Polisi, wanahabari na serikali

astalavista

Senior Member
Jul 7, 2014
156
159
POLISI_WANAHABA RI_SERIKALI. Kwanza niweke wazi kwamba nina maslahi na Wanahabari,ndio nina maslahi nao kwasababu mimi pia ni mmoja wa familia hiyo.. Jana kwa mara nyingine Tanzania ilishuhudia uhusiano mbovu kati ya Wanahabari na Watu wa Usalama(Polisi) .

Kupitia vyombo mbalimbali vya habari nilishuhudia wanahabari wakiongea kwa uchungu kiasi cha kupelekea kutoa machozi kuafuatia kupigwa kwa baadhi ya wenzao..INAUMIZ A NA KUSIKITISHA. Lakini nataka kusema kitu kwa Wanahabari hapa nchini,muda mrefu tumekuwa tukilalamika kwamba Serikali inanyima uhuru kwa vyombo vya habari tofauti na ilivyo andikwa katika katiba (act18 Freedom of êxpression).

Nataka kusema tumekuwa tunasahau kupigia kelele vitu vingine muhimu ambavyo vitakua nyenzo rahisi zaidi katika ufanisi wetu wa kazi(mfano kwa tukio lile la jana). Kuna msemo mmoja kwa wanahabari kwamba kutembea bila ya kuwa na KALAMU na KARATASI ni sawa na Mwanajeshi kwenda vitani bila kuwa na SILAHA.

Hii kauli sio mbaya,lakini lazima tukumbushane kwamba kuna mazingira yanatubidi kuwa na zaidi ya Kalamu na Karatasi. Ukweli ni kwamba kwenye matukio ambayo yanakuwa na hali ya vurugu na hatari zisizojulikana kama yale ya jana ni ngumu kwa watu wa usalama kutambua yupi ni mwanahabari na yupi si mwanahabari.

Kwa jinsi hali ilivyo sasa kubeba kamera pekee haitoshi kuwashawishi wanausalama kutambua wanahabari,na kwa mazingira hayo ya vurugu tusitegemee watu wa usalama kuomba vitambulisho vya kazi(huo muda hakuna). Kufuatia tukio la jana na matukio mengine huko nyuma,nafikiri sasa wanahabari umefika wakati wa kupaza sauti kwa wahusika wa vyombo hivyo vya habari kupatiwa mavazi maalumu kwa shughuri malumu kama hizo.

'PRESS JACKET' tujiulize wangapi wanayo? Kina nani walivaa ama wanavaa katika matukio kama yale?Kwanini hatuna? Na je hayana umuhimu kweli?. Tukubali sasa kwamba hata kwa upande wetu kuna upungufu katika vitendea kazi. Hata wanajeshi wakienda vitani wanakuwa tofauti na siku za kawaida. Hata watu wa afya kuna mazingira wanakuwa tofauti na siku za kawaida(mf' wale wa Ebola).

Kwanini si wanahabari?
Tunafanya kazi kwa mazoea sana.

Wasallam.
 
Ni fedheha kubwa sana kuona askari kushambulia wana habari let me declare that am not among of them (waandishi) lakini mwili ulisisimka kuona kile kitendo, solution ni kugoma kuandika habari zao fulstop.
 
Vitendea kazi (kama hiyo sare maalumu) ni muhimu kwa wanahabari lakini matumizi ya nguvu kubwa kuliko maarifa (kwa upande wa wanausalama) ni kujenga chuki kwa jamii
 
Mmetumika sana kama kondomu na mmepoteza ladha ndio maana mnapigwa sasa acheni bahasha za kaki mtakuwa salama moyoni




polisi_wanahaba ri_serikali.
Kwanza niweke wazi kwamba nina
maslahi na wanahabari,ndio nina maslahi
nao kwasababu mimi pia ni mmoja wa
familia hiyo..

Jana kwa mara nyingine tanzania
ilishuhudia uhusiano mbovu kati ya
wanahabari na watu wa usalama(polisi) .

Kupitia vyombo mbalimbali vya habari
nilishuhudia wanahabari wakiongea kwa
uchungu kiasi cha kupelekea kutoa
machozi kuafuatia kupigwa kwa baadhi ya
wenzao..inaumiz a na kusikitisha.

Lakini nataka kusema kitu kwa
wanahabari hapa nchini,muda mrefu
tumekuwa tukilalamika kwamba serikali
inanyima uhuru kwa vyombo vya habari
tofauti na ilivyo andikwa katika katiba
(act18 freedom of êxpression).

Nataka kusema tumekuwa tunasahau
kupigia kelele vitu vingine muhimu
ambavyo vitakua nyenzo rahisi zaidi katika
ufanisi wetu wa kazi(mfano kwa tukio lile
la jana).

Kuna msemo mmoja kwa wanahabari
kwamba kutembea bila ya kuwa na
kalamu na karatasi ni sawa na
mwanajeshi kwenda vitani bila kuwa na
silaha.

Hii kauli sio mbaya,lakini lazima
tukumbushane kwamba kuna mazingira
yanatubidi kuwa na zaidi ya kalamu na
karatasi.

Ukweli ni kwamba kwenye matukio
ambayo yanakuwa na hali ya vurugu na
hatari zisizojulikana kama yale ya jana ni
ngumu kwa watu wa usalama kutambua
yupi ni mwanahabari na yupi si
mwanahabari.

Kwa jinsi hali ilivyo sasa kubeba kamera
pekee haitoshi kuwashawishi
wanausalama kutambua wanahabari,na
kwa mazingira hayo ya vurugu
tusitegemee watu wa usalama kuomba
vitambulisho vya kazi(huo muda hakuna).

Kufuatia tukio la jana na matukio mengine
huko nyuma,nafikiri sasa wanahabari
umefika wakati wa kupaza sauti kwa
wahusika wa vyombo hivyo vya habari
kupatiwa mavazi maalumu kwa shughuri
malumu kama hizo.

'press jacket' tujiulize wangapi wanayo?
Kina nani walivaa ama wanavaa katika
matukio kama yale?kwanini hatuna? Na je
hayana umuhimu kweli?.

Tukubali sasa kwamba hata kwa upande
wetu kuna upungufu katika vitendea kazi.
Hata wanajeshi wakienda vitani
wanakuwa tofauti na siku za kawaida.
Hata watu wa afya kuna mazingira
wanakuwa tofauti na siku za kawaida(mf'
wale wa ebola).

Kwanini si wanahabari?
Tunafanya kazi kwa mazoea sana.

Wasallam.
 
Ni fedheha kubwa sana kuona askari kushambulia wana habari let me declare that am not among of them (waandishi) lakini mwili ulisisimka kuona kile kitendo, solution ni kugoma kuandika habari zao fulstop.

wengi wao hawana taaluma ya habari, walifeli form 4.
 
Sijafurahishwa kupigwa kwa wanahabar ila nasema walistahili kupigwa,na huwa nasema hapa kinachowatesa waandish wa habar wa Tanzania ni 'NDOA NA WANASIASA',waandishi wanadharauliwa na waajiri wao(wamiliki),watawala serikalin na hata tabaka la watanzania wenye uelewa wa mambo,
naposema ndoa namaanisha iwe kwa watu wa chama tawala au upinzani,siku ya kuvunja hii ndoa na kujitambua hamtanyanyasika.Tangu auawe ndugu yenu Mwangos palepale mlipaswa kubadilika,hata polis wasingewachezea,kwa sababu Cover angejikuta anahutubia mabenchi kila anapotaka kuongea na journalists,
hamna umoja,
nimemsikia mmoja jana akisema 'MIMI MWANDISHI WA HABAR WA SERIKALI,NAANDIKIA DAILYNEWS,YAAN NAPIGWA?',sasa mwandish kama huyu ni zu.zu,kwa maana nyingine aliyepaswa kupigwa ni wa chombo binafsi????ndo maana mnanyonywa na kudharauliwa na politicianz kuliko hata sisi walim
 
Ni fedheha kubwa sana kuona askari kushambulia wana habari let me declare that am not among of them (waandishi) lakini mwili ulisisimka kuona kile kitendo, solution ni kugoma kuandika habari zao fulstop.

hawawez kugoma kwakua hawaijui nafas yao,kupigwa na kuuliwa kwa Mwangos kipi kinaumiza sana,waandish wenyewe ndo wanaolea upuuz huo,
 
Hivi kuna mtu anaamini wale waandishi walipigwa kwa bahati mbaya? Kwamba haikuwa rahisi kuwatambua? Kwamba wangevaa sare wasingepigwa? Believe that and you will believe anything! Wale askari walijua wanafanya nini na walichoagizwa ndicho walikitekeleza. Ni kwa bahati tu safari hii hawakumlipua mtu (RIP Mwangosi)...kulingana na Farijala Hussein ndivyo walivyofundishwa, kupiga wananchi!
 
Poleni sana wakuu waandishi , Polisi na mahakama vinatakiwa kufanyiwa mabadiliko makubwa ili vyombo hivi viweze kufanya kazi ipasavyo. sababu watumishi wa vyombo hivi wanadhani wapo kutumikia chama tawala na sio watanzania wote.
 
Hoja ni walipigwa kwakuwa hawana majacket ama?Hivi polisi walishindwa kuuliza vitambulisho vya kazi!Kifupi waliamua tu kufanya waliyoyafanya

siko kwa kuwatetea watu wa usalama Mkuu,lakini kwa mazingira kama yale kuulizana vitambulisho pekee siyo suluhisho..ndio maana nikapendekeza uwepo wa PRESS JACKET ambayo kwa kiasi kikubwa ingeweza kupunguza ama kuondoa kabisa hili tatizo.
 
Hoja ni walipigwa kwakuwa hawana majacket ama?Hivi polisi walishindwa kuuliza vitambulisho vya kazi!Kifupi waliamua tu kufanya waliyoyafanya
Unauliza vitambulisho vya kazi wahuni wanaotumiwa na wanasiasa wanaingia polisi kwa kuandamana kama wehu kwanza wamepigwa kidogo wangewapiga wawavunje viuno kabisa au kupasua vichwa ili wajue namna yamkufuata taratibu na sheria.
 
Chagonja ndie adui mkuu wa waandishi wa habari, na ndiye aliye waamrisha ni worse kulilo Kamuhanda
 
Back
Top Bottom