PAC yashtushwa na mtaji wa 150,000 wa mwekezaji Mlimani City

Vitu vingine ni aibu hata kuvisema. Jamani hivi Watanzania Elimu yetu inatufaa kweli? Uwozo unaozidi kugunduliwa ni aibu kubwa kwa taifa. Mambo haya yote maovu yakitendeka maprofessor walikuwa wapi? Rais alikuwa wapi? Vyombo vya sheria vilikuwa wapi? Siwezi kuuliza Watanzania walikuwa wapi, Kwani tulikuwa tumewekwa gizani. Wizi uliokuwepo Tanzania MUNGU tu anayejuwa. Nashangaa cabinet ya Kikwete wote wako huru. Tanzania ni nchi mojawapo muhindi anakuja na briefcase tupu anaondoka billionea akisaidiwa na Viongozi wetu Wakati Watanzania wasota na maisha magumu. MARAIS waliopita wasikaze kisabuni mumewatesa Watanzania kwa vitendo vyenu, kazi ya urais mlikuwa hamuiwezi
Tuwashangae wote wanaosema 'madudu yanagunduliwa'. Yanagunduliwa vipi haya kwa sasa wakati yakitendeka watu walipigia kelele wizi huo wa wazi; lakini masikio yao yalizibwa na waliopiga kelele waliitwa wapinzani. Sasa wao wamegeuka na 'kuyaona' hayo madudu na wale walioyasema huko nyuma wanaitwa wachochezi na siyo wazalendo. What a crooked world.
 
ile karma ya watumishi hewa bado mbichi sana......nchi hii watu wanaamini makaratasi kuliko uwezo...kuwa na phd ni jambo moja but kuitumia hiyo phd kuwa na tija ni issue nyingine kabisa...nchi hii ina maprofessor hewa na phd hewa nyingi....natamani sana Tanzania itakayopima watu kwa uwezo na matokeo badala ya huu upuuzi wa vyeti...kuna majitu ya ovyo ovyo yamejaa kwenye taasisi za umma yanafanya maamuzi ya kibatamzinga kisa masters, na phd....inashangaza sana UDSM inashindwa kusimamia kamlimani city....ndo haya haya maprof uchwara yalikuj na hesabu zao za noah moja moja kwa kila mtz .....yaani bora hata siko huko maana ningekata shingo tu mpaka waliobakie warudishe phd waanze ipya kutafuta weledi....hii nchi inapotezwaga nao wasomi hewa...mnafukuza watu wasio na vyeti vya form 4 bt degree ni zao mnaacha makina lipumba mtaani ...yaani ningewafanya kitu cha*#@#%%#@*##%%
 
Mwekezaji alikuja na $75, kwa hiyo nani kajenga pale Mlimani?
 
Aiseeeee imagine na hapo ndio UDSM.. Home of intellectuals.. na wanaibiwa/wanaiba hivi..!? Sbb hilo ni dili la wazi kabisa, OMG..!!

I believe Mh. Rais wetu atatumbua watu hapa na kuwa kamata akina Mkandara..!! This is shame!! Inatia aibu sana jamani.. Yaani nchi hii, aisee
 
Hii hoja ya kuwa eti mwekezaji alikuja na mtaji wa 150000 ni dhaifu kbs. Wenzetu huwa hawaangalii mtaji wanachoangalia ni Idea. Mzungu alikuja na idea wakampa ardhi akaenda bank akapata pesa ndo maana leo mlimani city inapeform.
Kamati ya kina Lusinde (zero brain) isiangalie tu investment in terms of money, it should look on idea that investor imposed.
Labda tujadili hoja ya gawio na miaka lkn hii ya alikuja na shilingi ngapi ni si hoja. Mtaji wa kwanza kwa mzungu ni Akili.
 
Mwekezaji alikuja na $75, kwa hiyo nani kajenga pale Mlimani?
Swali hilo lafanana na wale Wadosi Airtel...
Wanadai Mwekezaji alitumia rasilimali za UDSM kuombea mikopo na kujenga hapo!
Ni Tanzania tu kwa kweli, yaani tuna umaskini wa kujitakia kwa kweli...hata hao hao Wazungu wanatushangaa tunapoenda na bakuli kuomba misaada, tunatia aibu...
 
Ni nani alijenga Mlimani City. Ni mwekezaji au serikali?
Aliyejenga ni mwekezaji lakini bila shaka alikopa pesa kutoka mabenki ya ndani na kujenga! Hilo jengo la mlimani city siyo jengo Bali ni banda kubwa! Halina thamani kubwa na life span yake ni ndogo sana. Mkataba ukiisha na jengo litakuwa lime-expire! Ni ajabu na kweli! Mikataba mingi ikiwemo ya madini ambayo imebaki kuwa ni siri ya wanufaika wachache (waliokuwa na dhamana kama vile joka la makengeza), ina vituko ambavyo vikiwekwa wazi hakuna anayeweza kuamini kilichomo!
Ndiyo maana hakuna anayethubutu kuruhusu mikataba ya madini na gesi kupelekwa bungeni!!!
 
Aliyejenga ni mwekezaji lakini bila shaka alikopa pesa kutoka mabenki ya ndani na kujenga! Hilo jengo la mlimani city siyo jengo Bali ni banda kubwa! Halina thamani kubwa na life span yake ni ndogo sana. Mkataba ukiisha na jengo litakuwa lime-expire! Ni ajabu na kweli! Mikataba mingi ikiwemo ya madini ambayo imebaki kuwa ni siri ya wanufaika wachache (waliokuwa na dhamana kama vile joka la makengeza), ina vituko ambavyo vikiwekwa wazi hakuna anayeweza kuamini kilichomo!
Ndiyo maana hakuna anayethubutu kuruhusu mikataba ya madini na gesi kupelekwa bungeni!!!
CCM inafilisi nchi
 
halafu tunawasifia kina Profesa Kabudi, he was the in-house lawyer aliyebariki hii mikataba
 
Another usanii wa kiwango cha lami... udsm ndyo ilotoa aslimia kubwa ya wateule wa sasa does it mean hawakuona huu mtaji?? Serikali iliyoingia huo mkataba ni ya Chama hiki hiki cha sasa haikuona?? Hivi wahusika wa wakati ule na wasasa wanatofauti?? USD 75 ardhi yote ile tuna shida mahali aseee
 
View attachment 678879
Namuona hapo Lusinde akiwa ameshika lisimu likubwa ndani ya Kamati ya Hesabu za Serikali PAC.Dah.



Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kurekebisha mkataba kati yake na kampuni ya Mlimani Holding Ltd kutokana na upungufu uliojitokeza, huku ikihoji sababu ya mwekezaji huyo kuja na mtaji wa Sh150,000 tu.


Wakizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichoketi eneo la Mlimani City jijinj Dar es Salaam leo Januari 18 wajumbe wa PAC walikosoa pia gawio la asilimia 10 la mapato yote kwa mwaka ambapo Mlimani City wamekuwa wakikata gharama zao kabla ya kulipa.


Jambo la tatu lililolalamikiwa ni umri wa mkataba ambapo UDSM imetaka upunguzwe kutoka miaka 50 hadi miaka 35.
Mbunge wa Magomeni (CCM) Zanzibar, Jamal Kassim amehoji sababu za chuo hicho kumpokea mwekezaji akiwa na mtaji wa Sh150,000.


"Ukisoma mkataba huu utaona mtaji wa mwekezaji ni Sh150,000 yaani Dola 75. Maana yake mwekezaji hakuja na pesa bali alichukua pesa za upangishaji na kuzifanya kuwa mkopo na anajilipa riba ya mabilioni ya fedha," amesema Kassim.


Mwenyekiti wa kamati hiyo, Naghenjwa Kaboyoka amehoji: "Je, Chuo kikuu cha Dar es Salaam kilimkubalije mwekezaji mwenye mtaji wa Dola 75 tu? Dhamana ilikuwa nini?"
Hoja hiyo ilimwibua Mbunge wa CCM (Vijana) , Khadija Naasir akihoji sababu ya mwekezaji huyo kutuma barua pepe kila anapotakiwa kutoa maelezo na UDSM.


Mbunge wa Ulanga Magharibi Dk Haji Mponda amesema mkataba huo ni mbovu kwa sababu umeshindwa kuna ardhi iliyopangishwa bila kutumika kwa muda mrefu.


Baada ya hoja za wabunge hao, Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Hilal Aeshi ameitaka kamati kuwaita watumishi wa UDSM walioshiriki kusaini mkataba huo ili wahojiwe na kuchukulia hatua.


"Kwa kuwa waliotia saini mkataba huo wapo, tuwaite Dodoma, wajieleze ili wachukuliwe hatua na Rais. Mimi nilikuwa mjumbe wa kamati ya madini ya Spika, tuliwaita waliohusika wakajieleza," amesema Aeshi.


Hata hivyo baadhi ya wabunge walitaka viongozi wa sasa wa UDSM wajieleze kabla ya kuwaita wa zamani.
Tofauti na mtazamo wa wabunge hao, Naibu Makamu mkuu wa chuo hicho anayeshughulikia utawala, Profesa David Mfinanga amekiri kuwa mkataba huo una mapungufu na kwamba wana mgogoro na Mlimani Holding.


Mwanasheria wa Chuo hicho, Profesa Bonaventure Rutinwa amesema tangu alipoteuliwa alianza kuupitia mkataba huo.
"Tangu nilipoteuliwa mwaka jana nilifika ofisini kwa Profesa Rwekaza Mukandala nikamuomba vipaumbele vitano vya kisheria, mojawapo akaniambia ni kuupitia mkataba wa Mlimani," amesema Profesa Rutinwa.


Akifafanua zaidi, Kaimu Katibu wa Baraza la Chuo hicho, Dr Saudin Mwakaje alikiri kuwepo tatizo la mtaji na kwamba walishaiambia kamati hiyo.


Awali Mkurugenzi wa mipango na maendeleo wa chuo hicho, Pancras Pujuru amesema Mlimani Holding iliingia mkataba huo mwaka 2004 ukiwa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza ulihusu kati yake na UDSM na sehemu ya pili ilikuwa kati yake na Serikali kupitia kituo cha
Hawa hawana mpango wowote kazi yao kubwa kuwaza matumbo yao huku nchi ikiteketea kwa sababu ya udhaifu wa muhimili wanaoutumikia
 
Hii hoja ya kuwa eti mwekezaji alikuja na mtaji wa 150000 ni dhaifu kbs. Wenzetu huwa hawaangalii mtaji wanachoangalia ni Idea. Mzungu alikuja na idea wakampa ardhi akaenda bank akapata pesa ndo maana leo mlimani city inapeform.
Kamati ya kina Lusinde (zero brain) isiangalie tu investment in terms of money, it should look on idea that investor imposed.
Labda tujadili hoja ya gawio na miaka lkn hii ya alikuja na shilingi ngapi ni si hoja. Mtaji wa kwanza kwa mzungu ni Akili.
Ww naona ni walewale tu! sasa hapo chuoni hakuna ma phd holder na wanafanya nn km hata kuwa idea km hiyo ya kujenga shoping malls walikua hawana. Alipo kuja huyo mwekezaji na idea yake huku hana mtaja si wangempiga chini wakasimamia wao.Kwa hapo broo hakuna la kujitetea tuna wasomi fekiiiiii ambao elimu haijawakomboa sio siri naionea sana huruma Tz Yetu km ndo wasomi dizain ya vyuo vyetu tunaowategemea.FULL KUKARIRI TU.
 
Hii hoja ya kuwa eti mwekezaji alikuja na mtaji wa 150000 ni dhaifu kbs. Wenzetu huwa hawaangalii mtaji wanachoangalia ni Idea. Mzungu alikuja na idea wakampa ardhi akaenda bank akapata pesa ndo maana leo mlimani city inapeform.
Kamati ya kina Lusinde (zero brain) isiangalie tu investment in terms of money, it should look on idea that investor imposed.
Labda tujadili hoja ya gawio na miaka lkn hii ya alikuja na shilingi ngapi ni si hoja. Mtaji wa kwanza kwa mzungu ni Akili.
Upuuzi... Yaani uje na vihela vyako mbuzi uhonge wapumbavu wachache upewe ardhi yetu kijinga uende bank pengine za ndani uchukue hela alafu usifie idea? Kumbaaafu in tz ardhi yote ni ya raisi # Mrpresident we need our land at mlimani city
 
Watanzania tusiwe wanafki kwenye hili mtu amecreate idea na akaweza kuandaa proposal na kuipresent ipasavyo mpaka UDSM wakampa ardhi kutekeleza idea yake then taasisi nyingine ndio ichukuwe huo mradi na kuutekeleza it's not good

Cha kuhoji hapo ni mikataba waliyoandikishiana ili kuwa fair in both side but kujaji kwamba why udsm hawakujenga wenyewe ni unafki na wivu wa maendeleo ya mtu

Poor thinking ndio maana hatuendelei.
 
Back
Top Bottom