BABA JUICE
JF-Expert Member
- Sep 5, 2010
- 426
- 52
Nilipanda gari linatoka tegeta kwenda kariakoo njiani konda akaanza kukusanya nauli,basi mama mmoja akatoa noti yake ya elfu mbili ya zamani, konda akamrudishia huyo mama shilingi elfu moja na mia tano noti mpya(hizi zilizotoka), huyo mama alivyopokea chenchi yake kuona ni noti mpya akasema "konda mimi sizipendi hizi pesa naomba unibadilishie,konda akamjibu waambie waliotengeneza wakubadilishie mimi mwenyewe napokea lakini sizipendi"watu wote kwenye gari waliangua kicheko.