Pamoja na makandokando yake, CCM ni ngumu kuing’oa kwa sababu wapinzani hawafuati kanuni za siasa

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Kila jambo kwenye maisha lina sheria zake, zidharau kwa gharama zako mwenyewe!

Najua kuna huu mjadala umekuwa unaendelea wa watu wanaoenda kuunga mkono juhudi kwamba wananunuliwa na wengine wamekuwa wanasema CCM wanaiba kura na kushinda kwa hila ila ngoja nikuelezee vitu viwili vitatu vitakusaidia kwenye uchambuzi wako wa siasa za Tanzania.

Baadhi yetu humu hatukuzaliwa jana. Tumeona Tanzania hii katika hali tofauti tofauti, matatizo yakija, yakikaa na baada ya muda (ambao wakati mwingine ni miaka mingi) matatizo hayo yanapatiwa ufumbuzi. Nikupe mfano mmoja. Wangapi wanakumbuka kipindi kile mabasi yalikuwa yana vile vibao vidogo wanaweka kwa ndani kuonyesha linakwenda wapi? Madereva wakawa wakijisikia muda wowote katika siku wanabadilisha ruti kwenda sehemu nyingine yenye abiria hali iliyokuwa inawapa usumbufu mkubwa abiria. Ilichukua muda mrefu mpaka ufumbuzi ukapatikana ambao ulikuwa ni kuyapaka mabasi yote rangi maalumu. Ninachotaka kusema wakati ule tatizo lilipokuwepo, kelele zilikuwa nyingi, ushauri ulikuwa unatolewa kila siku lakini ilichukua muda mrefu sana uamuzi kuchukuliwa ila sikumbuki kama iliwahi kuwa ajenda ya mwanasiasa yeyote wa upinzani!

Nimetoa mfano huo mdogo kusema tu kwamba kwenye suala la changamoto mbalimbali za kijamii na maendeleo, CCM inazitatua ila siyo kwa kasi ambayo wengi tungependa. Wangapi mnakumbuka kero za Muhimbili? Wengi mnaweza msitambue lakini Tanzania tumefanya mapinduzi kwenye sekta ya afya ingawa changamoto bado ni nyingi ila tumetoka mbali sana. Wamarekani wana msemo 'taking your sweet a$$ time', kwa maana ya kufanya vitu taratibu mnooo. CCM na serikali zake inachukua muda mrefu sana kutatua kero za watu ila ukweli ni kuwa, kwa wakati wanaoamua wao wanakujaga kuzitatua. Kuna kiongozi wa CCM sikumbuki ni nani alisikika hivi karibuni akisema CCM inaamua kama sehemu fulani ipate maendeleo au hapana, kwa bahati mbaya sana huo ni ukweli mtupu.

Tatizo kubwa la ndugu zangu wapinzani ni kuendelea kudhani ajenda kubwakubwa mfano shutuma kubwa za rushwa zinaweza kuwasaidia. Mimi nadhani hilo linaweza kufanikiwa kwa kiasi fulani kidogo sana ila haliwezi kuwapeleka Magogoni. Kuna mwanasiasa mmoja wa Marekani Tip O'Neal aliwahi kusema 'All politics is local', ni msemo na filosofia ambayo imekuja kukubalika kama ukweli usiopingika. Msemo huo una maana kama unataka ushinde katika uchaguzi wowote, siasa zenye mantiki na maana kwa mpiga kura mmoja mmoja ni zile zinazohusu mambo yanayomuhusu moja kwa moja kwa maisha yake ya kila siku. Kero zile ambazo zinamsumbua kila siku ndiyo zinaamua kura yake anampa nani. Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti, wanasiasa makini wanaiangalia philosophy hiyo na kuiweka ifit katika mazingira na nyakati za wakati huo. Moja ya kauli mbiu za kampeni ya Bill Clinton mwaka 1992 ulikuwa msemo mmoja ambao na wenyewe umekuwa kama 'ukweli usiopingika' ni msemo unaosema 'It's the economy, stupid' ukiwa na maana ni uchumi ndiyo unaomatter kwa mpiga kura, mengine yote ni mbwembwe tu! Yote hii inarudi kule kule, all politics is local!

Nasema haya kusisitiza tu kwamba skendo sijui Bombadia, sijui mambo ya Makonda, sijui ndege gani sujui, mpiga kura wa kawaida kwa maoni yake hizo issues hazimuathiri moja kwa moja katika maisha yake ya kila siku ya kujitafutia mkate, nawaambia ukweli. Na huyo mpiga kura anaweza akawa sahihi au asiwe sahihi, hilo siyo ninalotaka kuzungumzia hapa, siku moja nilimsikia Halima Mdee akijaribu kuelimisha kuhusu jinsi gani issue hizo zina athari kwa mpiga kura moja kwa moja, ila ni kupoteza muda tu, kuna ukweli usiopingika nimeutaja hapo juu. Augustine Mrema alikuwa na style ya 'kulipua mabomu', ilimfikisha wapi?

Mimi nadhani CCM wameamua tu kucheza siasa za rafu na kibabe ila naamini wana uwezo wa kushinda chaguzi bila watu kutolewa ngeu na makandokando mengine yasiyoeleweka. Ushauri kwa wapinzani, siasa za kupigia kelele issue za kitaifa zinauza magazeti sana ila haziwezi kuwapeleka Ikulu.

CCM itaangushwa na gravity, kanuni nyingine ya maisha isiyopingika!

NYONGEZA: Naona niseme natambua kuna wanasiasa wengi tu wa upinzani, hasa ngazi za chini wamefuata kanuni za siasa nilizozitaka hapo juu kwa ufanisi mkubwa. Inapokuja sasa wakati wa kupigania kushika dola, kuna sehemu wanakwama au wanajisahau na kwa mtazamo wangu sababu kubwa ni hii.
 
Mwanafunzi slow na mwanafunzi mwenye kupick faster yupi hupendwa na walimu?


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Lingine na ongezea hapo upinzani Kuna kitu haujakijua .watanzania wengi tuna roho ya "Bora tukose wote" kwa mfano Mimi nilikuwa mpinzani mzuri tu hapo mwanzo toka nijue kwamba mbowe alikuwa mmiliki wa club inayouza madawa ya kulevya na Tena akaja akakubali kumweka lowassa agombee urais tokea siku hiyo nikaona wapinzani hamna kitu ni miyeyusho kwa hiyo Bora CCM.. ndo hivo watajibeba maana wasichukulie poa tuliohama kwa sababu ya kutuwekea fisadi mkuu ni wengi hatujasahau walivyomchafuaga.
 
Ni kweli na lingine ni lile la kudai katiba mpya - hili ni watu wachache sana watampigia kura mpinzani kusudi afanikiwe kwa hilo! Japo ni kitu cha maana.
 
Ukweli wenyewe mnaujua, kuwa CCM imekosa mvuto kwa wananchi, kilichobaki ni CCM "kubebwa" na vyombo vya dola

Polisi+Wasimamizi wa uchaguzi+maDC&maRC, ndiyo siri ya ushindi wa CCM

Jaribu kuimagine Mkuu wa Mkoa wa Dar alidiriki kuwapongeza Polisi, baada ya "kuwapa" ushindi CCM wa Jimbo la Ukonga hivi karibuni

Kama CCM itaruhusu uchaguzi huru na haki, ni wepesi kuliko tissue paper!
 
Lingine na ongezea hapo upinzani Kuna kitu haujakijua .watanzania wengi tuna roho ya "Bora tukose wote" kwa mfano Mimi nilikuwa mpinzani mzuri tu hapo mwanzo toka nijue kwamba mbowe alikuwa mmiliki wa club inayouza madawa ya kulevya na Tena akaja akakubali kumweka lowassa agombee urais tokea siku hiyo nikaona wapinzani hamna kitu ni miyeyusho kwa hiyo Bora CCM.. ndo hivo watajibeba maana wasichukulie poa tuliohama kwa sababu ya kutuwekea fisadi mkuu ni wengi hatujasahau walivyomchafuaga.
Namba ya simu umesahau kuweka
 
Kwa hiyo CCM inafata kanuni za siasa?

Kuna nguli mmoja anayeheshimika sana kwenye historia anaitwa Nicolo Machiavelli aliwahi kufundisha kwamba 'It is better to be feared than loved, if you cannot be both' au kwa tafsiri ni 'Ni bora kuogopwa kuliko kupendwa kama haiwezekani kuwa vyote viwili'.
 
Ni kweli na lingine ni lile la kudai katiba mpya - hili ni watu wachache sana watampigia kura mpinzani kusudi afanikiwe kwa hilo! Japo ni kitu cha maana.

Mfano mzuri sana huu! Yaani wasipoelewa hata kwa mfano huu, basi tena hakuna zaidi tunaloweza kuwasaidia.
 
Kila jambo kwenye maisha lina sheria zake, zidharau kwa gharama zako mwenyewe!

Najua kuna huu mjadala umekuwa unaendelea wa watu wanaoenda kuunga mkono juhudi kwamba wananunuliwa na wengine wamekuwa wanasema CCM wanaiba kura na kushinda kwa hila ila ngoja nikuelezee vitu viwili vitatu vitakusaidia kwenye uchambuzi wako wa siasa za Tanzania.

Baadhi yetu humu hatukuzaliwa jana. Tumeona Tanzania hii katika hali tofauti tofauti, matatizo yakija, yakikaa na baada ya muda (ambao wakati mwingine ni miaka mingi) matatizo hayo yanapatiwa ufumbuzi. Nikupe mfano mmoja. Wangapi wanakumbuka kipindi kile mabasi yalikuwa yana vile vibao vidogo wanaweka kwa ndani kuonyesha linakwenda wapi? Madereva wakawa wakijisikia muda wowote katika siku wanabadilisha ruti kwenda sehemu nyingine yenye abiria hali iliyokuwa inawapa usumbufu mkubwa abiria. Ilichukua muda mrefu mpaka ufumbuzi ukapatikana ambao ulikuwa ni kuyapaka mabasi yote rangi maalumu. Ninachotaka kusema wakati ule tatizo lilipokuwepo, kelele zilikuwa nyingi, ushauri ulikuwa unatolewa kila siku lakini ilichukua muda mrefu sana uamuzi kuchukuliwa ila sikumbuki kama iliwahi kuwa ajenda ya mwanasiasa yeyote wa upinzani!

Nimetoa mfano huo mdogo kusema tu kwamba kwenye suala la changamoto mbalimbali za kijamii na maendeleo, CCM inazitatua ila siyo kwa kasi ambayo wengi tungependa. Wangapi mnakumbuka kero za Muhimbili? Wengi mnaweza msitambue lakini Tanzania tumefanya mapinduzi kwenye sekta ya afya ingawa changamoto bado ni nyingi ila tumetoka mbali sana. Wamarekani wana msemo 'taking your sweet a$$ time', kwa maana ya kufanya vitu taratibu mnooo. CCM na serikali zake inachukua muda mrefu sana kutatua kero za watu ila ukweli ni kuwa, kwa wakati wanaoamua wao wanakujaga kuzitatua. Kuna kiongozi wa CCM sikumbuki ni nani alisikika hivi karibuni akisema CCM inaamua kama sehemu fulani ipate maendeleo au hapana, kwa bahati mbaya sana huo ni ukweli mtupu.

Tatizo kubwa la ndugu zangu wapinzani ni kuendelea kudhani ajenda kubwakubwa mfano shutuma kubwa za rushwa zinaweza kuwasaidia. Mimi nadhani hilo linaweza kufanikiwa kwa kiasi fulani kidogo sana ila haliwezi kuwapeleka Magogoni. Kuna mwanasiasa mmoja wa Marekani Tip O'Neal aliwahi kusema 'All politics is local', ni msemo na filosofia ambayo imekuja kukubalika kama ukweli usiopingika. Msemo huo una maana kama unataka ushinde katika uchaguzi wowote, siasa zenye mantiki na maana kwa mpiga kura mmoja mmoja ni zile zinazohusu mambo yanayomuhusu moja kwa moja kwa maisha yake ya kila siku. Kero zile ambazo zinamsumbua kila siku ndiyo zinaamua kura yake anampa nani. Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti, wanasiasa makini wanaiangalia philosophy hiyo na kuiweka ifit katika mazingira na nyakati za wakati huo. Moja ya kauli mbiu za kampeni ya Bill Clinton mwaka 1992 ulikuwa msemo mmoja ambao na wenyewe umekuwa kama 'ukweli usiopingika' ni msemo unaosema 'It's the economy, stupid' ukiwa na maana ni uchumi ndiyo unaomatter kwa mpiga kura, mengine yote ni mbwembwe tu! Yote hii inarudi kule kule, all politics is local!

Nasema haya kusisitiza tu kwamba skendo sijui Bombadia, sijui mambo ya Makonda, sijui ndege gani sujui, mpiga kura wa kawaida kwa maoni yake hizo issues hazimuathiri moja kwa moja katika maisha yake ya kila siku ya kujitafutia mkate, nawaambia ukweli. Na huyo mpiga kura anaweza akawa sahihi au asiwe sahihi, hilo siyo ninalotaka kuzungumzia hapa, siku moja nilimsikia Halima Mdee akijaribu kuelimisha kuhusu jinsi gani issue hizo zina athari kwa mpiga kura moja kwa moja, ila ni kupoteza muda tu, kuna ukweli usiopingika nimeutaja hapo juu. Augustine Mrema alikuwa na style ya 'kulipua mabomu', ilimfikisha wapi?

Mimi nadhani CCM wameamua tu kucheza siasa za rafu na kibabe ila naamini wana uwezo wa kushinda chaguzi bila watu kutolewa ngeu na makandokando mengine yasiyoeleweka. Ushauri kwa wapinzani, siasa za kupigia kelele issue za kitaifa zinauza magazeti sana ila haziwezi kuwapeleka Ikulu.

CCM itaangushwa na gravity, kanuni nyingine ya maisha isiyopingika!

NYONGEZA: Naona niseme natambua kuna wanasiasa wengi tu wa upinzani, hasa ngazi za chini wamefuata kanuni za siasa nilizozitaka hapo juu kwa ufanisi mkubwa. Inapokuja sasa wakati wa kupigania kushika dola, kuna sehemu wanakwama au wanajisahau na kwa mtazamo wangu sababu kubwa ni hii.
Kabisa. Hawafuati kanuni...wanajiumba wao kama 'Mungu" n watakatifu, wapinzani hawataki wazo lolote isipokuwa kusifiwa. Wanataka wananchi waone walioko madarakani kama vile n "mashetani" na wao wapinzani n watakatifu. Haiwezekani.

Pia uchaguzi wa 2015 uliweka kila kitu wazi. Wananchi wanaelewa n nani mpinga ufisadi wa kweli, na nani siasa kwake n biashara tu!
 
Asante kwa ushauri Ila si kwamba tunyamaze kukemea rushwa na matumizi yasiyoidhinishwa na bunge. Si haki pia wakemeaji kushambuliwa kwa risasi. Ndiyo maana tuna leadership ambayo hugs wan-a majukumu.
Haya ya kuanzia uongozi kwenye tawi ndiyo iliwezesha CHadema kupata madiwani wengi ambao wengine wameamua kumtumikia shekel.
 
Asante kwa ushauri Ila si kwamba tunyamaze kukemea rushwa na matumizi yasiyoidhinishwa na bunge. Si haki pia wakemeaji kushambuliwa kwa risasi. Ndiyo maana tuna leadership ambayo hugs wan-a majukumu.
Haya ya kuanzia uongozi kwenye tawi ndiyo iliwezesha CHadema kupata madiwani wengi ambao wengine wameamua kumtumikia shekel.
Hawana Lolote hawa maccm, wananchi tuna imani na UPINZANI.

Kama vipi wakujibu wewe sii mimi.
TOKA LINI KULINDA MALI IMEKUWA KOSA LA JINAI?

Wananchi tunataka kuzilinda kura zetu kama tulindavyo utaifa wetu.
 
Hawana Lolote hawa maccm, wananchi tuna imani na UPINZANI.

Kama vipi wakujibu wewe sii mimi.
TOKA LINI KULINDA MALI IMEKUWA KOSA LA JINAI?

Wananchi tunataka kuzilinda kura zetu kama tulindavyo utaifa wetu.
"Wananchi tuna imani na upinzani! " What a generalization! Uko peke yako ukiandka mawazo yako peke yako, alafu unasema "wananchi"
 
Hawana Lolote hawa maccm, wananchi tuna imani na UPINZANI.

Kama vipi wakujibu wewe sii mimi.
TOKA LINI KULINDA MALI IMEKUWA KOSA LA JINAI?

Wananchi tunataka kuzilinda kura zetu kama tulindavyo utaifa wetu.
Wananchi wa wapi hao?, Jisemee mwenyewe, hivi bado hujatambua kwamba hatuna vyama vya upinzani tu. Kuna club za wanaharakati, na saccos za familia. Hao wanaorudi ccm wala wamechoka ubabaishaji. Chama kinatakiwa kuwa taasisi si kikundi cha porojo na propaganda uchwara.
 
Kila jambo kwenye maisha lina sheria zake, zidharau kwa gharama zako mwenyewe!

Najua kuna huu mjadala umekuwa unaendelea wa watu wanaoenda kuunga mkono juhudi kwamba wananunuliwa na wengine wamekuwa wanasema CCM wanaiba kura na kushinda kwa hila ila ngoja nikuelezee vitu viwili vitatu vitakusaidia kwenye uchambuzi wako wa siasa za Tanzania.

Baadhi yetu humu hatukuzaliwa jana. Tumeona Tanzania hii katika hali tofauti tofauti, matatizo yakija, yakikaa na baada ya muda (ambao wakati mwingine ni miaka mingi) matatizo hayo yanapatiwa ufumbuzi. Nikupe mfano mmoja. Wangapi wanakumbuka kipindi kile mabasi yalikuwa yana vile vibao vidogo wanaweka kwa ndani kuonyesha linakwenda wapi? Madereva wakawa wakijisikia muda wowote katika siku wanabadilisha ruti kwenda sehemu nyingine yenye abiria hali iliyokuwa inawapa usumbufu mkubwa abiria. Ilichukua muda mrefu mpaka ufumbuzi ukapatikana ambao ulikuwa ni kuyapaka mabasi yote rangi maalumu. Ninachotaka kusema wakati ule tatizo lilipokuwepo, kelele zilikuwa nyingi, ushauri ulikuwa unatolewa kila siku lakini ilichukua muda mrefu sana uamuzi kuchukuliwa ila sikumbuki kama iliwahi kuwa ajenda ya mwanasiasa yeyote wa upinzani!

Nimetoa mfano huo mdogo kusema tu kwamba kwenye suala la changamoto mbalimbali za kijamii na maendeleo, CCM inazitatua ila siyo kwa kasi ambayo wengi tungependa. Wangapi mnakumbuka kero za Muhimbili? Wengi mnaweza msitambue lakini Tanzania tumefanya mapinduzi kwenye sekta ya afya ingawa changamoto bado ni nyingi ila tumetoka mbali sana. Wamarekani wana msemo 'taking your sweet a$$ time', kwa maana ya kufanya vitu taratibu mnooo. CCM na serikali zake inachukua muda mrefu sana kutatua kero za watu ila ukweli ni kuwa, kwa wakati wanaoamua wao wanakujaga kuzitatua. Kuna kiongozi wa CCM sikumbuki ni nani alisikika hivi karibuni akisema CCM inaamua kama sehemu fulani ipate maendeleo au hapana, kwa bahati mbaya sana huo ni ukweli mtupu.

Tatizo kubwa la ndugu zangu wapinzani ni kuendelea kudhani ajenda kubwakubwa mfano shutuma kubwa za rushwa zinaweza kuwasaidia. Mimi nadhani hilo linaweza kufanikiwa kwa kiasi fulani kidogo sana ila haliwezi kuwapeleka Magogoni. Kuna mwanasiasa mmoja wa Marekani Tip O'Neal aliwahi kusema 'All politics is local', ni msemo na filosofia ambayo imekuja kukubalika kama ukweli usiopingika. Msemo huo una maana kama unataka ushinde katika uchaguzi wowote, siasa zenye mantiki na maana kwa mpiga kura mmoja mmoja ni zile zinazohusu mambo yanayomuhusu moja kwa moja kwa maisha yake ya kila siku. Kero zile ambazo zinamsumbua kila siku ndiyo zinaamua kura yake anampa nani. Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti, wanasiasa makini wanaiangalia philosophy hiyo na kuiweka ifit katika mazingira na nyakati za wakati huo. Moja ya kauli mbiu za kampeni ya Bill Clinton mwaka 1992 ulikuwa msemo mmoja ambao na wenyewe umekuwa kama 'ukweli usiopingika' ni msemo unaosema 'It's the economy, stupid' ukiwa na maana ni uchumi ndiyo unaomatter kwa mpiga kura, mengine yote ni mbwembwe tu! Yote hii inarudi kule kule, all politics is local!

Nasema haya kusisitiza tu kwamba skendo sijui Bombadia, sijui mambo ya Makonda, sijui ndege gani sujui, mpiga kura wa kawaida kwa maoni yake hizo issues hazimuathiri moja kwa moja katika maisha yake ya kila siku ya kujitafutia mkate, nawaambia ukweli. Na huyo mpiga kura anaweza akawa sahihi au asiwe sahihi, hilo siyo ninalotaka kuzungumzia hapa, siku moja nilimsikia Halima Mdee akijaribu kuelimisha kuhusu jinsi gani issue hizo zina athari kwa mpiga kura moja kwa moja, ila ni kupoteza muda tu, kuna ukweli usiopingika nimeutaja hapo juu. Augustine Mrema alikuwa na style ya 'kulipua mabomu', ilimfikisha wapi?

Mimi nadhani CCM wameamua tu kucheza siasa za rafu na kibabe ila naamini wana uwezo wa kushinda chaguzi bila watu kutolewa ngeu na makandokando mengine yasiyoeleweka. Ushauri kwa wapinzani, siasa za kupigia kelele issue za kitaifa zinauza magazeti sana ila haziwezi kuwapeleka Ikulu.

CCM itaangushwa na gravity, kanuni nyingine ya maisha isiyopingika!

NYONGEZA: Naona niseme natambua kuna wanasiasa wengi tu wa upinzani, hasa ngazi za chini wamefuata kanuni za siasa nilizozitaka hapo juu kwa ufanisi mkubwa. Inapokuja sasa wakati wa kupigania kushika dola, kuna sehemu wanakwama au wanajisahau na kwa mtazamo wangu sababu kubwa ni hii.

Unajifanya MTU mzima lakini kwa maandisho yako we dogo tu.

Ccm hawajawahi shinda uchaguzi toka 1995,uchaguzi Dar ulivurugwa makusudi tulipiga kura marambili, ndo mkapa akatangazwa mshindi.

1995 Zanzibar , CuF walishinda, Nyerere akaamuru tume imtangaze komando kwa nguvu. Uko hapo kaka

2010 Dr W. Slaa alimbwaga Jk kwa mbali lakkni time haikumtangaza. Slaa aliwahi kiri hadharani, kuibiwa kura

2015 E. Lowasa alimgaragaza magufuli, time ikapindua matokeo. Vituo vya kuhesabu kura ( tallying center) vya ukawa vikavamiwa vikaharibiwa, na wahusika wakawekwa ndani. Je unayajua haya ???

Kule zenji 2015 maalimu alishinda jecha akafanya yake. au umesahau.???

dogo hoja yako ya wapinzani kutofuata kanuni za siasa haina mashiko, kwa kuwa siasa za bongo hazifuati kanuni,
 
Wakiitaka wanaweza kuipata bila hata kuniuliza.

Ni hivi boss sio kwamba ccm imeamua kucheza rafu kwa bahati mbaya bali ndio njia iliyobakia. Ni kweli inaweza kushinda kihalali lakini hakuna uwezekano wa ccm kuwa na huo wingi mbovu unaowapa kiburi cha kuamua nini kifanyike. Na iwapo huu wingi mbovu wa ccm utaondoka mifumo yote itafanya kazi kwa weledi kwani hakutakuwa na vyeo vya upendeleo ili kulipa fadhila. Miradi itaenda nchi nzima kwa usahihi kwani kila eneo litakuwa na umuhimu na sio upendeleo wa atakapo kiongozi.

Kwa ajili ya huu wingi mbovu wa ccm unaopatikana kwa hizo rafu ndio unaona CDF, IGP, Spika, chief justice nk wanadhani ni robot za mkulu hivyo hawana popote wanaweza kumuambia hapa ni sawa au sio sawa na hapa ni mwisho wa madaraka yake. Kama unadhani ccm iko madarakani kwa kufuata kanuni unazoziamini shikilia hapo hapo.
 
Unajifanya MTU mzima lakini kwa maandisho yako we dogo tu.

Ccm hawajawahi shinda uchaguzi toka 1995,uchaguzi Dar ulivurugwa makusudi tulipiga kura marambili, ndo mkapa akatangazwa mshindi.

1995 Zanzibar , CuF walishinda, Nyerere akaamuru tume imtangaze komando kwa nguvu. Uko hapo kaka

2010 Dr W. Slaa alimbwaga Jk kwa mbali lakkni time haikumtangaza. Slaa aliwahi kiri hadharani, kuibiwa kura

2015 E. Lowasa alimgaragaza magufuli, time ikapindua matokeo. Vituo vya kuhesabu kura ( tallying center) vya ukawa vikavamiwa vikaharibiwa, na wahusika wakawekwa ndani. Je unayajua haya ???

Kule zenji 2015 maalimu alishinda jecha akafanya yake. au umesahau.???

dogo hoja yako ya wapinzani kutofuata kanuni za siasa haina mashiko, kwa kuwa siasa za bongo hazifuati kanuni,

1995 ulikuwa wapi? Mimi nilihudhuria mkutano wa mwisho wa kampeni wa NCCR-Mageuzi uliofanyika pale Jangwani. Wakati watu wanatawanyika tukapigwa mabomu ya machozi pale Magomeni.

Huwa wanasemaga, ukiwa unapambana na bingwa inabidi upigane naye kumshinda kwa K'O. Bingwa huwa hashindwi kwa point. Naomba utafakari hiyo kauli.
 
Asante kwa ushauri Ila si kwamba tunyamaze kukemea rushwa na matumizi yasiyoidhinishwa na bunge. Si haki pia wakemeaji kushambuliwa kwa risasi. Ndiyo maana tuna leadership ambayo hugs wan-a majukumu.
Haya ya kuanzia uongozi kwenye tawi ndiyo iliwezesha CHadema kupata madiwani wengi ambao wengine wameamua kumtumikia shekel.

Wanafanya kazi ya maana sana hilo sipingi wana sibishi na zaidi nawapa pongezi. Ila jiulize, kelele za miaka yote za wapinzani kwenye grand corruption imezipunguza hizo rushwa, jibu ni hapana! Jiulize, kelele za miaka yote hiyo zimewapeleka Ikulu, jibu ni hapana!

Kwa hiyo kama nilivyosema mwanzo, ni issue inayowapa umaarufu lakini hauongezi kura, at least siyo kwa uwiano wa nguvu kubwa na tahadhari wapinzani wanazochukua kupiga kelele hizo. It's just not worth it!

Mapambano ya rushwa ambayo ingeweza kuwapa kura nyingi ni ya hizi rushwa ndogondogo zinazoleta kero kwa maisha ya kila siku ya watu ambayo ndiyo mada niliyoleta. Ila hata kwa hilo wameshachelewa, ndiyo ajenda kuu ya Magufuli hiyo sasa hivi. Kumeshakucha, siyo muda wa kuvuta shuka sasa hivi.
 
Back
Top Bottom