MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Nimesoma kwa masikitiko makubwa kuhusu kijana, mwanaume, Mtanzania, aliyefariki baada ya kukamatwa na kuhojiwa na Polisi, hatimaye kufariki akiwa hospitalini, baada ya mateso aliyoyapata akiwa mikononi mwa Polisi kumzidia, hatimaye mauti kumfikia.
Habari hii imenikumbusha - na kunitia uchungu - yale yaliyowakuta wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge, waliouwawa na askari Polisi, na tume iliyoundwa na Rais Kikwete kuwatia hatiani. Lakini vipengele tata vya sheria viliwaweka huru akina Zombe na wenzake.
Nauliza, askari polisi watatesa na kuaa raia hadi lini? Huu ni ukiukwaji mkubwa wa Katiba juu ya Haki ya Kuishi ya raia, kwani Katiba imeweka wazi juu ya haki hii.
Hakuna askari polisi mwenye haki ya kuua raia, wala kutoa adhabu yoyote ile kwa raia, ikiwa ni wakati wa mahojiano au upelelezi wa kesi. Lakini Serikali imekuwa ikiyafumbia macho na masikio matukio haya ya ukiukwaji mkubwa wa haki, katiba na sheria.
Masikini, Mussa Juma amepoteza maisha yake mikononi mwa polisi, waliokula kiapo cha kuwalinda raia na mali zao. Leo polisi ndio wanaokuwa wa kwanza kabisa kuwaua raia! Je, hii ni haki?
Kwako Rais wetu, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete. Nakuomba uwawajibishe Makamanda Wakuu wa Mikoa yote ya Kipolisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ili kulinda heshima ya Jeshi la Polisi, kwani sasa, sisi wananchi hatuna imani nalo.
Pia, nakuomba uunde Tume ili kuchunguza kwa undani mauaji haya ya binadam huyu asiye na hatia.
Ukweli ni kwamba, wako askari WABAYA sana ndani ya Jeshi hilo, wanaoshirikiana moja kwa moja na wahalifu, wakiwalea na kuwafuga, kwa kuwa ushirika huo ni haramu wenye malengo ya maslahi binafsi, jambo ambalo ni ufisadi mkubwa kabisa!
TUNATAKA HAKI ITENDEKE! Rais, TIMIZA WAJIBU WAKO!
./Mwana wa Haki
Habari hii imenikumbusha - na kunitia uchungu - yale yaliyowakuta wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge, waliouwawa na askari Polisi, na tume iliyoundwa na Rais Kikwete kuwatia hatiani. Lakini vipengele tata vya sheria viliwaweka huru akina Zombe na wenzake.
Nauliza, askari polisi watatesa na kuaa raia hadi lini? Huu ni ukiukwaji mkubwa wa Katiba juu ya Haki ya Kuishi ya raia, kwani Katiba imeweka wazi juu ya haki hii.
Hakuna askari polisi mwenye haki ya kuua raia, wala kutoa adhabu yoyote ile kwa raia, ikiwa ni wakati wa mahojiano au upelelezi wa kesi. Lakini Serikali imekuwa ikiyafumbia macho na masikio matukio haya ya ukiukwaji mkubwa wa haki, katiba na sheria.
Masikini, Mussa Juma amepoteza maisha yake mikononi mwa polisi, waliokula kiapo cha kuwalinda raia na mali zao. Leo polisi ndio wanaokuwa wa kwanza kabisa kuwaua raia! Je, hii ni haki?
Kwako Rais wetu, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete. Nakuomba uwawajibishe Makamanda Wakuu wa Mikoa yote ya Kipolisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ili kulinda heshima ya Jeshi la Polisi, kwani sasa, sisi wananchi hatuna imani nalo.
Pia, nakuomba uunde Tume ili kuchunguza kwa undani mauaji haya ya binadam huyu asiye na hatia.
Ukweli ni kwamba, wako askari WABAYA sana ndani ya Jeshi hilo, wanaoshirikiana moja kwa moja na wahalifu, wakiwalea na kuwafuga, kwa kuwa ushirika huo ni haramu wenye malengo ya maslahi binafsi, jambo ambalo ni ufisadi mkubwa kabisa!
TUNATAKA HAKI ITENDEKE! Rais, TIMIZA WAJIBU WAKO!
./Mwana wa Haki