johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 84,031
- 142,090
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM komredi Polepole ataongea na waandishi wa habari kuanzia saa 10.00 jioni.
Kikubwa ni nidhamu ya kuzingatiwa kwa watia nia ya kugombea Ubunge na udiwani kwa tiketi ya chama tawala yaani chama dume CCM. Baba Lao.
Mkutano unafanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Updates;
Maendeleo hayana vyama!
===
Mh. Polepole ameanza kwa kueleza mafanikio waliyoyapata katika kutafuta Wagombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa Urais wa Zanzibar.
Kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Polepole amewashukuru Wanadodoma kwa kuwapokea vyema katika mji huo na Wajumbe wote waliofika katika mji huo kuwa na wakati mzuri sana na kuwafanya kumaliza mkutano wao kwa amani na mshikamano mkubwa.
Sambamba na hilo, Polepole amewashukuru Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kwa kumpa dhamana Mwenyekiti wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kugombea kwa kipindi kingine ili akaikamilishe kazi aliyoianza katika muhula wa kwanza.
Zaidi ya hayo, Polepole amewashukuru wasimamizi wa Uchaguzi kuanzia kwenye Halmashauri kuu kwa kazi waliyoifanya kuanzia kwenye mchakato wa kumpata Mgombea urais Zanzibar na Wasimamizi wa uchaguzi waliowezesha kumpata Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
Aidha, Polepole ameeleza kuwa kutokana na kuwapo kwa maswali mbalimbali yapo mambo mbalimbali ambayo chama kingependa kutoa ufafanuzi baada ya Uchaguzi wa Wagombea nafasi za Urais kukamilika.
Moja, Polepole amesema kuwa kumekuwepo na maswli mengi kuhusu gharama za fomu ya Wagombea wa Ubunge na Udiwani katika Chama cha Mapinduzi. Katika hili Polepole amesema kuwa "Chama cha Mapinduzi kinazuia michango holela kwakuwa chama hicho kinaongozwa kwa mujibu wa katiba na kanuni ambazo wamejiwekea. Hivyo, michango yote katika ngazi zote ni lazima kwanza ijadiliwe na ipitishwe na kamati ya siasa ya Halmashauri Kuu ya eneo husika".
Polepole ameongeza kuwa "licha ya kwamba kamati za siasa zina mamlaka ya kuweka mapendekezo ya michango hii, michango yoyote kwa Wanachama inabaki wakati wote kuwa ni michango ya hiari, ni marufuku Mwanaccm kulazimishwa kuchanga mchnango kwenye chama chetu. Mwanaccm anayeamini ana mchango anapenda kujitoa kwenye chama chetu afanye hivyo kwa hiari yake mwenyewe".
Polepole amesisitiza kuwa "kamwe, katu na asilani mchango usiwe kigezo cha kumpa au kumyima Mgombea fomu, Wagombea Wapewe fomu sawasawa na viwango vilivyoainishwa katika kanuni. Na mtu akishapewa fomu yake mnaweza kumweleza Chama kimepitisha harambee. kwahiyo wanachama wote wanakaribishwa kuchangia. Sasa iwe hiari yake kuchangia au kutokuchangia, ndani ya vikao tutajua huyu amejitoa kwenye chama na huyu hajitoi lakini kamwe isitumike kumkubalia mtu kupata fomu au kumkatalia."
Aidha akifafanua kuhusu viwango vya kuchukua fomu mbalimbali, Polepole ameeleza fomu ya udiwani kwa ngazi ya kata ni Shilingi elfu kumi tu (10,000/=), fomu ya Ubunge au Uwakilishi kwa Zanzibar ni Shilingi laki moja tu (100,000/=) lakini hii haizuii kamati ya siasa kuweka michango lakini si lazima.
Kwa upande wa fomu za Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Wawakilishi ni shilingi laki tano tu (500,000/=) wakati fomu za Urais ni shilingi milioni moja (1,000,000/=)
Pili, Polepole ameeleza jambo lingine lililofanyiwa mabadiliko katika katiba hiyo ni kupanua wigo wa demokrasia. Katika hili ameeleza kuwa Mkutano mkuu wa kata ambao awali ulijumuisha watu wachache kwa sasa utajumuisha pia Wajumbe wapya wanaoingia katika kikao hicho ambao pia ni Wenyeviti wa mashina yote katika kata husika ambao wanajulikana pia Mabalozi na wana dhamana ya kupiga kura za maoni.
Kwa upande wa ngazi ya Jimbo au Uwakilishi, Wataanza na Mkutano Mkuu wa jimbo ambapo katika Mkutano huo Wagombea wote wataingia na wataeleza kwanini wanataka kupewa dhamana ya Ugombea kupitia CCM kisha kamati za siasa za ngazi mbalimbali zitafuata utaratibu kwa kuweka mapendekezo mpaka kufikia Halmashauri Kuu ya taifa ambalo ndiyo itaamua jina moja.
Polepole ameeleza wamejifunza kutoka katika mchakato wa kupata Ugombea wa Urais walioufanya hivi karibuni. Kutokana na kujifunza huko ameeleza kuwa mchakato wa upigaji kura katika chama hicho utakuwa wa wazi ili kuepusha masononeko. Hivyo, wanataka uchaguzi ndani ya chama hicho kuwa huru na haki.
Sambamba na hilo, Polepole ameeleza utaratibu wa mawasiliano ndani ya chama na kubainisha kuwa hivi karibuni wataeleza sehemu ambapo taarifa za uchaguzi zitapatikana
Akisoma kipengele cha kanuni ya uongozi wa maadili ya chama kwa upande wa haki za Wanachama ukurasa wa (18) Polepole amesema Mwanachama atakuwa na haki ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi endapo kugombea nafasi nyingi kuitasababisha kuzorota kwa uhai wa Chama hatateuliwa.
Aidha, Polepole ametahadharisha Wagombea na watia nia kufanya vitendo ambavyo vinakatazwa na Chama ikiwemo kuweka mabango na kutumia vipeperushi na kupost kutia nia kuwa haviruhusiwi kwani ni sawa na kuanza kampeni kabla ya wakati wake.
Aidha, Polepole ameeleza ratiba ya Uchukuaji, urejeshaji fomu pamoja na mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali katika chama hicho kama ifuatavyo:
Kikubwa ni nidhamu ya kuzingatiwa kwa watia nia ya kugombea Ubunge na udiwani kwa tiketi ya chama tawala yaani chama dume CCM. Baba Lao.
Mkutano unafanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Updates;
Maendeleo hayana vyama!
===
Mh. Polepole ameanza kwa kueleza mafanikio waliyoyapata katika kutafuta Wagombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa Urais wa Zanzibar.
Kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Polepole amewashukuru Wanadodoma kwa kuwapokea vyema katika mji huo na Wajumbe wote waliofika katika mji huo kuwa na wakati mzuri sana na kuwafanya kumaliza mkutano wao kwa amani na mshikamano mkubwa.
Sambamba na hilo, Polepole amewashukuru Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa kwa kumpa dhamana Mwenyekiti wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kugombea kwa kipindi kingine ili akaikamilishe kazi aliyoianza katika muhula wa kwanza.
Zaidi ya hayo, Polepole amewashukuru wasimamizi wa Uchaguzi kuanzia kwenye Halmashauri kuu kwa kazi waliyoifanya kuanzia kwenye mchakato wa kumpata Mgombea urais Zanzibar na Wasimamizi wa uchaguzi waliowezesha kumpata Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
Aidha, Polepole ameeleza kuwa kutokana na kuwapo kwa maswali mbalimbali yapo mambo mbalimbali ambayo chama kingependa kutoa ufafanuzi baada ya Uchaguzi wa Wagombea nafasi za Urais kukamilika.
Moja, Polepole amesema kuwa kumekuwepo na maswli mengi kuhusu gharama za fomu ya Wagombea wa Ubunge na Udiwani katika Chama cha Mapinduzi. Katika hili Polepole amesema kuwa "Chama cha Mapinduzi kinazuia michango holela kwakuwa chama hicho kinaongozwa kwa mujibu wa katiba na kanuni ambazo wamejiwekea. Hivyo, michango yote katika ngazi zote ni lazima kwanza ijadiliwe na ipitishwe na kamati ya siasa ya Halmashauri Kuu ya eneo husika".
Polepole ameongeza kuwa "licha ya kwamba kamati za siasa zina mamlaka ya kuweka mapendekezo ya michango hii, michango yoyote kwa Wanachama inabaki wakati wote kuwa ni michango ya hiari, ni marufuku Mwanaccm kulazimishwa kuchanga mchnango kwenye chama chetu. Mwanaccm anayeamini ana mchango anapenda kujitoa kwenye chama chetu afanye hivyo kwa hiari yake mwenyewe".
Polepole amesisitiza kuwa "kamwe, katu na asilani mchango usiwe kigezo cha kumpa au kumyima Mgombea fomu, Wagombea Wapewe fomu sawasawa na viwango vilivyoainishwa katika kanuni. Na mtu akishapewa fomu yake mnaweza kumweleza Chama kimepitisha harambee. kwahiyo wanachama wote wanakaribishwa kuchangia. Sasa iwe hiari yake kuchangia au kutokuchangia, ndani ya vikao tutajua huyu amejitoa kwenye chama na huyu hajitoi lakini kamwe isitumike kumkubalia mtu kupata fomu au kumkatalia."
Aidha akifafanua kuhusu viwango vya kuchukua fomu mbalimbali, Polepole ameeleza fomu ya udiwani kwa ngazi ya kata ni Shilingi elfu kumi tu (10,000/=), fomu ya Ubunge au Uwakilishi kwa Zanzibar ni Shilingi laki moja tu (100,000/=) lakini hii haizuii kamati ya siasa kuweka michango lakini si lazima.
Kwa upande wa fomu za Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Wawakilishi ni shilingi laki tano tu (500,000/=) wakati fomu za Urais ni shilingi milioni moja (1,000,000/=)
Pili, Polepole ameeleza jambo lingine lililofanyiwa mabadiliko katika katiba hiyo ni kupanua wigo wa demokrasia. Katika hili ameeleza kuwa Mkutano mkuu wa kata ambao awali ulijumuisha watu wachache kwa sasa utajumuisha pia Wajumbe wapya wanaoingia katika kikao hicho ambao pia ni Wenyeviti wa mashina yote katika kata husika ambao wanajulikana pia Mabalozi na wana dhamana ya kupiga kura za maoni.
Kwa upande wa ngazi ya Jimbo au Uwakilishi, Wataanza na Mkutano Mkuu wa jimbo ambapo katika Mkutano huo Wagombea wote wataingia na wataeleza kwanini wanataka kupewa dhamana ya Ugombea kupitia CCM kisha kamati za siasa za ngazi mbalimbali zitafuata utaratibu kwa kuweka mapendekezo mpaka kufikia Halmashauri Kuu ya taifa ambalo ndiyo itaamua jina moja.
Polepole ameeleza wamejifunza kutoka katika mchakato wa kupata Ugombea wa Urais walioufanya hivi karibuni. Kutokana na kujifunza huko ameeleza kuwa mchakato wa upigaji kura katika chama hicho utakuwa wa wazi ili kuepusha masononeko. Hivyo, wanataka uchaguzi ndani ya chama hicho kuwa huru na haki.
Sambamba na hilo, Polepole ameeleza utaratibu wa mawasiliano ndani ya chama na kubainisha kuwa hivi karibuni wataeleza sehemu ambapo taarifa za uchaguzi zitapatikana
Akisoma kipengele cha kanuni ya uongozi wa maadili ya chama kwa upande wa haki za Wanachama ukurasa wa (18) Polepole amesema Mwanachama atakuwa na haki ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi endapo kugombea nafasi nyingi kuitasababisha kuzorota kwa uhai wa Chama hatateuliwa.
Aidha, Polepole ametahadharisha Wagombea na watia nia kufanya vitendo ambavyo vinakatazwa na Chama ikiwemo kuweka mabango na kutumia vipeperushi na kupost kutia nia kuwa haviruhusiwi kwani ni sawa na kuanza kampeni kabla ya wakati wake.
Aidha, Polepole ameeleza ratiba ya Uchukuaji, urejeshaji fomu pamoja na mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali katika chama hicho kama ifuatavyo: