Opinion: Ubunge wa Afrika Mashariki, Washindi ni Hawa?!

Hii thread imekwenda shule na inaleta raha, hasa CV za baadhi ya wagombea wetu ambao wana elimu na uzoefu wa kutosha. Wakuu hebu tusaidiane kujua Watanzania tuna matatizo gani? Hebu tupime elimu, uzoefu na uwezo wa wanasiasa wa Kenya, Uganda na hata Rwanda na walivyotumia sifa hizo katika maendeleo ya Taifa, ama walivyoharibu. Tuanze na walipo madarakani kwa sasa akiwamo Makamu wa Rais Dk. Mohamed Bilal, Omar Nundu, Profesa Maghembe, Profesa Kapuya, Dk. Shukuru Kawambwa,Profesa David Mwakyusa, Profesa Mark Mwandosya, Makame Mbarawa, Dk. Haji Mponda, Dk. Lucy Nkya, Profesa Ibrahimu Lipumba, Dk. Slaa, Dk.Sengondo Mvungi etc. Naomba tuangalie waliotumia vyema elimu tuwalinganishe na hawa wanaoomba sasa. Halafu tuangalie majukumu yao huko waendako ni yapi, kama yanalingana na uwezo wao na je, changamoto zilizopo ni zipi? Je, changamoto hizo zinahitaji watu wa aina gani? Je, waliopo wanakidhi matakwa ya changamoto hizo? Dunia sasa inaelekea wapi? Afrika Mashariki inaelekea wapi? Tanzania tumezidiwa nini na wenzetu na kama watakaochaguliwa wataweza kusaidia kuhimili kasi ya mageuzi ya sasa. Tuendelee.
 
....
By :
CCM's Publicity and Ideology Secretary, Nape Nnauye allayed members fears saying that matter had been discussed earlier, with reference to Uganda's case and that Tanzania is on the right track. Announcing the results of the election, Prime Minister Mizengo Pinda the following women from Zanzibar won; Septuu Nassor with 177 votes. Safia Ali Rijaal and Mariam Usi Yahaya won with 169 and 179 votes respectively.
By :
The men from Zanzibar who were declared winners included; Said Bilal, 197 votes. Abdallah Ali Mwinyi scooped 187 votes while Zuber Ali Maulid came through with 176 votes. Dr Haji Mwita Haji with 168 votes beat Amada Khatibu by one vote. Last but not least was Hamis Jabir Makame with 143 votes.
From the mainland Angela Kizigha topped the list with 160 votes was followed closely by Fancy Nkuhi, and Shyrose Bhanji with 147 1nd 145 votes respectively. Janeth Mmari won 133votes while Janet Mbene and Godberha Kinyondo almost came to a tie with 116 and 115 votes respectively.
For the men from mainland Adam Kimbisa garnered 196 votes. Dr Edmund Mndolwa came second with 159 votes. Siraju Kaboyonga with 153 votes, beat Bernard Mulunyaby ten votes. Even tighter was the four votes William Malecela had over Elibariki Kingu's 132 votes. Likewise Evance Rweikiza's 125 votes against Mrisho Gambo's 121. Charles Makongoro Nyerere came through with 113 votes.
All the contestants had to express themselves in English for three minutes each before the delegates and party leaders.
The endorsement of CCM's members Parliament came at a time when Uganda's Attorney General was at the EAC Secretariat in Arusha seeking court guidance and interpretation of how the Ugandan Parliament should elect members to represent the country at EALA


Baada ya kupima vigezo nilivyovieleza, hebu tuangalie hapo juu jinsi kura zilivyopigwa na hao ni wabunge wa CCM ambao ndio wengi bungeni, utaona kuna kila dalili matokeo yakafanana sana na hayo hapo juu na tofauti ikawa ndogo kulingana na karata za mwisho watakazocheza wagombea na zaidi maelezo ya mwisho mbele ya wabunge wote na hatari inaweza kuwakumba watakaoteleza katika kujibu maswali dakika za mwisho. Siasa za makundi ndani ya CCM nazo zinaweza kuwaumiza wagombea vijana kama hapatakuwa na umakini na Utaifa zaidi katika upigaji kura.
 
Baada ya kupima vigezo nilivyovieleza, hebu tuangalie hapo juu jinsi kura zilivyopigwa na hao ni wabunge wa CCM ambao ndio wengi bungeni, utaona kuna kila dalili matokeo yakafanana sana na hayo hapo juu na tofauti ikawa ndogo kulingana na karata za mwisho watakazocheza wagombea na zaidi maelezo ya mwisho mbele ya wabunge wote na hatari inaweza kuwakumba watakaoteleza katika kujibu maswali dakika za mwisho. Siasa za makundi ndani ya CCM nazo zinaweza kuwaumiza wagombea vijana kama hapatakuwa na umakini na Utaifa zaidi katika upigaji kura.

Pasco,Halisi,Geza Ulole,Keil,

..naomba CV za Nkuhi na Shy-rose ili tuweze kujua ni vigezo gani vimetumika kuwapa kura na kumzidi PhD holder Dr.Kinyondo.
 
Ubunge wa Afrika masharaiki ni uwakiishi wa nchi katika jumuiya. Kwa mtazamo wangu Tunahitaji watu wa kusimamia masilahi ya nchi kuliko vyama. Ukifuatilia kuna agenda kwa baadhi ya wanachama kuhusu mweleko wa Jumuiya.
Tunahitaji watu wenye uweledi wa hali ya juu ambao peke yao wanaweza kusimama bila kutegemea hadidu rejea za serikali

Tunahitaji watu wanaoweza kusoma alama za nyakati, mwelekeo wa dunia na thamanai za taifa letu. Watu watakaoweza kujenga hoja na hoja zikasimama zenyewe. Hapa hatuhitaji majina bali wasifu wa mgombea ambaye si CCM, CDM n.k

Nakiri kuwa baadhi ya wagombea sijui sifa zao, lakini haitaniuzuia kutaja baadhi ya sifa za wagombea
Awali niseme sikubaliani na hoja ya 'young or energetic'. Tuzingantie uwezo kwanza. Nina mifano kila siku kuwa bunge la sasa lina vijana wengi, je wamefanya kitu gani tofauti na lile la zamani? Vijana wenyewe si akina Lusinde!!

Adam Kimbisa: Huyu amewahi kuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam. Hakuna chochote anachoweza kutonyesha kuhusu uwezo wake wa kazi. Muda wake wote hali ya jiji imezidi kuwa mbaya. Meya asiyeweza kutafuta suluhu ya maji kujaa Pamba house hawezi kutusadia katika medani kubwa ya uwakilishi.

Twaha Issa Taslimu: Huyu ni mwanasheria aliyebobea. Mtazamo wake juu ya Tanzania ni mdogo kuliko Uzanzibar.
Sina hakika kama yupo kwa masilahi ya nchi au sehemu ya nchi

Dr Bilal: Huyu ni msomi anayeweza kujenga hoja. Hata kama ana mizigo mingine lakini kiwango chake cha ufahamu na uzooefu katika siasa za pande zote za nchi ni kitu muhimu sana.

Siraju Kabuyonga: Huyu alikuwa mbunge wa CCM, katika michango yake sijaona mahali alipowahi kusimama kidete kwa masilhai ya taifa zaidi ya majibu mazuri ya mh waziri..... Sidhani kama atatusaidia.

Shyrose Bhanji: Amegombea nafasi nyingi ndani ya chama chake na mara nyingi amebwagwa. Sifa yake kuu ni kutokata tamaa katika kulekea ndoto zake za kisiasa.Huenda analo jambo analotaka kulifanya kwa taifa bahati mbaya hajapata nafasi. Ana uzoefu kama afisa mahusiano na sijui hilo linawezaje kulisaidia taifa. Sijui uelewa wake wa mambo ya kitaifa ua kimataifa. Mahusiano yake binafsi na wana jamii yaliyowekwa wazi yanatia wasi wasi ingawaje kila mtu ana maisha binafsi.

C.Makongoro nyerere: Pamoja na kubebwa na jina kubwa la baba yake, uenyekiti wa chama mkoani Mara umempa nafasi nyingine ya kujidhihiri. Kwa sasa amekuwa mwiba mkali kwa chama chake hasa mafisadi. Ameonekana kusimamia utaifa zaidi kuliko chama. Swali ni je elimu yake inatosha kupambana na magwiji wa nchi jirani katika hoja?

W.Malecela( Le Baharia): Huyu kama makongoro anajina kubwa nyuma yake. Sina wasifu wake kwa undani hata hivyo.
Advantage aliyo nayo ni kuwa amejijenga kama yeye kwa kuchanganyika na makundi ya kijamii. Mwingiliano wake na jamii unamweka mahali pa kuwa mtu anayewasiliana na jamii. Pengine hilo pamoja na exposure yake vunaweza kuwa plus.
Tatizo lake ni pale uchama unapotangulia utaifa, na hapa tunahoji, je anaweza kusimamia thamani za taifa hata kama zinapingana na masilahi ya chama chake?

Ni mtazamo binafsi kwa uchache
 
Ubunge wa Afrika masharaiki ni uwakiishi wa nchi katika jumuiya. Kwa mtazamo wangu Tunahitaji watu wa kusimamia masilahi ya nchi kuliko vyama. Ukifuatilia kuna agenda kwa baadhi ya wanachama kuhusu mweleko wa Jumuiya.
Tunahitaji watu wenye uweledi wa hali ya juu ambao peke yao wanaweza kusimama bila kutegemea hadidu rejea za serikali

Tunahitaji watu wanaoweza kusoma alama za nyakati, mwelekeo wa dunia na thamanai za taifa letu. Watu watakaoweza kujenga hoja na hoja zikasimama zenyewe. Hapa hatuhitaji majina bali wasifu wa mgombea ambaye si CCM, CDM n.k

Nakiri kuwa baadhi ya wagombea sijui sifa zao, lakini haitaniuzuia kutaja baadhi ya sifa za wagombea
Awali niseme sikubaliani na hoja ya 'young or energetic'. Tuzingantie uwezo kwanza. Nina mifano kila siku kuwa bunge la sasa lina vijana wengi, je wamefanya kitu gani tofauti na lile la zamani? Vijana wenyewe si akina Lusinde!!

Adam Kimbisa: Huyu amewahi kuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam. Hakuna chochote anachoweza kutonyesha kuhusu uwezo wake wa kazi. Muda wake wote hali ya jiji imezidi kuwa mbaya. Meya asiyeweza kutafuta suluhu ya maji kujaa Pamba house hawezi kutusadia katika medani kubwa ya uwakilishi.

Twaha Issa Taslimu: Huyu ni mwanasheria aliyebobea. Mtazamo wake juu ya Tanzania ni mdogo kuliko Uzanzibar.
Sina hakika kama yupo kwa masilahi ya nchi au sehemu ya nchi

Dr Bilal: Huyu ni msomi anayeweza kujenga hoja. Hata kama ana mizigo mingine lakini kiwango chake cha ufahamu na uzooefu katika siasa za pande zote za nchi ni kitu muhimu sana.

Siraju Kabuyonga: Huyu alikuwa mbunge wa CCM, katika michango yake sijaona mahali alipowahi kusimama kidete kwa masilhai ya taifa zaidi ya majibu mazuri ya mh waziri..... Sidhani kama atatusaidia.

Shyrose Bhanji: Amegombea nafasi nyingi ndani ya chama chake na mara nyingi amebwagwa. Sifa yake kuu ni kutokata tamaa katika kulekea ndoto zake za kisiasa.Huenda analo jambo analotaka kulifanya kwa taifa bahati mbaya hajapata nafasi. Ana uzoefu kama afisa mahusiano na sijui hilo linawezaje kulisaidia taifa. Sijui uelewa wake wa mambo ya kitaifa ua kimataifa. Mahusiano yake binafsi na wana jamii yaliyowekwa wazi yanatia wasi wasi ingawaje kila mtu ana maisha binafsi.

C.Makongoro nyerere: Pamoja na kubebwa na jina kubwa la baba yake, uenyekiti wa chama mkoani Mara umempa nafasi nyingine ya kujidhihiri. Kwa sasa amekuwa mwiba mkali kwa chama chake hasa mafisadi. Ameonekana kusimamia utaifa zaidi kuliko chama. Swali ni je elimu yake inatosha kupambana na magwiji wa nchi jirani katika hoja?

W.Malecela( Le Baharia): Huyu kama makongoro anajina kubwa nyuma yake. Sina wasifu wake kwa undani hata hivyo.
Advantage aliyo nayo ni kuwa amejijenga kama yeye kwa kuchanganyika na makundi ya kijamii. Mwingiliano wake na jamii unamweka mahali pa kuwa mtu anayewasiliana na jamii. Pengine hilo pamoja na exposure yake vunaweza kuwa plus.
Tatizo lake ni pale uchama unapotangulia utaifa, na hapa tunahoji, je anaweza kusimamia thamani za taifa hata kama zinapingana na masilahi ya chama chake?

Ni mtazamo binafsi kwa uchache

Uchambuzi mzuri.
 
Inasikitisha kuona mtu kama wewe unaleta siasa ati mama Janet Mbene na Mndolwa hawafai...Hebu angalia CV zao kwanza na si kupelekewa watu wasiojua chochote kuhusu economic blocks! Kama wakina Fancy Nkuhu na Shyrose Banji

Ahsante Mkuu. Makosa tunayafanya hapahapa kesho tunakuja kujilaumu na kuwalaumu wakenya. Kesho tunapeleka watu ambao hawajui chochote wanasaini miswada ya kutumaliza tunaanza kuwalaumu wenzetu waliopeleka watu makini. EAC inahusu zaidi mambo ya kiuchumi hivyo ni bora tukapeleka watu watakaotusaidia katika hilo na wala si wapiga tarumbeta. Kwamba mtu anajua.publicity basi anafaa, hee kwani EAC wanaenda kugawa madawati.
 
Mkuu Nguruvi, heshima yako sana mkuu wangu ninaomba kusema machache kuhusiana na post yako hasa inaponigusa:-

- Binafsi nimesoma mambo ya Marine Engineering, Criminology na Political Science; nimepata bahati ya kutembelea 90% ya Dunia, nimefanya kazi Europe na USA na pia nilifanya Internship ya mwaka mmoja katika Ubalozi wa Dominican Republic UN, kule New york, kwenye General Assembly; ninaamini haya yote yananipa uzoefu mkubwa sana wa kuweza kuliwakilisha taifa letu EAC.

- EAC tulianza na Customs Union, sasa tupo kwenye Common Market, hivi viwili ni projected as only transitional elements katika kuelekea kwenye One Currency na eventually a Federation. In the process kuna ishus za Land,, Labour, Trade, NTB na mengineyo, I mean kuweka taifa kwanza which is what I always believe in, ninasema hivi:-

- Sio siri kwamba somehow Tanzania, bado hatujajitayarisha vya kutosha na the Competition from our patners States kwenye EAC, na ninaamini sana kwamba wenzetu wanajua hilo na wanajaribu sana kutukimbiza kwenye Federation wakati tukiwa bado hatujajipanga sawa sawa, however bado tunao muda wa kutosha kujipanga na for now ni lazima sana tutumie a Delaying process ili in the process tujipange, kwanza kwenye elimu, tatizo letu la Elimu limetuletea tatizo kubwa la kutokuwa na exposure, halafu ustaarabu wetu wa kibinadam umetufanya tuwe non-aggressive katika kusimamia interest za taifa letu. Tanzania tunahitaji kuuchukulia uwakilishi wetu EAC very serious;

Kwa mfano, ishu kama NTB I mean we can't afford kushusha viwango vya uzito wa malori yanayosafirisha mizigo kwenda kama Kenya na Rwanda wanavyotaka kwa sababu tukishusha viwango ni sisi ndio tutakaoumia kwa sababu Ardhi yetu ni kubwa sana, Lori linahitaji kusaifiri karibu Mile 1,500 kufika baadhi ya mipaka ya wenzetu, wakati wao inahitaji only 200 miles kufika yanapokwenda kwao, sasa tukishusha viwango ni bara bara zetu ndio zitaumia, we can't do this!

- Tanzania tusikubali kabisa maelewano yanayohusu ardhi kwa sababu wenzetu hawana, sasa huhitaji kuwa na PhD kuelewa kwamba huwezi kuwa na urafiki wa ardhi na mtu asiye na ardhi wakati wewe unayo, tukumbuke historia jinsi Wazungu walivyotupa Bibblia, huku wanachukua ardhi yetu, I mean tunaweza na Union bila kushirikisha ardhi mpaka tutakapokuwa tayari na alternative.

- One currency, kwenye hili sijaona Kenya wakiwa aggressive kama kwenye ishus zingine, meaning kwamba hawalitaki kwa sababu hela za Kenya ni kubwa kuliko zote za EAC, sasa this should be a wake up call kwetu kwamba kwenye hizi marathon za one Federation, kuna mitego mingi sana ambayo inaweza kuishia kutuumiza mbele ya safari, sarafu yetu ni hafifu sasa tunaingiaje kwenye one curreny na Kenya? Ndio maana ninasema tunahitaji muda wa kujipanga kwanza.


I mean binafsi ninaamini sana in the Union, kwa sababu it is all about Economy, kusonga mbele kitaifa na hasa wananchi wetu tunahitaji sana the union, lakini ninasema tusiwe na haraka na tusikubali kukimbizwa, twende pole pole na pia tujifunze siasa za give and take, lakini pawepo na nia ya kuwaelimisha wananchi wote wa Tanzania tunafanya nini huko EAC.

William @Dodoma City!
 
Mkuu Willy siku zote ulikuwaa wapi kuyasema haya? Haya ndiyo tunataka yamulikwe huko EAC na siyo kwenda kupiga makofi tu wenzetu wanajenga mikakati ya kuutawala uchumi wa EA kisha watanzani zaidi ya milioni 40 tuwe tu ni soko lao. Mkuu ukumbuke pia kwamba uwingi wetu ni asset, wanautaka huo uwingi kama soko si vinginevyo.
 
Wanatakiwa kuchaguliwa kupitia vyama ni wabunge 9 kutoka tanzania mgawanyo uko hivi wa wanaume CCM bara nafasi 3 na visiwani nafasi 2 na wanawake bara nafasi 2 ambazo zinagombewa na wana ccm 6 na CUF 1 na visiwani moja ambao ni mgombea namba 6,8 na 10 anatakiwa mmoja na vyama vya upizani muakilishi ni mmoja tu kuna kila dalili nafasi hii itakwenda kwa CUF au UDP
 
Ahsante Mkuu. Makosa tunayafanya hapahapa kesho tunakuja kujilaumu na kuwalaumu wakenya. Kesho tunapeleka watu ambao hawajui chochote wanasaini miswada ya kutumaliza tunaanza kuwalaumu wenzetu waliopeleka watu makini. EAC inahusu zaidi mambo ya kiuchumi hivyo ni bora tukapeleka watu watakaotusaidia katika hilo na wala si wapiga tarumbeta. Kwamba mtu anajua.publicity basi anafaa, hee kwani EAC wanaenda kugawa madawati.

- Mkuu ninaomba sana kutofautiana na wewe, kwani hizo CV zenye uchumi zimetusaidia nini Tanzania kwanza? I mean Tanzania tuna wachumi wangapi tena wanaotambuliwa na International Community, eti wametufanyia nini hapa hili taifa? Ni haki ya kila mwananchi kugombea nafasi yoyote ile ya siasa, uchumi bila kujua siasa huwezi kutuwakilisha huko EAC na ukatuletea mafanikio taifa, ni muhimu wawakilishi wetu huko wakajua siasa.

- Ukijua uchumi ni lazima ujue na siasa, kwamba kuna ishus ambazo zitaleta utata huko EAC na wengine watajaribu kuwagawa au kuwa-manipulate into believing kwamba wengine wote wanaunga mkono hoja ni wewe tu ndio hutaki, sasa siasa ni kuibeba ishu kwa wananchi wa Taifa lako waamue na kuwarudia EAC ukiwaambia kwamba wananchi wetu wamekataa, huwezi fanya haya kama hujui siasa,

- Kama hili taifa tumeamua tunataka wachumi tu ndio watuwakilishe EAC, then tubadili the process wachaguliwe na Rais tu, lakini kama ni nafasi yoyote inayohusu siasa ndani yake wananchi waachiwe uhuru wa kugombea, kama tunaoamini kwamba ahwafai basi tuonyeshe mifano ya waliowahi kufaaa huko EAC na CV zao, Great Thinkers tujikite zaidi kwenye haki na fairness badala ya ushabiki wa Yanga na simba.

- Shyrose anaongoza shirika kubwa la benki kama NMB, ameliongoza shirika hilo kwenye kuchangia ishus nyingi sana za maendeleo zinazowagusa wananchi moja kwa moja, madawati, mafuriko, elimu, sasa unaposema hafai exactly unatumia vigezo gani? Kama ameweza kuwaelimisha Wazungu kule NMB kuishirikisha benki yao kuchangia taifa na hasa wananchi wenyewe atashindwa nini kusimamia interest za taifa EAC?

I mean, inanisikitisha sana ninapokaa na wabunge huku Dodoma, wakilalamika kwamba JF ni chombo cha matusi matusi siku hizi zamani ndio walikuwa na hoja sana, people tubadilike kama tunaowapigia kelele tuandike hoja na facts, tuwasaidie viongozi kuja hapa kuchota hoja kama tulivyokuwa zamani, fulani hafai kuwa kiongozi sawa onyesha sababu na onyesha sababu za anayefaa na aliyoyafanyia taifa.

- Otherwise, tunaharibu character za wananchi wasioweza kuja kujitetea bila sababu za msingi, it is unfair!

William @Dodoma City!
 
Sorry, hii thread ilikuwa inasumbua techinical, hivyo nimeihamishia hapa

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nge-wa-afrika-mashariki-washindi-ni-hawa.html

Sorry for any inconveniences caused!

Pascal.

Wanabodi,

Nimekuwepo mjini Dodoma kwa siku mbili tatu. This is my opinion kuhusu Uchaguzi wa nafasi ubunge wa Afrika Mashariki, wagombea gani wana chances zaidi za kushinda na sababu zao za kushinda zikiwemo strength na weaknesses za baadhi yao!.
1. WAGOMBEA WALIOTEULIWA
KUNDI A: WAGOMBEA WANAWAKE
S/ JINA CHAMA
1. Nd. Angela Charles Kizigha CCM
2. Nd. Fancy Haji Nkuhi CCM
3. Dkt. Godbertha Kokubanza Kinyondo CCM
4. Nd. Janet Deo Mmari CCM
5. Nd. Janet Zebedayo Mbene CCM
6. Nd. Maryam Ussi Yahya CCM
7. Nd. Rose Daudi Mwalusamba CUF
8. Nd. Sebtuu Mohamed Nassor CCM
9. Nd. Shy-Rose Sadruddin Bhanji CCM
10. Nd. Sofia Ali Rijaal CCM
My Opinion
Kundi hili wanatakiwa wawili (3). Mbunge bora wa kundi hili ni Fancy Nkuhi kwa sababu ya elimu bora na Shyrose Bhaji kwa sababu ni bingwa wa publicity hivyo kusaidia Watanzania kuifahamu vizuri hii jumuiya. Chances kubwa zimewalalia Janet Mmari na Janet Mbene simply because kuna wazito wanene wanawabeba!. Mmari alikuwepo amefanya nini kustahili kurejea?. Mbene aliteuliwa kuwa mbunge wa kuteuliwa siku chache kabla bunge lililopita halijamalizika, nani anajua sababu ni zipi?, hivyo atachaguliwa Eala kuzikamilisha!. Most unfortunate ni Dr.Godbetha ambaye ni msomi wa Ph.D kwa sababu she belongs to the elite class "mshomile"!
KUNDI B: WAGOMBEA WA ZANZIBAR
S/N JINA CHAMA
1. Nd. Abdullah Ali Hassan Mwinyi CCM
2. Dkt. Ahmada Hamad Khatib CCM
3. Dkt. Haji Mwita Haji CCM
4. Nd. Khamis Jabir Makame CCM
5. Dkt. Said Gharib Bilal CCM
6. Nd. Zubeir Ali Maulid CCM
My Opinion
Kundi hili anatakiwa wawili (2), Dr. Ahmada anasimama more chances na ndiye the best, ila kwa vile siasa za Zanzibar majina ya ubini yana matter sana, kama ilivyokuwa kwa Karume, hakuwa na lolote zaidi ya jina, hivyo naomba msishangae jina la Gharib Bilal ndilo litakapita!.
KUNDI C: WAGOMBEA WA VYAMA VYA UPINZANI
S/N JINA CHAMA
1. Nd. Antony Calist Komu CHADEMA
2. Dkt. Fortunatus Lwanyantika Masha UDP
4. Nd. Juju Martin Danda NCCR-MAGEUZI
5. Nd. Micah Elifuraha Mrindoko TLP
6. Nd. Mwaiseje S. Polisya NCCR-MAGEUZI
7. Nd. Nderakindo Perpetua Kessy NCCR- MAGEUZI
8. Nd. Twaha Issa Taslima CUF
My Opinion
Hapa anatakiwa mmoja (1) the best option ni Komu wa Chadema akifuatiwa na Dr. Fortunatus Masha ila atakayechaguliwa ni Taslima wa CUF kufuatia wabunge wengi ambao ni CCM kuwajibika kumchagua mgombea wa CUF ambaye ni mwana ndoa wao kwenye ile ndoa ya CCM na CUF!.
KUNDI D: WAGOMBEA WA TANZANIA BARA
S/N JINA CHAMA
1. Nd. Adam Omar Kimbisa CCM
2. Nd. Bernard Musomi Murunya CCM
3. Nd. Charles Makongoro Nyerere CCM
4. Dkt. Edmund Bernard Mndolwa CCM
5. Nd. Elibariki Immanuel Kingu CCM
6. Dkt. Evans Mujuni Rweikiza CCM
7. Nd. John Dunstan Lifa-Chipaka TADEA
8. Nd. Mrisho Mashaka Gambo CCM
9. Nd. Siraju Juma Kaboyonga CCM
10. Nd. William John Malecela CCM
My Opinion
Hapa zinatakiwa nafasi 3. The best options hapa ni William, Mrisho na Dr. Rweikiza (The young, vibrant and energetic). Watakao chaguliwa ni Kimbisa, Edmund Mndolwa for connections na Makongoro Nyerere kumuenzi tuu Baba wa Taifa!. (Inaonyesha kuna watu wamekuja na fungu la kufa mtu huwezi amini hata wale ambao huwezi amini kuwa wana vuta, wamevutishwa!).

Hitimisho
Haya ni maoni tuu, matokeo sio lazima yatokee hivi hivyo nawaombeni msinitolee mimacho kama nlivyomtabiria Sioi ushindi kule Arumeru halafu aliyeshinda ni Nasari. Na wewe unaruhusiwa na kutoa maoni yako nani unadhani anafaa zaidi na kwa sababu zipi?, kama kuna mtu unaona hafai au hakupaswa hata kuwepo miongoni mwa wagombea pia unaweza kumtaja na sababu.

NB. Naomba kusisitiza sana, tuwajadili kila mmoja based on the their own merit na sio kuwajadili kwa majina ya baba zao!, baba zao ni baba zao, na wao ni wao ndio maana wamesimama!.

Natanguliza Shukrani.

Pasco.

Pasco na wote waliochangia thread hii mmefanya uchambuzi mzuri.Mgombea achaguliwe kwa sifa na vigezo(elimu(uchumi,sheria,biashara ya kimataifa,utawala),uzoefu na uelewa mpana wa mambo ya economic blocks siyo Eac tu msingi wa hili ni ili uweze kufanya uchambuzi mzuri.
kwenye kundi la kwanza janeth mbene,janeth mmary na fancy nkulu ila chakushangaza katika uchaguzi wa awali Angela Kizigha aliongoza huyu yeye sifa yake ni pesa na siyo hizo sifa hapo juu.Ni form four lever ila kama unavyojua bongo ukiwa na pesa kila unapata kwenye cv yake inaonyesha ana ana masters ya mzumbe ameipataje utajiju.huyu mama amekuwa mfadhili chama.ana uzoefu wowote kwenye mambo yanayohusu Eac lakini kama tujuavyo ccm huyu atapita.mwenye cv yake atupie humu wanabodi waichambue

Mytake:katika hili tunatakiwa kuweka utaifa mbele na wala siyo pesa wala fadhila.
 
William,

1. hili suala la elimu ya wa-Tanzania unapendekeza lishughulikiwe namna gani? naomba ueleze exposure unayoizungumzia ktk muktadha wa elimu ya Mtanzania.

2.kuhusu suala la sarafu, kama hela yetu ni ya chini kuliko ya Kenya maana yake, theoretically, ni kwamba tunaweza kuuza bidhaa nyingi zaidi kwao, kuliko wao wanavyoweza kuuza kwetu. Kitu cha kushangaza ni kwamba mambo ni kinyume na hicho nilichokieleza hapo juu. Je, Tanzania itaweza vipi kubadili mazingira ambapo nchi yetu ni "dampo" la bidhaa za Kenya.

3.Suala la free movement. Kwanini tusifuate model ya NAFTA ambapo Mexicans hawaruhusiwi kuingia USA hovyo-hovyo bila kufuata taratibu za USA? Kwanini unafikiri EU[ulisema unaunga mkono free movement] model ni nzuri kwetu ukizingatia kwamba Tanzania hatuna mfumo wa utambulisho kama SSN na national ID??

4.Ni hatua gani unafikiri zinapaswa kuchukuliwa wakati tuna-slow down the process? wasiwasi wangu ni kwamba tunaweza kufika mahali tukaishiwa sababu na visingizio vya kusema twende polepole.

5.Kuhusu Non-Tariff Barriers[NTB] isiishie kwenye uzito wa magari ya mizigo tu. Kenya wanalazimisha mpaka wa Golongoja ufunguliwe ili waweze kuvusha watalii wao kuingia Serengeti bila Tanzania kupata chochote kile.
 
Pasco,

tunashukuru kwa utafiti wako,unajua hawa watu CCM team,bado akili hazijawa vizuri,ushabiki unazidi kuliko uelewa,bado wanafikiri Ubunge wa Afrika Mashariki nikama Udiwani wa Kata.

Nimezungumza na wengi,bado akili zao zinaelekeza kwenye kubebana zaidi kwa ajili ya masilahi na si ushindani.

Narudia tena CCM watatugharimu sana,iwapo watafanya makosa,kwani wenzetu ni wajanja sana,sitashangaa ushabiki ukiwekwa mbele tayari nayasikia makundi kati yao..

Watu ambao ni Ex wabunge wote hawasitahili,hata wale waliomaliza mda wao.
 
Mkuu Wiliam nimesema tupeleke watu watakaotusaidia katika mambo ya uchumi na sijasema tupeleke wasomi wa uchumi.Mtu anaweza kujua mambo ya uchumi kwa kufanya kazi katika mashirika mbalimbali yaani anakuwa na experiance ama hata exposure tu kwenye mambo hayo. Si lazoma uwe na PHD ya uchumi bali uelewa wa mambo hayo. Ukiamua kugombea nafasi yoyote ya kisias basi wewe ni mwanasiasa hivyo mambo ya political lobbying yanaanzia hapo. Hatutaki kupeleka watu ambao hawajui kiuchumi Tanzania tunataka nini ndani ya JUmuiya, Rwanda, Kenya nk wanataka nini. Ukiyajua hayo basi unaweza kujenga hoja ya kiasiasa na siyo kujenga hoja ya kisiasa bila kujua unaijenga kwenye misingi gani hasa ya kiuchumi.

Tuking'ang'ania siasa tutapigwa bao manake wenzetu watajenga hoja zilizoenda shule siye tunapeleka kiswahili mingi. Tutajikuta tunapwaya. Uchumi ni siasa.
 
William,

1. hili suala la elimu ya wa-Tanzania unapendekeza lishughulikiwe namna gani? naomba ueleze exposure unayoizungumzia ktk muktadha wa elimu ya Mtanzania.

2.kuhusu suala la sarafu, kama hela yetu ni ya chini kuliko ya Kenya maana yake, theoretically, ni kwamba tunaweza kuuza bidhaa nyingi zaidi kwao, kuliko wao wanavyoweza kuuza kwetu. Kitu cha kushangaza ni kwamba mambo ni kinyume na hicho nilichokieleza hapo juu. Je, Tanzania itaweza vipi kubadili mazingira ambapo nchi yetu ni "dampo" la bidhaa za Kenya.

3.Suala la free movement. Kwanini tusifuate model ya NAFTA ambapo Mexicans hawaruhusiwi kuingia USA hovyo-hovyo bila kufuata taratibu za USA? Kwanini unafikiri EU[ulisema unaunga mkono free movement] model ni nzuri kwetu ukizingatia kwamba Tanzania hatuna mfumo wa utambulisho kama SSN na national ID??

4.Ni hatua gani unafikiri zinapaswa kuchukuliwa wakati tuna-slow down the process? wasiwasi wangu ni kwamba tunaweza kufika mahali tukaishiwa sababu na visingizio vya kusema twende polepole.

5.Kuhusu Non-Tariff Barriers[NTB] isiishie kwenye uzito wa magari ya mizigo tu. Kenya wanalazimisha mpaka wa Golongoja ufunguliwe ili waweze kuvusha watalii wao kuingia Serengeti bila Tanzania kupata chochote kile.

1. ELIMU: Tuongeze viwango vya elimu, nimeona pale New York City, mayor akibalisha viwango vya elimu in two years na sasa viwango vipo juu, meaning kwamba inawezekana hata sisi tukiamua kulivalia njuga hilo, wananchi wetu wamepuuza elimu kwa sababu as a Nation tumepuuza pia, sasa kama kweli tunataka ku-compete kule EAC tuongeze viwango vyetu vya elimu, halafu elimu ya Uraia pia, Joka Kuu hatuna njia yoyote nyingine isipokuwa ni sisi wenye kuongeza viwango vya elimu yetu, kumbuka at one point in our Nation's history tulikwua tunaongoza Africa kwa elimu, sasa tujipange tena.

2. SARAFU: the fact kwamba Kenya hawaiguzi hii ishu kabisa ni kwamba hawaitaki kwa sababu wameshajua kwamba itawaumiza, sasa na sisi tujifunze kama wao, tusiingie kwenye sarafu moja mpaka kwanza tumejipanga na uchumi, tuitumie ardhi yetu kutafuta investment toka nje, mimi ninashangaa sana kuona wananchi wengi wana ardhi kubwa sana, lakini ukiwashauri kuitumia wka investment hawataki kabisa, majuzi tulienda nyumbani kwa wazazi wa rafiki yangu sana, kule Mikocheni wana ardhi kubwa sana ya ajabu, nikamshauri mzeee vipi akiruhusu ile ardhi iwe investsted na maghorofa ya kupnagisha, akaniaambia mtoto wake asubiri kwanza yeye afe ndio afanye hayo, sasa with this kind of mentality hatuendi kokotee, as a nation tuamue kufanya changes serious kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi wetu kubadilika na kuanza kuwa na ideas za ku-invest na kuingia ubia na wenye uwezo.

3. FREE LABOUR MOVEMMENT: Ni kweli ninaunga mkono hoja lakini only if it is done rightly, meaning kwamba Serikali yetu lazima isimame kidete na kudai balance tena za kisheria za kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanaaajiriwa huko wka wenzetu, yaani iwe kama an exchange of labour, wenzetu ni wazuri kwenye sekta fulani na sisi ni wazuri kwenye sekta fulani tubadilishane, isiachiwe hiivi hivi tu. Kuhusu EU na US and Mexico, ni kwamba mengi hatuyajui wanayoyafanya hao wenzetu ambayo hawayasemi, uweli ni kwamba wanayafanya isipokuwa kwa vile vyama vyao vyao vya wafanyakazi hawataki ijulikane kwamba wanafanya ndio maana hawasemi. Well, kama tunataka one Federation ni lazima tufike mahali tukubali hii hoja, lakini again ninasema tujipange kwanza na kutafiti kisayansi.

4. DELAY PROCESS: Unajua haya ni lazima yafanyike as a national agenda, with our government serious involvement na very cauciously, kuwe na coordination between wahusika, kuwe na public opinion, taifa lielimishwe tulipo sasa na wenzetu walipo, na what need to be done kuwafikia wenzetu angalau kwa aslimia fulani, kwa sababu ni muhimu sana pia ku-take risks, lakini we cannot afford kukimbia mbio mbio bila kujipanga kwanza, tuwe na priorities ya kuelewa kwamba kama tunataka maendeleo tunaiihitaji EAC, lakini National interest iwe kwanza na tuw wakweli na hali yetu halisi, kama haiwezekani basi tujiondoe kwenye EAC, kuliko kwenda kuwa mzigo na uwanja wa kutumiwa na wenzetu.

5. UTALII: Ninasema kwamba tujiimarishe na sisi kwenye hilo, tujifunze mbinu za wenzetu wao wanatumia sana media kujitangaza na utalii, wana better facilities za utalii kuliko zetu, hapa Tanzania nimeona mahoteli mengi ya kitalii yakiongozwa na wa-Kenya, sawa ni one step, lakini we need to do more again as a nation!

William @Dodoma City!
 
Mkuu tulikuwa tunaongoza Afrika kwa kuwa na asilimia kubwa ya watu wanaojua kusoma na kuandika baada ya yale madarasa ya ngumbaru na siyo kuongoza kielimu Afrika!
 
pasco ningeulizwa na Mungu sasa hivi unataka nini ningemwambia, anionyeshe kwa cv za wanaochaguliwa kuwa wabunge wa hili bunge kutoka kwa wenzetu. pia anionyeshe commitment walizonazo katika kazi hii ndipo sasa ningerudi kuwadiscuss hawa wakwetu.

all in all tunahitaji watu ambao ni committed, na wenye exposure na well educated. pia watu wenye experience kwenye maswala ya kimataifa katika nyanja za uchumi, social, health na communication. lakini shy rose banji kwa kweli hafai kabisa hapa kwanza elimu yake haikumkomboa. manake kama hapa Jaffarai alimzingua hadi ikawa skendo akienda huko akina kidumu si ndo watampagawisha zaid??????????
 
Mkuu Wiliam nimesema tupeleke watu watakaotusaidia katika mambo ya uchumi na sijasema tupeleke wasomi wa uchumi.Mtu anaweza kujua mambo ya uchumi kwa kufanya kazi katika mashirika mbalimbali yaani anakuwa na experiance ama hata exposure tu kwenye mambo hayo. Si lazoma uwe na PHD ya uchumi bali uelewa wa mambo hayo. Ukiamua kugombea nafasi yoyote ya kisias basi wewe ni mwanasiasa hivyo mambo ya political lobbying yanaanzia hapo. Hatutaki kupeleka watu ambao hawajui kiuchumi Tanzania tunataka nini ndani ya JUmuiya, Rwanda, Kenya nk wanataka nini. Ukiyajua hayo basi unaweza kujenga hoja ya kiasiasa na siyo kujenga hoja ya kisiasa bila kujua unaijenga kwenye misingi gani hasa ya kiuchumi.

Tuking'ang'ania siasa tutapigwa bao manake wenzetu watajenga hoja zilizoenda shule siye tunapeleka kiswahili mingi. Tutajikuta tunapwaya. Uchumi ni siasa.

- Mkuu ukweli ni kwamba EAC kama bunge sio ishu sana kwa sababu bado kwenye EAC kuna Sekretarieti ambayo ndio hasa chombo cha kuamua maamuzi ya EAC kiutaalamu, sasa mimi nimeshauri sana kwa wabunge hapa Dodoma na hata kwenye speech yangu bungeni Dar, kwamba tuwe na sheria ya kulazimisha a serious co-ordination kati ya wabunge wa EAC na bunge letu, kuhakikisha kwamba kinachowakilishwa kule ni kitu kinachoeleweka na kukubalika na taifa, kwa sababu kule wenzetu wote wanafanya hivyo.

- Infact katika kuhakikishwa wabunge wao EAc hawarubuniwi, wenzetu wabunge wao EAC hulipwa pia na serikali zao na kuhudumiwa huduma zote muhimu na nchi zao, as opposed na sisi ambayo inatufanya tuwe open kwa kurubuniwa kwenye hoja muhimu sana kwa masilahi yao. Ikiidi wawakilishi wetu huko wapewe washauri wa uchumi kuhakikisha kwamba wanawasaidia kwenye ishus kama hizo.

Otherwise, ninakubaliana na hoja zako here!

William @Dodoma City!
 
pasco ningeulizwa na Mungu sasa hivi unataka nini ningemwambia, anionyeshe kwa cv za wanaochaguliwa kuwa wabunge wa hili bunge kutoka kwa wenzetu. pia anionyeshe commitment walizonazo katika kazi hii ndipo sasa ningerudi kuwadiscuss hawa wakwetu.

all in all tunahitaji watu ambao ni committed, na wenye exposure na well educated. pia watu wenye experience kwenye maswala ya kimataifa katika nyanja za uchumi, social, health na communication. lakini shy rose banji kwa kweli hafai kabisa hapa kwanza elimu yake haikumkomboa. manake kama hapa Jaffarai alimzingua hadi ikawa skendo akienda huko akina kidumu si ndo watampagawisha zaid??????????

- Mkuu again this is unfair, Shyrose ni binadam kama wengine wote tulivyo ni wapungufu, lakini masuala ya binafsi sidhani kama yana anything to do na perfomance ya mtu kiuongozi, kama anaweza kuiongoza bank kubwa kama NMB kufanya mambo mengi kwa wananchi kwa nini ashindwe kusimamia interest ya taifa kule EAC?

- Mambo ya Clinton na Monica hayakumzuia Clinton kuwa the best US president ever!

William @Dodoma City!
 
Back
Top Bottom