Pascal mayalla aachane na yafuatayo:-

Kibunago

JF-Expert Member
Jan 11, 2008
300
122
Akiwa ndani ya Sabasaba na PPR na baada ya kuona bidhaa fulani inayovutia katika banda la maonyesho, hukosi kumsikia akinena, "……….utafikiri vinatoka ulaya…." au atajishtua na kuuliza "………hivi kweli hivi / hizi si ready made……..?".

Kaka yangu Mayalla,

1. Haijalishi unafanya mzaa au unataka kunogesha kipindi chako; matumizi ya mara kwa mara (kwenye public media) ya kuona kitu kizuri unasema kinatoka Ulaya au nje ya nchi ni mabaya sana na ni dalili za ukosefu wa kuwa na mawazo mapana. Aidha matumizi hayo yanaweza kuwa na athari kwa jamii (hususani watoto na vijana) ambao wanaangalia TV na kumsikia Mwanahabari mzoefu na Mwasisi wa Kiti-Moto kama wewe unakiri kwa kinywa (by implication) kuwa vizuri vinatoka Ulaya au nje tu kwa kutoweka TAHADHALI mwanzoni au mwishoni mwa kipindi chako kuwa baadhi ya maneno yako unayoyatumia (kama hayo) ni ya kuchekesha tu na yasichukuliwe maanani.

2. Tena utambulisho wa ‘ready-made' kwa bidhaa zenye mvuto au ubora ni wa utata mkubwa sana. Hivi ‘ready-made' huwa ni already made toka lini na nini na nani? Je, kuna bidhaa tunazipokea toka mbinguni kama mikate iliyodondoka pale jangwani kwa wana wa Israel? Maana wao wangeweza kusema, "We received Manna prepared / processed / ‘ready- made by Allah". Kama unamaanisha ‘already processed', je ni nani alisema kuwa bidhaa zinazoonekana katika mabanda yote hayo hazijawa processed kwa namna moja au nyingine?

Mayalla angalia sana wewe ni kioo na kwa kupitia chombo kikubwa cha mawasiliano kama TV na Asasi yenu ya PPR unaweza kupotosha sana jamii kama sio na wewe pia kuendelea kujipotosha na kujiaibisha. Tafadhali achana kabisa na matumizi mabaya ya hiyo misamiati unapotangaza biashara ya Watanzania!
 
Ni ushauri mzuri, (ki mtazamo hasi), (ki mtazamo chanya) huenda akisema hivi humaanisha kuwa surprised, na kumaanisha si ulaya peke yake wanaweza tengeneza vitu vizuri peke yao, hata Africa tunaweza, ndo maana huuliza ili muhusika akatae, ili kudhihirishia umma kuwa ni vya Africa na, waafrica wameweza.
 
Nakubaliana na mtoa mada na naomba kuongezea kuwa..tunamuomba awe balanced katika matumizi ya maneno coz kipindi chake hutazamwa na watu wa age tofauti...Ni mbaya sana kuzungumza na watu wazima kama unazungumza na watoto na ni mbaya kuzungumza na watoto kama unazungumza na watu wazima...Kiukweli me huwa na-switch kwa channels zingine kila kipindi chake kinaporushwa...Yaani kuna utoto mwingi sana, kitu ambacho sikukitegemea kutoka kwa Seasoned presenter kama yeye....Hata hivyo haya ni maoni yangu tu so kama hayana maana unaweza kuyaacha....
 
Ni ushauri mzuri, (ki mtazamo hasi), (ki mtazamo chanya) huenda akisema hivi humaanisha kuwa surprised, na kumaanisha si ulaya peke yake wanaweza tengeneza vitu vizuri peke yao, hata Africa tunaweza, ndo maana huuliza ili muhusika akatae, ili kudhihirishia umma kuwa ni vya Africa na, waafrica wameweza.

Yes hata mi nilimuelewa hivyo,alikuwa akiuliza si kwa kumaanisha kuwa cha Ulaya ni bora,ila alikuwa anajaribu kuonesha ile kasumba jamii iliyo nayo kwamba sisi hatuwezi kutengeneza bidhaa bora na bidhaa bora lazima iwe
imetoka nje,hivyo alikuwa anataka tu wale aliokuwa akiwahoji wathibitishie uma kwamba ni bidhaa zilizotengenezwa nyumbani.
 
Anadhihirisha ulimbukeni tulionao baadhi ya waafirka kwamba kila kizuri ni cha mzungu, kuku mzuri ni wakizungu, ng'ombe bora ni wakizungu, bata vile vile. Wakiona aliyonyong'onyea hawakawii kusema wakiswahili huyo, kama ni ng'ombe wa kimasai huyo.

Anaboa sana hata mm nimemsikia, ajirekebishe ili jamii isipoteze imani naye.
 
Back
Top Bottom