inauma? nini inauma? Mnakaa kama maboga mnasema inauma? Na itawawauma kwelikweli japo haina meno. Mmezidi undondocha enyi watanzania. Nafuu ya pundamilia kule manyara wanapigania haki zao kuliko watanzania. Mpaka mtakapojua umuhimu wa kuwafurumusha Kikwete Pinda na genge lao, hata kwa mawe ikipidi, mtaendelea kukiona kilichomnyoa kanga manyoya ya shingo

We si mtanzania?,unakichaa kweli wewe,kama hujui kujenga hoja acha kutuchefua na maneno ya kwenye taarabu...
 
Inauma? nini inauma? Mnakaa kama maboga mnasema inauma? Na itawawauma kwelikweli japo haina meno. Mmezidi undondocha enyi watanzania. Nafuu ya pundamilia kule manyara wanapigania haki zao kuliko watanzania. Mpaka mtakapojua umuhimu wa kuwafurumusha Kikwete Pinda na genge lao, hata kwa mawe ikipidi, mtaendelea kukiona kilichomnyoa kanga manyoya ya shingo
Na kweli,watanzania wamezidi ukunguruu,acha wakomeshwe
 
Hawa askari kweli wametoroka. Nilikuwa bar ya hawa maaskari inaitwa mkoromboko.wametoroka awapo na haijulikani wameenda wapi. Ninaowajua ni musa,shamsi, bonge. Mauaji haya ni kweli yanahusu raia wa rungwe.haijajulikana siri ilivuja vp had wakasepa.
 
mimi huwa nawaambia, siku JWtz,watakapochukua nchi hii,Polisi wote watavaa kanga mitaani,na itakuwa kiama kwao, maana wanajifanya miungu watu,wanaua raia kama kuku,
 
mimi huwa nawaambia, siku JWtz,watakapochukua nchi hii,Polisi wote watavaa kanga mitaani,na itakuwa kiama kwao, maana wanajifanya miungu watu,wanaua raia kama kuku,
Hilo halipo mkuu wangu! Pengine hujui miundo ya majeshi yetu! Uasi unaweza kutokea lakini utazua vita tu na hiyo itashirikisha majeshi yote kwa mfumo tulionao!
 
Achen kukurupuka hakuna m2 alotoroka
Wewe ndio unakurupuka au ni mhusika a.k.a muuaji? Unataka niwataje majina kisha uniambie wako wapi? Ila nimesikia tetesi wapo 2 waliorudi wakanaswa wapo ndani lock up. Nimeambiwa mke wa mmojawapo waliotoroka wote yupo Kasulu tena mjamzito, bado sijajua ukweli wa hili ila nitarudi hapa na taarifa kamili
 
Hawa askari kweli wametoroka. Nilikuwa bar ya hawa maaskari inaitwa mkoromboko.wametoroka awapo na haijulikani wameenda wapi. Ninaowajua ni musa,shamsi, bonge. Mauaji haya ni kweli yanahusu raia wa rungwe.haijajulikana siri ilivuja vp had wakasepa.

Simple tu mkuu,wakati mlikuwa mnawaona jalada lilikuwa limepelekwa kwa DPP, aliporejesha majibu kwamba wakamatwe na kushtakiwa kwa murder mlolongo ambao umeanzia makao makuu Polisi Dar,walishastuliwa na ndo maana wakasepa,kimsingi hakuna cha kusepa maana taarifa zao zajulikana,ni kulindana tu
 
Hawa askari kweli wametoroka. Nilikuwa bar ya hawa maaskari inaitwa mkoromboko.wametoroka awapo na haijulikani wameenda wapi. Ninaowajua ni musa,shamsi, bonge. Mauaji haya ni kweli yanahusu raia wa rungwe.haijajulikana siri ilivuja vp had wakasepa.
Umenena mkuu, japo kuna mmoja alisema nimekurupuka hawa jamaa hawajatoroka. Nikufahamishe kidogo hiyo baa imeshauzwa na mmiliki sasa hivi ni askari polisi wa hapa kigoma mjini ila nadhani kuna watakaokuwa wanamsaidia kusimamia huko Ksl.
 
Achen kukurupuka hakuna m2 alotoroka
Ulisema tunakurupuka sasa hapa mkurupakaji atajulikana ni nani, Hizi ni updates nzuri sana na zimenifurahisha japo kidogo. Soma kwa makini hapa chini nilivyokurupuka tena


Na. Pardon Mbwate na Felister Elias wa Jeshi la Polisi Kigoma
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Kihenya Kihenya amesema sambamba na hayo askari polisi saba wameweza kufikishwa mahakama ya hakimu mkaazi wa kigoma wakikabiliwa na mashitaka mauaji. maelezo ya matukio hayo ni kama ifuatavyo-
Kamanda huyo amesema Askari wame kufikishwa mahakamani kwa tuhuma ya mauaji tarehe 16/03/2012 Askari saba wa Wilaya ya Kasulu walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Mkoa wa kigoma wakikabiliwa na tuhuma za mauaji.Askari hao wanatuhumiwa Kusababisha kifo cha Festo Stephano Sekaino mkazi wa Kijiji cha runwempya Wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma ,tukio ambalo linalodaiwa kutokea mnamo tarehe 06/08/2011. askari waliofikishwa mahakamani ni: Baraka Hongoli mkaguzi, D 9200 cpl Mawazo Mohamed, F.8252 d/cpl Swahibu Kalaghe, E.9409 pc Charles Weleka, F5276 d/c Shamsi Lung'uno, G. 1659 pc Jerry Dawson, G, 2699 pc Amrani Rajabu. pia kuna askari wawili ambao ni F.6677 d/c Musa Wilfred na G.2663 d/c Adili Mshana. hawajapatikana na juhudi za kuwatafuta zinaendelea.




Hawa wawili hawakurudi kabisa, hao walionaswa walidanganywa mambo yameisha wakajileta kama serikali ni yao wakanaswa, Gooooooooooooood!!!!!!!!
 
Mkuu hujakurupuka nadhani huyo bwana alikuwa na,lake japo.Alikuwa kamtumwa lakini ajue wazi watu wanayajua mambo zaidi anavyodhani.
 
Mkuu hujakurupuka nadhani huyo bwana alikuwa na,lake japo.Alikuwa kamtumwa lakini ajue wazi watu wanayajua mambo zaidi anavyodhani.
Mkuu hapo umenena, ukiwa mwana JF huwezi kukurupuka, unajipanga hasa ndio unaingia. Kwa kuwa alitumwa hajarudi hadi sasa au unawezekana ni mmoja wa walinaswa na hapa bangwe hawapewi muda wa kuzurura nje kama walivyokuwa kule kasulu. Narudi KGM next wk nitakuwa mahakamani kila siku, Dar washkaji wanafurahi sana jamaa wamenaswa
 
Wewe ndio unakurupuka au ni mhusika a.k.a muuaji? Unataka niwataje majina kisha uniambie wako wapi? Ila nimesikia tetesi wapo 2 waliorudi wakanaswa wapo ndani lock up. Nimeambiwa mke wa mmojawapo waliotoroka wote yupo Kasulu tena mjamzito, bado sijajua ukweli wa hili ila nitarudi hapa na taarifa kamili
xo mbona unakurupuka na unaongea habri ambzo hazna kichwa wala miguu achen majungu...'we co msemaj we 2lia maneno maneno by queen drne
 
Ulisema tunakurupuka sasa hapa mkurupakaji atajulikana ni nani, Hizi ni updates nzuri sana na zimenifurahisha japo kidogo. Soma kwa makini hapa chini nilivyokurupuka tena


Na. Pardon Mbwate na Felister Elias wa Jeshi la Polisi Kigoma
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SSP Kihenya Kihenya amesema sambamba na hayo askari polisi saba wameweza kufikishwa mahakama ya hakimu mkaazi wa kigoma wakikabiliwa na mashitaka mauaji. maelezo ya matukio hayo ni kama ifuatavyo-
Kamanda huyo amesema Askari wame kufikishwa mahakamani kwa tuhuma ya mauaji tarehe 16/03/2012 Askari saba wa Wilaya ya Kasulu walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Mkoa wa kigoma wakikabiliwa na tuhuma za mauaji.Askari hao wanatuhumiwa Kusababisha kifo cha Festo Stephano Sekaino mkazi wa Kijiji cha runwempya Wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma ,tukio ambalo linalodaiwa kutokea mnamo tarehe 06/08/2011. askari waliofikishwa mahakamani ni: Baraka Hongoli mkaguzi, D 9200 cpl Mawazo Mohamed, F.8252 d/cpl Swahibu Kalaghe, E.9409 pc Charles Weleka, F5276 d/c Shamsi Lung’uno, G. 1659 pc Jerry Dawson, G, 2699 pc Amrani Rajabu. pia kuna askari wawili ambao ni F.6677 d/c Musa Wilfred na G.2663 d/c Adili Mshana. hawajapatikana na juhudi za kuwatafuta zinaendelea.




Hawa wawili hawakurudi kabisa, hao walionaswa walidanganywa mambo yameisha wakajileta kama serikali ni yao wakanaswa, Gooooooooooooood!!!!!!!!

xo m naamin wenyewe wanaakil zaid yako...''2lia man acha pyepyepyepye..'
 
Mkuu hujakurupuka nadhani huyo bwana alikuwa na,lake japo.Alikuwa kamtumwa lakini ajue wazi watu wanayajua mambo zaidi anavyodhani.

Sijakurupuka joe...'na wala cna llte jambo bur mda mwingne 2we 2nafikiria..'nn maana ya m2 kupelekwa mahakaman..,'achen mambo ya kizaman bana..'nyie ndo mnaomdic lulu kammaliz the great..'
 
This is unnecessary panic of the people who use to leave in past rather than the present.@Mtazamo,kama polisi watavaa khanga jiulize wewe itakuwaje?Uczungumzie tu jeshi kuchukua nchi ukadhan polisi itawacost. Angalia Mali pale nani inamcost.
 
Back
Top Bottom