Waziri Mkuu Mizengo Pinda anaondoka Dar es Salaam leo usiku kwenda Geneva, Uswisi kumwakilisha Rais Jakaya Kikwete kwenye Mkutano Mkuu wa Shirika la Mawasiliano la Kimataifa (International Telecommunication Union ITU).
Pinda atafuatana na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msola.
Mkutano huo utajadili wajibu mkubwa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kuendeleza uchumi. Katika mkutano huo kutakuwa na kikao maalum cha wakuu wa nchi.
Serikali inatilia mkazo uendelezaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini kwa ajili ya kuleta maendeleo ya kiuchumi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Pinda atafuatana na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msola.
Mkutano huo utajadili wajibu mkubwa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika kuendeleza uchumi. Katika mkutano huo kutakuwa na kikao maalum cha wakuu wa nchi.
Serikali inatilia mkazo uendelezaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano nchini kwa ajili ya kuleta maendeleo ya kiuchumi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI