Picha - Uamsho Zanzibar ngangari hadi kieleweke

303313_10150805900486176_721596175_9887001_1467272456_n.jpg
 
At4NPC6CIAEToKH.jpg+large.jpg


HIZ.jpg

Picha hisani ya Michuzi blog

Licha ya mabomu na vitisho vya serikali, waandamaji Zanzibar wangali ngangari kudai maoni yao kuhusu serikali ya Muungano. Haki ya wananchi si kitu cha kuporwa kirahisi siku hizi. Bora tu kusikiliza madi yao na kuyafanyia kazi, lakini nguvu si lo lote na si chochote kwani ni kuchochea zaidi vurugu. Madai yao hayajasikilizwa muda mrefu na kudharaulika kila walipotaka kutoa maoni yao, matokeo leo ndiyo haya.

Kwa nini mwataka kuuana kwa vitu ambavo havina msingi sana? kama mnataka kujitenga sawa serikali ya mapinduzi zanzibar itisheni kura ya maoni haraka watu waamue wanachotaka wazanzibar may be wamechoka mafisadi wa huku bara! wapeni haki yao!!
 
Tusiwasingizie viongozi wa dini yao kwa kila ajenda, hili la Muungano ni kitendawili kilichotegwa, kufumba na kufumbua ipo siku wanaotetea kwa nguvu zote wataumbuka.

Ndoa za kushinikizwa zina matatizo mengi sana tofauti na ndoa za hiari ya wanandoa kwani kwa maamuzi yao sahihi wamekubaliana kwa ridhaa yao kufunga ndo, lakini hizi za mkeka matokeo ndo hayo.

We unasema nini? Tusiwalaumu viongozi wa dini wakati makanisa yamechomwa moto? Kwa nini wasichome ofisi ya RC kama shida ni muungano?
 
Nakubaliana nawe, kwani picha hizi ni maandamano yanayoendelea baada ya mabomu usiku kucha asubuhi wameamkia maandamano. Wapeni haki yao wanayodai, kuendelea kuwanyima haki yao ni kuchochea machafuko kama haya tunayoshuhudia sasa. Somo la urahia kuhusu sheria na haki ya kuhoji muungano lililotolewa na Tundu Lisu linafanya kazi yake, na hapa wameshaamua hadi kieleweka, hakuna kurudi nyuma.
Naomba Mungu aepushie mbali,Shetani ameanza Tanzania baada ya kuua sana SYRIA.
 
tatizo ni elimu ya madrasa ndiyo inayo wapelekea hadi kuchukua uamuzi wa kuchoma makania na vurugu zingine
 
Kinachotokea Zanzibar ni FULL UDINI. Udini at its highest level. PERIOD. Viongozi (CCM) waliushabikia, wakauendekeza, na hata kuufadhili kwa maslahi mafupi ya kisiasa sasa mambo yameharibika - na bado.

Tunaisikia Boko Haram ee? Tunaisikia Al-Shabaab ee? Sasa iko mlangoni mguu mmoja ndani. Matokeo ya viongozi kutoshughulikia matatizo kwa wakati kwa hofu ya kuwaudhi akina fulani ndio haya.

Matokeo ya viongozi kusimama majukwaani tena majukwaa rasmi ya kitaifa kama Bungeni na kuanza kushadadia udini kama turufu ya kisiasa dhidi ya wengine kwa faida ya kulinda maslahi ya chama chetu badala ya kuzungumzia ukweli halisi ndio haya.

Naomba niwatahadharishe viongozi wa CCM ambao kila kukicha hawaachi kukihusisha CHADEMA na udini usiokuwepo lakini katu hutawasikia wakizungumzia makundi yaliyo dhahiri kwa udini kama hili la uamsho huko Zanzibar! Mnakoipeleka nchi siko! Kikundi hiki na mengineyo kadhaa hasa kupitia mwamvuli wa nyumba za ibada yamelelewa kwa muda mrefu na CCM hususan huko Zanzibar, yamekuwa, na sasa yanajipambanua kwa rangi zao halisi - eti Dola ya KIISLAM YA Zanzibar!

Kama wengi wasemavyo, nchi hii itaingizwa kwenye machafuko hususan ya kidini na CCM na si vinginevyo - yetu macho.

Nafikiri tusipindishe, na kusingizia udini. Wazanzibari hawautaki muungano. Full stop, wameanza siku nyingi tangu Mwalimu akiwa rais, na je Mwalimu naye aliushabikia udini. Wengine mwalimu aliwatimua kwa chama, nk.

Tukubali tu yaishe, yani ya kwamba tutakiane kila mema, kila mmoja aende zake. Ingekuwa gumzo kama ndo ungekuwa muungano wa kwanza kuvunjika.
Wanzazibari wapewe wanachokitaka, mnawang'ang'ania wa nini?
 
There are two alternatives
1. serikali tatu Tanganyika Zanzibar ba federal- na baadaye meru nao watadai wawe state na kila mkoa kuwa state!!
2. Zanzibar uwe kama mikoa mingine ile ya bara -- Ndoto!!
Lakini ya serikali mbili hayana tija!!!
 
Na wewe acha mambo ya kizamani Nyerere wa kazi gani huku ukijua ni marehemu. Swala hapa ni watu wanataka haki ya kusikilizwa maoni yao juu ya muungano kuna ugumu gani kusikiliza hata kama wakisema hawautaki si ni sawa kwa sababu muungano huko kwa ajili ya zanzibar na bara kama zanzibar wanachi wanaona hakuna umuhimu sasa nani anaona umuhimu kwa niaba yao. Sasa unasema habari za marehemu umefilisika kimawazo nenda ukamfufue kama wewe unashindwa kutumia akili ambazo umepewa kujui tu kwamba hiki kitu nakihitaji au la hadi marehemu aje akufikirie NI TATIZO acha watu waamue KUNA SHIDA GANI?
BABA WA TAIFA JULIUS KAMBARAGE NYERERE, Upo wapi Mwalimu wa nchi hii,Baba yetu ungekuwepo leo hii NENO LAKO MOJA TU LINGEBADILISHA NCHI HII.
Haya uliyasema na kuyatabiri mda mrefu sana. NAKUMBUKA WAKATI WA UCHAGUZI 1995 ULIONGEA MAMBO MENGI KUHUSU MUUNGANO. Leo hii yanatokea hakuna anayeweza kukumbuka uliyosema. NARUDIA....SEMA NENO MOJA TU HUKO ULIKO LIBADILISHE NCHI YETU.
 
...Katiba ya Zanzibar Toleo la 2010 inatambua kwamba, "Zanzibar ni nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano." Na huu ndi ukweli wa kihistoria, siyo?! Tatizo lisilotatuliwa ni kwa nini Tanganyika haitaki kuwa na katiba yake na kuitambulisha Tanganyika kwenye muungano (?)! Huu ni mshangao unawafanya baadhi ya Wazanzibari kudahi kwamba Tanganyika ina "agenda" ya siri nyuma ya muungano wa kulazimisha!

Cha ajabu na cha kusikitisha; CCM ilipowaruhusu Wazanzibari kuanzisha mchakato wa kuanzisha Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUKI) ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) walidhani itaishia hapo...; walijidanganya hata pale walipokubali kuanzisha mchakato "ghushi" wa katiba kwamba watawabana wananchi wa Zanzibar wasiujadili muungano, hasha; wameshindwa! Nadhani wameweza kuwatia "uzezeta" wananchi wa bara kwa kuwa watu wa Tanganyika wamezowea kuburuzwa na kwao muungano hawaujui kwa jinsi wanavyoujua wananchi wa Zanzibar. Zanzibar wanajitambua na wanajijua; Watanganyika wamejishahau kama "misukule" au "mandondocha" waliyechukuliwa na wachawi na kufanywa "mazemule."

Nadhani hakuna asiyeona harakati za utambuzi na utambulisho wa Wazanzibari; na mara zote kunapotokea hamkani ya kisiasa visiwani wanaotafuta sababu ya kutuliza gafugafu la joto la kisiasa huwa ni Watanganyika kwa kutumia nafasi yao kama ilivyokuwa mwaka 1964 na kama alivyofanya Mwalimu Nyerere...wanafunika "kawa" mwanaharamu apite ilhali wanalikuza tatizo la sintofahamu ya muungano badala ya kutafuta ufumbuzi wa kudfumu wa muungano!

Hivi; kama Wazanzibari wanataka kupiga kura ya maoini juu ya muungano kuna kosa gani? Na hata wakiukataa muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwani ni dhambi? Tuache uwendawazimu wa kudhani vile tunavyodhani kla siku itakuwa kama ilivyokuwa mwaka 1964 au 1984 au 1995 au 2000 au 2005; siku hazigandi, na wananchi wa Zanzibar kama watu huru wanawafundisha "jambo" wananchi wa Tanganyika kwa kuwa Tanganyika iliingizwa kwenye muungano ili kuimeza Zanzibar kwa vile Tanganyika haikuwekwa kwenye ramani isipokuwa Zanzibar ndiyo iliyowekwa.

Nadhani umefika wakati sasa wa kutumia akili yenye satwa ya maamuzi makini na ya kimkakati; wapo waliyehusika kwa namna moja na au nyingine kuhakikisha kwamba Sudan Kusini inajitoa kwenye SUDAN KUBWA; na leo wote ni mashahidi kwamba kuna nchi mpya mbili zilizokuwa moja zinaitwa Sudan Kusini na Sudan Kaskazini - nchi moja ya Wakristo (wengi) na nchi nyingine ya Waislam (wengi). Je, hamuoni kwamba Zanzibar wana haki ya kuamua hatma yao? Na je, hamuoni kwamba Tanganyika ina haki ya kuamua hatma yao? Kwani ni nani aliyewaambia kwamba waliyeasisi muungano ni "miungu" na au "malaika" wenye asili ya watu na walichokifanya kilikuwa maagizo ya Mungu?! Tusijitoe fahamu na au akili ya kudhani kwamba watu wanaweza kudanganywa kwa muda wote na au nguvu zinaweza kutumika muda wote kuwatisha na kuwaogopesha watu wasidai uhuru na haki yao ya kujiamulia mambo yao!

Tuache uzezeta wa akili; turuhusu uhuru na haki ya watu kujiamulia mambo yao wenyewe hata kama kwa upande mmoja ni uchungu na au fedheha. Uhuru, haki na wajibu wa wananchi ni kuamua kwa jinsi wanavyoona wao inafaa! Na hakuna katika historia ya binadamu kwamba aina ya utawala na au uongozi wa kisiasa ulilazimisha jinsi ya kutawala na ukabaki milele - kila utawala ni wenye kwisha na kunapotokea "mapinduzi ya fikra" hapo ndipo panapokuwa chemchemi ya harakati za ujenzi mpya wa nchi mpya na watu wenye mtazamo mpya wa kiakili na kifalsafa. Uhuru kwanza; ubabe na vita vya kuua haki ya kuwa huru baadaye! Huwezi kuwalazimisha binadamu wenye akili timamu ya utambuzi kama unavyoweza kuwalazimisha punda kubeba mizigo huku wakitandikwa bakora na kusukumwa alimuradi mzigo ufike! Punda; hata kama ni mnyama (hayawani) asiyejitambua, akichoka hugoma na lazima abwage mizigo na mateke ayarushe hewani kuonyesha hasira zake....inasemekana kwamba hata wakati mwingine, punda akichoka kuburuzwa na kutandikwa baokora huku amemebeshwa mizigo mizito hurusha mateke na hata kumjeruhi mmiliki. Huyu si binadamu mwenye akili ya utambuzi; nadhani serikali ya JMT na ile ya SUK (ndani ya SMZ) wasiwafanye Wazanzibari na Watanganyika kama "punda" wa kuwalazimisha vile wao (SJMT na SMZ na CCM) wanavyotaka...wafuate utashi wa wananchi unavyotaka; nadhani muafaka ni: KURA YA MAONI JUU YA MUUNGANO! Hili ndio suluhisho la kidemorasia; kama CCM imeamua twende kwa njia ya demokrasia haina budi kukubali "matokeo" ya demokrasia hata kama ni machungu kwa chama hicho!

Mkuu, heshima yako, mimi sina cha ziada umemaliza kazi...
 
hawana lolote,washajazwa ujinga huko madrasatul....

Wewe huo ujinga wako umejazwa kanisani au...?
Lete hoja uckurupuke dada, kama unautaka huu muungano si ni wewe tuu!! Wazanzibari pamoja na ujinga wetu tunajua tunchofanya na kukitetea.
 
Lakini kumbuka wanachodai ni haki yao ya msingi, na wanawajibika kwa uhuru wao kuamua kuukubali Muungano au kuukataa kama wanavyoukana sasa. Kuna faida gani kung'ang'ania Muungano, unatufaidia nini Watanganyika kama si kutuongezea mzigo tu?

Bajeti kubwa, wanaongeza ukubwa wa Bunge, wanatuchukulia ajira zetu wabara wakati sisi Wabara hatutii pua huko Kwao Zenj.

hapa hoja sio muungano,hawa uhamsho wanapigania uislamu ndio maana wanachoma nyumba za Mungu..
Sasa adhabu yao ni kuigeuza Znz mtaa ndani ya Tanga,na Shein awe afsa mtendaji wa mtaa wa znz.
 
Huwezi kuacha kuzilaumu serikali zote mbili (Ya Muungano na ya Zanzibar) kwa kushindwa kuyazuia haya. Ni siku chache tutawaona hawa au ndugu zao wakivaa mabomu na kujitoa mhanga. Nyuma ya yote haya wala si suala la muungano bali DINi. Pili, kukosa kazi na ajira ya kudumu na ya maana kwa wengi wa hawa watu kunachangia kuwa rahisi kurubuniwa!!!!!
 
Back
Top Bottom