ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wakati mwingine askari polisi wa usalama barabarani wanashindwa kukaa barabarani badala yake wanajificha kwenye vibanda kuvizia madereva wafanye kosa ili waombe posho. Wiki iliyopita nilikuwa na jamaa mtukutu, aka "U-turn" kwenye mapishano ya kuingilia MNI Airport Dar katika barabara ya Nyerere, kumbe askari wa usalama barabarani wamejificha wanavizia posho, ghafla askari polisi akaibuka kwenye vibanda na kuanza kukimbilia barabarani klwa kasi ya ajabu akiwa na kofia mkononi ili kumpiga mkono, jamaa alipomwona akaongeza mwendo na kumwacha akiwa anapunga mkono tu huku kachama kinywa, kapoteza posho..
Leo naingia tena hapa Airport, ghafla naona Binti amevalia bluzi nyeupi na sketi ya kibluu ya khaki...anapunga mkono karibia na kuingia getini ambapo wateja wanachukulia kadi kwenye mashine ya kuruhusu kuingia uwanjani, nasimama kwa utii wa amri ya dola, nauliza ati kulikoni afande?..yupo siriasi anajibu ..nimekusimamisha nikukagee, mara anaomba tufungue milango ya gari..anaulizaz kwenye begi kuna nini.., anadai anataka kukagua mizigo..nauliza huu ukaguzi wan je ya geti umeanza lini?..anajibu nakagua , ni wajibu wetu ..hafungui begi anauliza nani anasafiri wewe au mkeo namwambia mimi..anataka kukagua pochi ya mamsapu ..namwambia wewe mbona ueleweki, unakagua nini?...anauliza..."naomba leseni yako'.." hasira zinanishika namjibu ..unanichelewesha..ebu sema unachotaka..anasema "leseni mzee" akisitasita, wakati huo huo magari mengine yanapita hayakaguliwi......hauliza mbona hayo hukagui? hana jibu...naishiwa uvumilivu namuuliza wewe unajuia kazi yako?..kwa hasira naondoa gari akiwa amesimama tu hana la kusema..eti huyu nae anataka rushwa kwenye geti..
Leo naingia tena hapa Airport, ghafla naona Binti amevalia bluzi nyeupi na sketi ya kibluu ya khaki...anapunga mkono karibia na kuingia getini ambapo wateja wanachukulia kadi kwenye mashine ya kuruhusu kuingia uwanjani, nasimama kwa utii wa amri ya dola, nauliza ati kulikoni afande?..yupo siriasi anajibu ..nimekusimamisha nikukagee, mara anaomba tufungue milango ya gari..anaulizaz kwenye begi kuna nini.., anadai anataka kukagua mizigo..nauliza huu ukaguzi wan je ya geti umeanza lini?..anajibu nakagua , ni wajibu wetu ..hafungui begi anauliza nani anasafiri wewe au mkeo namwambia mimi..anataka kukagua pochi ya mamsapu ..namwambia wewe mbona ueleweki, unakagua nini?...anauliza..."naomba leseni yako'.." hasira zinanishika namjibu ..unanichelewesha..ebu sema unachotaka..anasema "leseni mzee" akisitasita, wakati huo huo magari mengine yanapita hayakaguliwi......hauliza mbona hayo hukagui? hana jibu...naishiwa uvumilivu namuuliza wewe unajuia kazi yako?..kwa hasira naondoa gari akiwa amesimama tu hana la kusema..eti huyu nae anataka rushwa kwenye geti..