Hali katika kata ya Pasua usiku kucha kuanzia jana ilikua imechafuka baada ya wananchi kuchukizwa na maamuzi ya kikundi cha ulinzi shirikishi katika mtaa wa Bomambuzi kuwapiga mpaka kuwasababishia vifo watu wawili ndugu kuwatuhumu kuwa ni wez.
Chanzo ni wizi uliotokea katika duka la bidhaa na mwenye duka hilo kumhisi mfanyabiashara mwenzake kuwa amehusika nawizi huo na kuwakodisha kikundi hicho maarufu KUNGURU ambacho kinafadhiliwa na Meya wa manispaa ya moshi Mh. JAFFAR MICHAEL kumhoji mfanyabiashara huyo dukan kwake na kumkuta na vocha zikiwemo zilizoibiwa ndipo walipoanza kuwapiga mpaka kupoteza maisha na wananchi wakaanzisha vurugu kupinga mauaji hayo kwa kuwa waliouawa walikua sio wezi bali aliuziwa baadhi ya vocha.
Vurugu ilikua ni kubwa kwan nyumba katika mtaa wa bomambuzi zimechomwa moto na nyingine kupasuliwa vioo ikiwemo ya Meya. Polisi walishindwa kudhibiti machafuko hayo kutokana na maelfu ya watu wakiwa na silaha za jadi kuwashinda nguvu vurugu zimeendelea mpaka alfajiri.
Mpaka sasa ulinz ni mkali Polisi wamemwagwa kila mahali.Vijana wa KUNGURU wengi wameshatiwa mbaroni mpaka sasa kwa kweli uharibifu ni mkubwa kwan nyumba nyingi zimeharibiwa
Chanzo ni wizi uliotokea katika duka la bidhaa na mwenye duka hilo kumhisi mfanyabiashara mwenzake kuwa amehusika nawizi huo na kuwakodisha kikundi hicho maarufu KUNGURU ambacho kinafadhiliwa na Meya wa manispaa ya moshi Mh. JAFFAR MICHAEL kumhoji mfanyabiashara huyo dukan kwake na kumkuta na vocha zikiwemo zilizoibiwa ndipo walipoanza kuwapiga mpaka kupoteza maisha na wananchi wakaanzisha vurugu kupinga mauaji hayo kwa kuwa waliouawa walikua sio wezi bali aliuziwa baadhi ya vocha.
Vurugu ilikua ni kubwa kwan nyumba katika mtaa wa bomambuzi zimechomwa moto na nyingine kupasuliwa vioo ikiwemo ya Meya. Polisi walishindwa kudhibiti machafuko hayo kutokana na maelfu ya watu wakiwa na silaha za jadi kuwashinda nguvu vurugu zimeendelea mpaka alfajiri.
Mpaka sasa ulinz ni mkali Polisi wamemwagwa kila mahali.Vijana wa KUNGURU wengi wameshatiwa mbaroni mpaka sasa kwa kweli uharibifu ni mkubwa kwan nyumba nyingi zimeharibiwa