Poleni Watanganyika, poleni sana

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,638
697,929
Tuuweke unafique kando! Tunapaswa kujitathmini upya
Sisi ni wanafiki. (Kupitia bunge hilo limethibitika
Sisi ni waoga na wazito kuchukua maamuzi magumu
Sisi ni waongeaji sana kuliko watendaji (keyboard warriors)
Sisi ni makuwadi (huu ukweli mchungu)
Sisi ni wabinafsi
Sisi ni waongo sana
Sisi si wamoja na hatuna umoja
Sisi hatuna uzalendo na hatujanyooka

Leo hii kuna Tanzania na kuna Zanzibar! Nyeusi tuite nyeusi jamani.. Je Tanganyika iko wapi? Imebaki kwenye makabrasha ya kumbukumbu ghalani.

Suala la kuuza/kugawa/kubinafsisha bandari zetu zote za Tanganyika ya makaratasi, limetuacha uchi na kuthibitisha sisi ni watu wa namna gani.

Wenzetu ndugu zetu na jirani zetu Zanzibar wametuzodoa, wametubeza, wametupasha, wametukejeli na kutucheka sana humu mitandaoni. Wametupa majina mengi mabaya na ya kukarahisha sana! TUNASTAHILI!

Tumejawa na unyonge na unafiki wa ajabu kabisa! Hatuna mbele hatuna nyuma kama sigara kali! Nyuma ni mbele na mbele ni kama nyuma. Tukiwashwa mbele nyuma tunavutika! Tukiwashwa nyuma mbele tunavutika!

Jana kilichoitwa kikao cha viongozi wa dini kimetoa mwelekeo mpya mpya kwenye hili sakata! Kimepangua na kufisha hoja zote zilizotumiwa na bunge kukubaliana na kile kilichokuwa kimepangwa na wenye ajenda zao!

Nyeusi tuite nyeusi, kikao kile pamoja na kuitwa ni kikao cha viongozi wa dini.. Lakini kiuhalisia RC ndio ilikuwa kila kitu kwenye kile kikao, kuanzia maandalizi, mipango, hoja mpaka wayforward ya nini kifanyike baada ya hapo! Kuna taasisi bado zitabaki kuwa juu miongo mingi ijayo kutokana na elimu! Na ndio maana EL alisisitiza sana elimu.

Bunge letu! a laughing stock of the century tusiwaseme vibaya marehemu kwakuwa hawapo kujitetea lakini tukumbuke nyayo zao zinaishi kila walikopita! Tusingekuwa na bunge la namna hii kama kuna watu wasingekuwa na fikra finyu maono kimo cha mbilikimo!

Watetezi wa uwekezaji kandamizi wa kinyonyaji na kitapeli, wameokotezwa huko na huko na kupewa chochote kulingana na hadhi zao (price tags) lakini zisikilize hoja zao sasa! Sio hoja ni vioja! Wanapiga tu kelele na kupayuka kama mahoka kwa sangoma! Cha kushangaza wamepata uungwaji mkono na wajinga wengi.

Viongozi na wanasiasa walioko madarakani! Hawa sijui wanawaza nini! Au ndio ule usemi shibe mwana malevya? Hakuna hata mmoja aliyejitokeza waziwazi na kusema kwa sauti thabiti HILI HALIFAI! wote wanaishia kunong'ona mafichoni tena kwa sauti ya woga! Hawatuwazii sisi, hawaliwazii taifa! Wanajiwazia wao na matumbo yao na familia zao.

Poleni Watanganyika! Poleni sana! Kuna tabaka la wapigaji walioamua kujimilikisha hii nchi, ubinafsi na unafiki wetu na woga wetu vimetufanya tuwaache wakue na kujijenga kwa nguvu mno! Sasa hawagusiki tena! Na kamwe hawajitokezi hadharani bali huwatumia makuwadi na vibaraka wao tangu juu mpaka chini kabisa, kila mahali na kila penye mikono ya uamuzi.. NA WOTE HAO NI WATANGANYIKA WENZETU.

Tusiwalaumu wezi tuwalaumu waliowaonesha wezi mlango wa kuingilia huku wakiwalinda ili waweze kuiba nyumbani kwetu bila kukamatwa.

Poleni watanganyika! Tumeziona rangi zetu halisi


20230613_083223.jpg
 
Back
Top Bottom