Rutunga M
JF-Expert Member
- Mar 16, 2009
- 1,769
- 1,382
Taarifa za hivi punde kutoka Bukoba ni kuwa polisi wawili waliokuwa na tabia ya kuzizia wananchi na kuwatoa rushwa wamevamiwa na wananchi kisha kupigwa mithiri ya vibaka kabla ya kuokolewa na wenzao katika harakati za mwisho mwisho za kuwaunguza kwa moto.
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Bukabuye wilayani Missenyi ambapo polisi hao kutoka kituo kikuuu cha polisi mjini Bukoba walikodi teksi kwa lengo la kwenda kuvizia wanaovusha kahawa ya magendo kwenda Uganda ili kuwatoa rushwa na kuwa hii ni tabia yao ya kila siku.
Kutokana na vitendo vyao wananchi walijikusanya wakazuia gari hilo kisha kuanza kuwapatia kipigo, kuvunjavunja gari kabla ya kukolewa na polisi wa kituo cha Kanyigo huko Missenyi.
Hivi sasa polisi mmoja amekimbia hajulikani alipo, ingawa wawili wapo hoi katika hospitali ya mkoa KAGERA.
Polisi wanafanya jitihada za kufanya gwaride ili wananchi wawatambue wengine ambao hawajajulikana.
Ni hayo .
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Bukabuye wilayani Missenyi ambapo polisi hao kutoka kituo kikuuu cha polisi mjini Bukoba walikodi teksi kwa lengo la kwenda kuvizia wanaovusha kahawa ya magendo kwenda Uganda ili kuwatoa rushwa na kuwa hii ni tabia yao ya kila siku.
Kutokana na vitendo vyao wananchi walijikusanya wakazuia gari hilo kisha kuanza kuwapatia kipigo, kuvunjavunja gari kabla ya kukolewa na polisi wa kituo cha Kanyigo huko Missenyi.
Hivi sasa polisi mmoja amekimbia hajulikani alipo, ingawa wawili wapo hoi katika hospitali ya mkoa KAGERA.
Polisi wanafanya jitihada za kufanya gwaride ili wananchi wawatambue wengine ambao hawajajulikana.
Ni hayo .