Pata maziwa ya ng'ombe halisi kabisa

Kinumbo

JF-Expert Member
Dec 8, 2019
2,742
4,932
Wakuu natumai mko njema kabisa.

Kwa wakazi wa Dar es salaam nawasogezea huduma hii adhimu kabisa. Natoa huduma ya kuuza maziwa ya ng'ombe halisi kabisa, ni maziwa ya ng'ombe OG. Namanisha kuwa ni maziwa halisi yasio kuwa ata na tone la maji, ni maziwa ambayo ng'ombe anakamuliwa kisha unaletewa. Ni maziwa ambayo ukiyatumia hauto jutia kabisa na utahitaji kuyatumia Kila siku.

Kama utakuwa na kipimo chako cha kupima ili kujilidhisha kuwa ni halisi kabisa ni ruksa, hakuna ujanja ujanja ni maziwa fresh kabisa. Hakuna longo longo wakuu uaminifu ndio jadi yangu. Tutumie maziwa kwa afya bora wakuu, karibuni sana.

Napokea oda kutoka ndani ya Dar es salaam popote pale nitakufikia. Wale wa migahawa na mahotelini popote pale nakuletea maziwa ya ng'ombe halisi kabisa. Wale wa oda kubwa kubwa na ndogo ndogo nakuletea bila shida kabisa. Jukumu lako wewe ni kunipa oda yako tu na itakufikia hapo hapo ulipo.

Pia naombeni connection ni sehemu gani hapa Dar es salaam ina uhaba na uhitaji wa maziwa ya ng'ombe halisi. Nitajitahidi nifike huko nitoe huduma hiyo na nitapita mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba kuhakikisha wanapata huduma rafiki kabisa.

Bei ya maziwa ni Tsh. 2,000 tu kwa lita moja. Bei ya lita kumi kumi ni Tsh. 18,000 tu. Hauto ingia gharama zozote zile za usafiri, wewe ni kunipa oda yako na mzigo wa maziwa halisi unakufikia popote pale ulipo, malipo ni baada ya kupokea mzigo wako. Karibuni sana wakuu, huduma naitoa kwa uaminifu mkubwa mno ni wewe tu ushidwe.

Siku za kazi ni kuanzia Jumatatu mpaka Jumapili, na muda wa kazi ni asubuhi kuanzia saa 1:00 mpaka saa 6:45 mchana, na alasiri kuanzia saa 10:00 mpaka saa 2:00 usiku.

Karibuni sana wakuu napokea oda ujazo wowote ule na pia naleta popote pale ndani ya Dar es salaam. Jenga afya kwa maziwa ya ng'ombe halisi kabisa.

Weka oda yako kuanzia sasa.
 
Kila la kheri. Kwenye biashara ya maziwa ukitaka kufanikiwa uwe mwaminifu kwa kuuza maziwa halisi. Pia usafi ni muhimu sana. Ukishajenga mtandao wa wanunuzi kazi inakuwa rahisi sana.
Asante sana, uaminifu ndio jadi yangu mkuu usafi pia umezingatiwa. Maziwa ni halisi kabisa, karibu sana .
 
Back
Top Bottom