Padri Karugendo amchambua Pombe Magufuli??

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,503
55,134
..mwandishi anaelezea aliyoyaona na kuyasikia Chato, jimboni kwa waziri Magufuli.


..ni tuhuma nzito za upendeleo,ukabila, na rushwa.


..ninapata wasiwasi kwamba ukiamua kumchunguza kwa umakini Pombe Magufuli unaweza ku-conclude kwamba ni "mchanyato" wa kiula,msuya, na mramba.


..wengine wanafikiri anafaa kuwa Waziri Mkuu au hata Raisi.

raia mwema said:
Wakati ninarejea Dar es Salaam, kutoka Kagera, nilisimama Chato, Lunzewe, Isaka, Igunga, Singida, Dodoma, Morogoro. Sehemu zote hizi nimeshuhudia mikutano ya wagombea wa CCM, wakijinadi kwa wanachama ili kupigiwa kura ya maoni. Sehemu zote hizi kulikuwa na dalili za nguvu ya fedha.



Baadhi ya wagombea wamenunua simu za mkononi na kusambaza majimboni kwao. Kwingine pikipiki zimesambazwa. Kule Chato mgombea mmoja alikuwa akiwaelezea wanachama wa CCM, kwamba kwa vile analipenda sana jimbo alihakikisha barabara ya Bwanga-Kyamyorwa inapinda kupitia Chato, badala ya ramani yake ya kupitia Biharamulo mjini. Na kwamba ametumia kila uwezo wake kuhakikisha Mji wa Chato unakuwa na huduma muhimu na majengo ya kisasa kiasi una sifa zote za kuwa makao makuu ya Mkoa wa Geita.


Majigambo mengine ya mheshimiwa huyo ni kwamba amefanikiwa kuleta Mkoa mpya wa Geita na kuhakikisha Chato, inatengwa kutoka Mkoa wa Kagera.



Kwa wengi hili halikuwa jambo jipya maana siku zote mheshimiwa huyu hakukubali kuwa Chato ni sehemu ya Mkoa wa Kagera. Hakuna uhakika wa asilimia 100 kuonyesha kuwa watu wengi wa Chato, walitamani kutengwa kutoka Mkoa wa Kagera. Hivyo hili la kuimega Chato kwenda Mkoa wa Geita linaweza kumjenga au kumbomoa.


Kuipindisha barabara ni aina fulani ya rushwa. Ingawa barabara hii imechangia kiasi kikubwa kwa maendeleo ya Chato na Kimwani, imekwamisha maendeleo ya maeneo mengine kama vile Buziku, Lukola na Biharamulo mjini. Hata hivyo, barabara hii imejengwa kisiasa. Imeharibika mapema. Ukipita kwenye barabara hii huwezi kuamini kama ni mpya. Na kusema kweli kama mkadarasi aliyeijenga barabara hii amelipwa na kuondoka, atakuwa ametenda dhambi kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na kama kuna Mtanzania aliyemsaidia mkandarasi huyu kuhujumu Taifa letu, basi Mtanzania huyu ni bora apate zawadi ya kwenda jela si chini ya miaka mitano. Nchi nyingine kama China, mtu kama huyu anapigwa risasi na kutoweka kwenye uso wa dunia.


Na hili ndilo tatizo la mambo yote yanayofanyika kwa mtindo huu wa rushwa na hongo. Wagombea wakipitishwa kwa rushwa na hongo, wakifika madarakani wanajifanyia mambo yao. Hawana muda wa kuwakumbuka wapiga kura wao, maana walimalizana wakati wa uchaguzi. Mtu anayehonga ili apate ukandarasi wa kujenga barabara, akishafanikiwa anajenga ovyo ovyo maana amekwisha malizana na wahusika.


Mfano mzuri ni Barabara ya Bwanga-Kyamyorwa. Kama barabara hii ilikaguliwa na wahandisi wetu na kupitishwa, ina maana walihongwa, au wakandarasi waliojenga walitoa hongo ili kupata kazi hiyo. Hivyo walijenga kwa kiwango cha chini na kujiondokea. Kufuatana na barabara hii ilivyoharibika mtu hahitaji shahada ya uhandisi kutambua kwamba kazi ilifanywa chini viwango.


Hoja ninayoijenga hapa ni kwamba bila kutafuta dawa ya ugonjwa huu wa rushwa na hongo, tutaendelea kutawaliwa na watawala waliochaguliwa kwa rushwa na hongo na hawa kwa vyovyote vile hawawezi kuwa na mapenzi na maendeleo ya wananchi wote zaidi ya kupenda maendeleo yao binafsi na kuendelea kutafuta fedha ili washinde chaguzi nyingine na wakae madarakani milele.


Tunahitaji mfumo utakao tuwezesha kuwachagua viongozi wetu kwa kufuata sifa, uwezo wa kiakili na kutenda kazi, uzalendo, uadilifu na sifa nyinginezo za kiongozi makini.
 
sijaelewa anashitaki au ana lalamika? hata si makosa kupindisha barabara ikiwa bado inawasaidia wana jamhuri ya muungano hata kama si ilivyokusudiwa
 
Onyisile Obheli said:
sijaelewa anashitaki au ana lalamika? hata si makosa kupindisha barabara ikiwa bado inawasaidia wana jamhuri ya muungano hata kama si ilivyokusudiwa

Onyisile Obheli,

..bila shaka wana Chato ni sehemu ya jamhuri na wanastahili barabara ya lami.

..tatizo ni kwamba mbunge wa Chato, kwa kutumia nafasi ya uwaziri wa miundo mbinu, ameamua kuvuruga mipango ya serikali na kulazimisha uujenzi wa barabara uchepuke na kupitia kwenye jimbo lake. kwangu mimi huo ni ukosefu mkubwa wa maadili na ni upendeleo wa waziwazi.

..tatizo lingine ni kwamba barabara yenyewe imejengwa kwa viwango duni, ambayo ni dalili ya wazi kwamba rushwa imetembea hapo. inawezekana vipi waziri anayesifika kwa umakini na usimamizi, kama John Magufuli, akaruhusu barabara ya kiwango cha chini ijengwe jimboni kwake?

..ndiyo maana nikamfananisha na Nalaila Kiula, Cleopa Msuya, na Basili Mramba.

..ajabu ni kwamba ameweza vipi kuwa under the radar muda wote huu?
 
Nadhani aliyeiandika habari hii alikuwa na mashahi binafsi na uchaguzi wa chato au chuki binafsi dhidi ya Mbunge huyo ambaye wengi tunamwona kama mtetezi wa wanyonge na mfuatitiliaji wa sheria.

Tuhuma dhidi yake naona hazikuwa na ushahidi wa kutosha. JPM ni mchapakazi mzuri. Wakubwa wengi hawampendi kwa sababu anawafunika kiutendaji.

He is a PM material!
 
sijaelewa anashitaki au ana lalamika? hata si makosa kupindisha barabara ikiwa bado inawasaidia wana jamhuri ya muungano hata kama si ilivyokusudiwa

Anyisile Obheli, Hata mimi simwelewi elewi huyu Karugendo. Alitaka magufuli achote hiyo mihela na kuipeleka ufukweni ama Uarabuni?????????? Amefanya maendeleo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa TZ na waTZ wote wanafaidika.

Kuhusu suala la Chato kuletwa mkoa mpya wa Geita, mbona hata kule kwa Mizengo Pinda huo mkoa nao umetengwa, kwa maana hiyo Magufuli napo ameingilia huko.

Karugendo ana chembechembe za ukabila, hakuna kingine kinachomsukuma.
 
Onyisile Obheli,

..bila shaka wana Chato ni sehemu ya jamhuri na wanastahili barabara ya lami.

..tatizo ni kwamba mbunge wa Chato, kwa kutumia nafasi ya uwaziri wa miundo mbinu, ameamua kuvuruga mipango ya serikali na kulazimisha uujenzi wa barabara uchepuke na kupitia kwenye jimbo lake. kwangu mimi huo ni ukosefu mkubwa wa maadili na ni upendeleo wa waziwazi.

..tatizo lingine ni kwamba barabara yenyewe imejengwa kwa viwango duni, ambayo ni dalili ya wazi kwamba rushwa imetembea hapo. inawezekana vipi waziri anayesifika kwa umakini na usimamizi, kama John Magufuli, akaruhusu barabara ya kiwango cha chini ijengwe jimboni kwake?

..ndiyo maana nikamfananisha na Nalaila Kiula, Cleopa Msuya, na Basili Mramba.

..ajabu ni kwamba ameweza vipi kuwa under the radar muda wote huu?
sawasawa kabisa, nashukuru kama umetambua kuwa wana chato ni sehemu ya wanajamhuri
hivyo walistahili kupatiwa barabara, pia unaweza ukute serikali ndiyo iliyotaka kula rushwa
kwa kutaka kujenga barabara tofauti na chato ambayo pengine ndiyo iliyokusudiwa na
hivyo mbunge alistukia dili na kuhahakisha barabara inajengwa ilipokusudiwa.

sasa narudi kukuunga mkono kwamba sasa jambo la msingi sasa liwe ni kiwango cha barabara
sasa, ili tuweze kuona huyo m jenzi alistahili kulipwa kwa kiwango cha barabara ambacho ni kibovu
ama lah??
 
..mwandishi anaelezea aliyoyaona na kuyasikia Chato, jimboni kwa waziri Magufuli.


..ni tuhuma nzito za upendeleo,ukabila, na rushwa.


..ninapata wasiwasi kwamba ukiamua kumchunguza kwa umakini Pombe Magufuli unaweza ku-conclude kwamba ni "mchanyato" wa kiula,msuya, na mramba.


..wengine wanafikiri anafaa kuwa Waziri Mkuu au hata Raisi.

Nonsense,

Huna Mpya, majungu yamekujaaa.... si bora ya huyo aliyejenga rami mbovu kuliko waliotorosha mapesa yenu nje ya nchi na bado mkawakumbatia.

Kama huna cha kuchangia usijaze junks hapa.
 
Nonsense,

Huna Mpya, majungu yamekujaaa.... si bora ya huyo aliyejenga rami mbovu kuliko waliotorosha mapesa yenu nje ya nchi na bado mkawakumbatia.

Kama huna cha kuchangia usijaze junks hapa.

Kwa mitizamo hii no wonder ROSTAM, MRAMBA na CHENGE wanashinda kwa kishindo.....
 
Anyisile Obheli, Hata mimi simwelewi elewi huyu Karugendo. Alitaka magufuli achote hiyo mihela na kuipeleka ufukweni ama Uarabuni?????????? Amefanya maendeleo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa TZ na waTZ wote wanafaidika.
Kuhusu suala la Chato kuletwa mkoa mpya wa Geita, mbona hata kule kwa Mizengo Pinda huo mkoa nao umetengwa, kwa maana hiyo Magufuli napo ameingilia huko.Karugendo ana chembechembe za ukabila, hakuna kingine kinachomsukuma.

Ina maana huoni kabisa kuwa alichofanya Magufuli ni aina ya ufisadi unaokiuka misingi ya uongozi kwa ajili ya mslahi yake binafsi kisiasa? Mbona mnashangaa ya Mramba kushinda uchaguzi akiwa na kesi ya kujibu ya ufisadi. Hujui kuwa aina hii ya uongozi ndiyo inayojenga wanasiasa hovyo katika constituent zao na huku wanaendelea kuhujumu maslahi ya taifa.

Una uhakika gani kuwa Magufuli hakupigania kuitoa chato katika Kagera kwa misingi na maslahi ya kikabila kwa kuwa anaamini kuwa wao ni wasukuma zaidi kuliko wahaya? By the way kama kuna mtu ana prejudices za kirangi, kikabila na hata kidini Magufuli ni mmoja wao. Padre Karugendo ni mfano wa kuigwa wa watanzania waliokumbatia uzalendo wa kweli ulio above petty prejudices zilizowajaa baadhi ya viongozi wetu wanaojifaragua na uzalendo.

omarilyas
 
kaka2002,chaMtuMavi,Anyisile,Bill,

..mimi sina tatizo na jimbo la Chato kujengewa barabara ya lami. lakini naamini hiki kitendo alichofanya Magufuli, cha kutumia madaraka yake, na kulazimisha ujenzi wa barabara uelekee jimboni kwake ni kinyume na kiapo chake cha utumishi.

..huyu hana tofauti na wale watu wasiokuwa na uungwana ambao huruka foleni ya chakula, au kuchukua fedha benki, au kwenye taa za barabarani, lakini yeye Magufuli amefanya hivyo kwenye mradi wa maendeleo/barabara. hii inaweza kuonekana ni kitendo "powa" kama wewe ni mwananchi wa Chato, lakini kama wewe ni mwananchi wa eneo ambalo limepokonywa mradi huo sidhani kama utamsifia Magufuli.

..aliyoyafanya Magufuli ndiyo anayoyafanya Kawambwa sasa hivi amelundika miradi kibao Bwagwamoyo hana habari na maeneo mengine ya Tanzania. sijui hata tunaelekea wapi.

..sasa tabia hii ya Mawaziri kupokonya miradi ya maendeleo haikuanza na Magufuli. lakini tulimheshimu sana Magufuli na hatukutegemea kwamba hatatumbukia katika uchafu huo.

..Padri Karugendo ana hoja ya msingi hapa. taarifa alizozileta zinaelekeza kwamba MAGUFULI ana nuka RUSHWA, UKABILA, na UPENDELEO. kudai kwamba ana afadhali kwasababu amejenga barabara ya lami hata kama ni feki-feki ni sawa na wale wanaoona chongo wakaita kengeza.

NB:

..hata Raisi Mwinyi wakati anaondoka madarakani alimsifia sana Nalaila Kiula[waziri wa ujenzi], kwa uchapakazi. alipokuja kuchunguzwa ikakutwa ana madudu kibao.
 
sawa joka kuu,
hata miye sikupingi, ila ninachokiona mimi, hapo hakuna tatizo, is just like the way to make Maghufuli to be seen as others whos made grow their outside A/c, bila kujari kuwa lile ni jasho la wanajamhuri ya muungano, hata kama hiyo barabara ilitakiwa kujengwa Maswa lakini mbunge akapindua na kuijenga Rungwe mi kwangu ni sawa, maana kitaifa maendeleo ya Maswa ni ya Rungwe,
na Rungwe ni ya Maswa, mimi mtazamo wangu hapo kama Padre Karugendo angekuwa na maarifa B ambayo yangeyahoji maarifa A basi hapo jambo kuu na kuhoji ni kwani serikali chini ya Maghufuli imemlipa mkandarasi aliyejenga barabara kwa kiwango kibovu na si vinginevyo
 
... hiki kitendo alichofanya Magufuli, cha kutumia madaraka yake, na kulazimisha ujenzi wa barabara uelekee jimboni kwake ni kinyume na kiapo chake cha utumishi.
Hata mimi ningekuwa Mbunge halafu ukanipa uwaziri ningefanya vivyo hivyo. Nina kiapo cha kujenga kwetu (Mbunge) nina kiapo cha kutumikia Taifa zima (Waziri). Msahafu wa biblia unasema huwezi kutumikia wake wawili. Tatizo ni Katiba.

Wewe JokaKuu ungefanyaje? Ungeepukaje mgongano wa kimaslahi huo? Usipopeleka barabara kwenu makusudi maana yake uwaziri umekinza kazi na kiapo chako cha ubunge, toka kwenye ubunge. Ukipeleka barabara kwenu kwanza, umeshindwa kufikiria Taifa zima, jiuzulu uwaziri. Ukikaa hufanyi chochote, we zobe, toka! Ukisimama nchale, ukikaa nchale, ukikimbia nchale.

Na ndio wa kina Mramba walivyojenga makwao. Na mawaziri wengine wengi tu, labda wote toka Katiba iandikwe. Sijali kama namtetea Magufuli, japo Magufuli ni mchemshaji mkubwa tu. Natetea Katiba, Katiba ni kubwa kuliko Magufuli. Hata kwenye matokeo ya kesi ya Mgombea huru nilisema nimesikitika mno, hata majaji waliandika wamesikitika, lakini walikuwa sawa kabisa, tatizo ni Katiba.

Tupige kelele Katiba irekebishwe, Mbunge asiwe Waziri.


..hata Raisi Mwinyi wakati anaondoka madarakani alimsifia sana Nalaila Kiula[waziri wa ujenzi], kwa uchapakazi. alipokuja kuchunguzwa ikakutwa ana madudu kibao.
Kiula alishinda kesi mahakamani, sitamwita fisadi. Japo inawezekana kweli kakwiba! Katiba inasema usimwite mtu mwizi kamwe iwapo umemwona mahakamani hana hatia. Naheshimu sana misingi ya sheria na Katiba. Katiba ni kubwa kuliko Nalaila Kiula.
 
Hiyo bara bara ilipopitishwa ndipo ilipostahili toka wakati wa mwinyi ila hiyo plan anayoiongea Karungendo ndo njama yenyewe iliyokuja baadae kumumaliza MP Magufuli.
 
Hivi mnajua klichompa ushindi wa kishindo Mramba? Wakati akiwa Waziri wa Miundo Mbinu alilazimu barara ya kuelekea jimboni mwake kuwekewa lami wakati ambapo haikuwepo katika plan za serikali. Wabunge wenzake walimjia juu na hata kutishia kuzuia ajeti ya wizara yake lakini mwishoni kama CCM wakaongea na kuyamaliza. Leo hii Mramba anawakejeli consience ya watanzania na kuwa role model kwa viongozi wajao....Athari ya kuhalalisha uvunjaji misingi ya uongozi kama wafanyavyo kina magufuli na mramba ni kubwa mno kwa hatima ya Taifa...Ni kujenga utamaduni wa kisiasa unaojali ujanjaujanja miongoni mwa wapiga kura na hivyo kuendelea kuwapa uhalali wa kisiasa maadui wa ndani wa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

omarilyas
 
..mwandishi anaelezea aliyoyaona na kuyasikia Chato, jimboni kwa waziri Magufuli.


..ni tuhuma nzito za upendeleo,ukabila, na rushwa.


..ninapata wasiwasi kwamba ukiamua kumchunguza kwa umakini Pombe Magufuli unaweza ku-conclude kwamba ni "mchanyato" wa kiula,msuya, na mramba.


..wengine wanafikiri anafaa kuwa Waziri Mkuu au hata Raisi.

Hayo ya chato,Kiula na Mramba siwezi kuyaongelea,lakini hili la Msuya nitalitetea. Kwanza watu wa wilaya ya mwanga ambayo wengi hawajui kuwa ipo milimani na siyo barabarani [moshi-Dar] ni wachapakazi wazuri. Watu hawa walianza kujiletea maendeleo miaka ya mjerumani kwa kitu kinachoitwa ''msaragambo'' yaani shughuli za umma kwa kujitolea ingawa kama hushiriki unapigwa faini. Wamejenga barabara kwenye milima kwa mikono yao kabla ya mwingereza hajafika. Walianza kujenga shule zao ikiwa ni pamoja na zile za dini miaka ya 1900. Hawakubaguana kwa misingi hiyo. Walikuwa wakulima wazuri wa kahawa ,ndizi n.k. Ushindani wao ulikuwa ni kusomesha watoto,yaani mzazi kama huna mtoto aliyekwenda school basi ni failure kwako.
Msuya alikuwa kiuongozi mzuri, siku moja aliambiwa wilaya nzima inapata nafasi 62 za sekondari ikilinganishwa na wanafunzi maelfu wanaomaliza darasa la saba. Aliwajibu wananchi,ongezeni shule zenu za private, na wananchi wakamsikiliza. Leo hii mpango wa sekondari za kata ni kiongezeo tu lakini hadi mwaka 2000 kila tarafa ilikuwa na sekondari.
Akaulizwa, hatuna dispensary, akawajibu jengeni ikifika wakati wa kupau muniite wananchi, wakajenga na wakati ulipofika akaleta mabati na wauguzi,leo kila kata at least ina dispensary.
Nguvu ya mheshimiwa msuya ilikuwa ni kuonyesha njia na kuwahamisisha watu wake. Nakumbuka aliwahi kuwaambia wananchi waanzishe Bank yao kwa kujichangia,leo Bank hiyo inafungua matawi mkoa wa Kilimanjaro. Ushawishi wake kwa nafasi yake ni pale palipohitajika msaada ambao wananchi wasingeweza kuutoa. Kwa mfano hili la Bank, yeye alitumia ushawishi ili Bank isajiliwe na sio ipewe pesa na serikali.
Nimetembea Tanzania yote, eti kuna sehemu inahitaji kufyekwa nyasi,basi wananchi wamelala hadi serikali ilete grader. Nendeni kule sehemu za Mbaga, Usangi, Ugweno muone barabara,shule na vituo vya afya vimejengwa kwa nguvu za wananchi. Hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusema katika hotuba zake.
Leo hii yupo profesa Magahembe,ambaye ni waziri kwa miaka kumi, lakini nenda kaangalie Mwanga ilivyodorora. Hana lolote jipya bali kujivunia mafanikio ya akina Msuaya, Kisumo, Marehemu Mgonja[kabla ya kugawa majimbo].
Hizi hadithi mnazosikia kuhusu msuya si kweli, mimi nishahidi kwasababu nimeishi maeneo hayo na asailimia 90 ya sehemu za tanzania.
Mwaka 19.. nikiwa nasoma mkoa wa pwani wananchi walikuwa wanatuita ''wafungwa wa kisiasa'' [sekondari] na wazazi wao walikuwa wanachekelea! leo hii Mkoa wa pwani upo nyuma kimaendeleo kwa kila nyanja ukilinganisha na wilaya ya mwanga.
Waulizeni akina Msabah, JK, Mtulya,n.k wamefanya nini kuzuia midundiko ili watoto wafanye homework. Ni kwanini Mpare au Mchaga aende Kimazichana na afanikiwe kwa kilimo. Waulizeni akiana Jk na wenzake kwanini nanasi moja la pale chalinze liuzwe sh 500,wanafanya nini kuwatafutia soko watu wao. Msuya aliwatafutia soko watu wake kupia KNCU na kuuza kahawa ili walipe ada za watoto wao.
Mbona kule Kagera/Mbeya/ wapo mbele kimaendeleo! msuya antoka huko!
Waulizeni wapogoro kwanini walime mchele kilombero na kisha wakeshe wakicheza ngoma, Msuya aliwaambia watu wake straight on the face'' The best investment in this world is education''
Kama akiamua kugombea tena nitamchagua Msuya, kwa sababu ni kiongozi si mtawala.
 
sijaelewa anashitaki au ana lalamika? hata si makosa kupindisha barabara ikiwa bado inawasaidia wana jamhuri ya muungano hata kama si ilivyokusudiwa

Kwa hiyo barabara ambayo ilikusudiwa kutoka Dar, kupitia Dodoma na kwenda moja kwa moja mpaka Kigoma ukiibadili ukaifanya itoke Dar ipitie Mbeya na kutoka Mbeya ndiyo iende Kigoma itakuwa sawa tu? Si kote kuna wananchi wa Tanzania kwa mujibu wako.

Swala hapa linakuja huu ujanja ujanja umelisababishia taifa hasara kiasi gani, kwa nini watu wanafanya mambo kijanja janja hivi ?

Mimi siku zote namuona John Magufuli kama fraud tu anayejua kujionyesha kama mchapakazi wa kweli lakini hana lolote la maana.
 
Hayo ya chato,Kiula na Mramba siwezi kuyaongelea,lakini hili la Msuya nitalitetea. Kwanza watu wa wilaya ya mwanga ambayo wengi hawajui kuwa ipo milimani na siyo barabarani [moshi-Dar] ni wachapakazi wazuri. Watu hawa walianza kujiletea maendeleo miaka ya mjerumani kwa kitu kinachoitwa ''msaragambo'' yaani shughuli za umma kwa kujitolea ingawa kama hushiriki unapigwa faini. Wamejenga barabara kwenye milima kwa mikono yao kabla ya mwingereza hajafika. Walianza kujenga shule zao ikiwa ni pamoja na zile za dini miaka ya 1900. Hawakubaguana kwa misingi hiyo. Walikuwa wakulima wazuri wa kahawa ,ndizi n.k. Ushindani wao ulikuwa ni kusomesha watoto,yaani mzazi kama huna mtoto aliyekwenda school basi ni failure kwako.
Msuya alikuwa kiuongozi mzuri, siku moja aliambiwa wilaya nzima inapata nafasi 62 za sekondari ikilinganishwa na wanafunzi maelfu wanaomaliza darasa la saba. Aliwajibu wananchi,ongezeni shule zenu za private, na wananchi wakamsikiliza. Leo hii mpango wa sekondari za kata ni kiongezeo tu lakini hadi mwaka 2000 kila tarafa ilikuwa na sekondari.
Akaulizwa, hatuna dispensary, akawajibu jengeni ikifika wakati wa kupau muniite wananchi, wakajenga na wakati ulipofika akaleta mabati na wauguzi,leo kila kata at least ina dispensary.
Nguvu ya mheshimiwa msuya ilikuwa ni kuonyesha njia na kuwahamisisha watu wake. Nakumbuka aliwahi kuwaambia wananchi waanzishe Bank yao kwa kujichangia,leo Bank hiyo inafungua matawi mkoa wa Kilimanjaro. Ushawishi wake kwa nafasi yake ni pale palipohitajika msaada ambao wananchi wasingeweza kuutoa. Kwa mfano hili la Bank, yeye alitumia ushawishi ili Bank isajiliwe na sio ipewe pesa na serikali.
Nimetembea Tanzania yote, eti kuna sehemu inahitaji kufyekwa nyasi,basi wananchi wamelala hadi serikali ilete grader. Nendeni kule sehemu za Mbaga, Usangi, Ugweno muone barabara,shule na vituo vya afya vimejengwa kwa nguvu za wananchi. Hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusema katika hotuba zake.
Leo hii yupo profesa Magahembe,ambaye ni waziri kwa miaka kumi, lakini nenda kaangalie Mwanga ilivyodorora. Hana lolote jipya bali kujivunia mafanikio ya akina Msuaya, Kisumo, Marehemu Mgonja[kabla ya kugawa majimbo].
Hizi hadithi mnazosikia kuhusu msuya si kweli, mimi nishahidi kwasababu nimeishi maeneo hayo na asailimia 90 ya sehemu za tanzania.
Mwaka 19.. nikiwa nasoma mkoa wa pwani wananchi walikuwa wanatuita ''wafungwa wa kisiasa'' [sekondari] na wazazi wao walikuwa wanachekelea! leo hii Mkoa wa pwani upo nyuma kimaendeleo kwa kila nyanja ukilinganisha na wilaya ya mwanga.
Waulizeni akina Msabah, JK, Mtulya,n.k wamefanya nini kuzuia midundiko ili watoto wafanye homework. Ni kwanini Mpare au Mchaga aende Kimazichana na afanikiwe kwa kilimo. Waulizeni akiana Jk na wenzake kwanini nanasi moja la pale chalinze liuzwe sh 500,wanafanya nini kuwatafutia soko watu wao. Msuya aliwatafutia soko watu wake kupia KNCU na kuuza kahawa ili walipe ada za watoto wao.
Mbona kule Kagera/Mbeya/ wapo mbele kimaendeleo! msuya antoka huko!
Waulizeni wapogoro kwanini walime mchele kilombero na kisha wakeshe wakicheza ngoma, Msuya aliwaambia watu wake straight on the face'' The best investment in this world is education''
Kama akiamua kugombea tena nitamchagua Msuya, kwa sababu ni kiongozi si mtawala.

Ha ha ha!
 
Kwa hiyo barabara ambayo ilikusudiwa kutoka Dar, kupitia Dodoma na kwenda moja kwa moja mpaka Kigoma ukiibadili ukaifanya itoke Dar ipitie Mbeya na kutoka Mbeya ndiyo iende Kigoma itakuwa sawa tu? Si kote kuna wananchi wa Tanzania kwa mujibu wako.

Swala hapa linakuja huu ujanja ujanja umelisababishia taifa hasara kiasi gani, kwa nini watu wanafanya mambo kijanja janja hivi ?

Mimi siku zote namuona John Magufuli kama fraud tu anayejua kujionyesha kama mchapakazi wa kweli lakini hana lolote la maana.
Kwa hiyo barabara ambayo ilikusudiwa kutoka Dar, kupitia Dodoma na kwenda moja kwa moja mpaka Kigoma ukiibadili ukaifanya itoke Dar ipitie Mbeya na kutoka Mbeya ndiyo iende Kigoma itakuwa sawa tu? Si kote kuna wananchi wa Tanzania kwa mujibu wako.

Swala hapa linakuja huu ujanja ujanja umelisababishia taifa hasara kiasi gani, kwa nini watu wanafanya mambo kijanja janja hivi ?

Mimi siku zote namuona John Magufuli kama fraud tu anayejua kujionyesha kama mchapakazi wa kweli lakini hana lolote la maana.
sawa mkuu Kiranga,
we unaona ni tatizo, hivi nikuulize swali hivi hiyo imejengwa Bukavu nchini DRC ama?
harafu punguza jazba kwa kila kitu, utapasuka bure, na kama hasara basi hakuna mtu wa kumnyoshea mwenziye kidole,, je hili Maghufuli ni kosa kubwa sana kiasi hicho?
mi ninavyo ona posti zako nyingi, naona kabisa kuwa unaongozwa na hasira/jazba zaidi
usitake kutuletea mtazamo wako kuwa mtazamo wa taifa, Maghufuli hata kama hana lolote kama unavyodai basi ana afadhari kuliko bosi wake
 
Sielewi mnacholalamika..huezi ukalalmikia hiyo version ya lobbying huku ukiacha kuangalia mzizi wa tatizo lenyewe ambalo ni kukumbatia utendaji wa kisiasa badala ya dira na masterplan za kitaalam.
 
Sielewi mnacholalamika..huezi ukalalmikia hiyo version ya lobbying huku ukiacha kuangalia mzizi wa tatizo lenyewe ambalo ni kukumbatia utendaji wa kisiasa badala ya dira na masterplan za kitaalam.

Hayo mambo ya masterplan za kitaalam unayajua wewe, unamuona mjomba mjomba wambwela huyu hapa chini, anakwambia barabara inayotoka Dar kukata katikati mpaka Kigoma uki i divert kuipeleka mbeya halafu kuirudisha Kigoma ni poa tu, as long as haiendi DRC.

Nina mashaka hata kama ramani ya Dar, Kigoma na Mbeya zilivyokaa huyu anaielewa.Yeye kashamchunuku Magufuli kwa hiyo ukisema maneno ya masterplan anakuona mzushi tu.

Anyisile Obheli kaandika haya maneno hapo chini bila hata ya aibu, halafu anajaribu ku justify mambo ya Magufuli kwa relativism, two wrongs do not make a right, tutasema hili mara ngapi jamani ?

sawa mkuu Kiranga,
we unaona ni tatizo, hivi nikuulize swali hivi hiyo imejengwa Bukavu nchini DRC ama?
harafu punguza jazba kwa kila kitu, utapasuka bure, na kama hasara basi hakuna mtu wa kumnyoshea mwenziye kidole,, je hili Maghufuli ni kosa kubwa sana kiasi hicho?
mi ninavyo ona posti zako nyingi, naona kabisa kuwa unaongozwa na hasira/jazba zaidi
usitake kutuletea mtazamo wako kuwa mtazamo wa taifa, Maghufuli hata kama hana lolote kama unavyodai basi ana afadhari kuliko bosi wake
 
Back
Top Bottom