Nyumba ndogo........

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,563
Mara nyingi nimeshasikia watu wakishangaa kwa bwana fulani kutembea (sex) nje ya ndoa yake na mwanamke ambaye pengine havutii kihiiiivyo kama mkewe wa ndoa. Au mwanamke kutembea na kijibwana ambacho hakina A wala B compared na Mr wake.

Na mara nyingi wote ukiwauliza wanatoa sababu nzuri tu za kuwafanya wao wakubaliwe huo udhaifu wao. Utasikia mume akidai kuwa the woman -anajua mapenzi, ananifanya nijisikie mwanaume, has more time for me, ananiheshimu e.t.c.

Na mke akiulizwa vipi mbona unatembea na kibarua wenu atajibu either “Ananifanya nijisikie vizuri, ananifanya nijisikie wa maana, anajua pa kunigusa n.k

Na wakati mwingine tunaambiwa kuwa nyumba ndogo zina ufahamu wa hali ya juu kuhusu kile ambacho tunakikosa majumbani mwetu kwa wenzi wetu so tunakimbilia kwao ili tuvipate either kama ni feelings /hisia ambazo sisi kama wanandoa hukosa kwa wenzi wetu na kuamua kwenda kutafuta sehemu kwao.​

Sijui lakini hawa watu tunaotembea nao nje ya ndoa (nyumba ndogo, ving'asti e.t.c) wanaonekana wako smart sana kujua tunachokikosa ndani ya ndoa zetu.​

Swali langu ni je wanajuaje kuwa tunamiss hiki na kile katika ndoa zetu? Tunawaambia wenyewe au?​
 
Unatutega wewe

Msanii natega vipi? mie nashindwa kuelewa mpaka umrate nyumba ndogo aas better in fulfilling your love desire ina maana mkeo hujamwambia kuwa akikufanyia hivi vile unaridhika?

Iweje nyumba ndogo ajue your weak point na mkeo asijue? au wanatumia uchawi?
 
Mara nyingi nimeshasikia watu wakishangaa kwa bwana fulani kutembea (sex) nje ya ndoa yake na mwanamke ambaye pengine havutii kihiiiivyo kama mkewe wa ndoa. Au mwanamke kutembea na kijibwana ambacho hakina A wala B compared na Mr wake.

Na mara nyingi wote ukiwauliza wanatoa sababu nzuri tu za kuwafanya wao wakubaliwe huo udhaifu wao. Utasikia mume akidai kuwa the woman -anajua mapenzi, ananifanya nijisikie mwanaume, has more time for me, ananiheshimu e.t.c.

Na mke akiulizwa vipi mbona unatembea na kibarua wenu atajibu either “Ananifanya nijisikie vizuri, ananifanya nijisikie wa maana, anajua pa kunigusa n.k

Na wakati mwingine tunaambiwa kuwa nyumba ndogo zina ufahamu wa hali ya juu kuhusu kile ambacho tunakikosa majumbani mwetu kwa wenzi wetu so tunakimbilia kwao ili tuvipate either kama ni feelings /hisia ambazo sisi kama wanandoa hukosa kwa wenzi wetu na kuamua kwenda kutafuta sehemu kwao.​

Sijui lakini hawa watu tunaotembea nao nje ya ndoa (nyumba ndogo, ving'asti e.t.c) wanaonekana wako smart sana kujua tunachokikosa ndani ya ndoa zetu.​

Swali langu ni je wanajuaje kuwa tunamiss hiki na kile katika ndoa zetu? Tunawaambia wenyewe au?​

Nzuri sana
 
Mara nyingi nimeshasikia watu wakishangaa kwa bwana fulani kutembea (sex) nje ya ndoa yake na mwanamke ambaye pengine havutii kihiiiivyo kama mkewe wa ndoa. Au mwanamke kutembea na kijibwana ambacho hakina A wala B compared na Mr wake.

Na mara nyingi wote ukiwauliza wanatoa sababu nzuri tu za kuwafanya wao wakubaliwe huo udhaifu wao. Utasikia mume akidai kuwa the woman -anajua mapenzi, ananifanya nijisikie mwanaume, has more time for me, ananiheshimu e.t.c.

Na mke akiulizwa vipi mbona unatembea na kibarua wenu atajibu either “Ananifanya nijisikie vizuri, ananifanya nijisikie wa maana, anajua pa kunigusa n.k

Na wakati mwingine tunaambiwa kuwa nyumba ndogo zina ufahamu wa hali ya juu kuhusu kile ambacho tunakikosa majumbani mwetu kwa wenzi wetu so tunakimbilia kwao ili tuvipate either kama ni feelings /hisia ambazo sisi kama wanandoa hukosa kwa wenzi wetu na kuamua kwenda kutafuta sehemu kwao.​

Sijui lakini hawa watu tunaotembea nao nje ya ndoa (nyumba ndogo, ving'asti e.t.c) wanaonekana wako smart sana kujua tunachokikosa ndani ya ndoa zetu.​

Swali langu ni je wanajuaje kuwa tunamiss hiki na kile katika ndoa zetu? Tunawaambia wenyewe au?​

huwa hatuwaambii ila wenyewe ni wataalamu tu wakujua kuwa tunakosa nini uko tunakotoka kwahiyo wana-consolidate hapo hapo hadi tunajikuta tunamwaga mchele penye kuku wengi. Wenye nyumba ndogo wanaweza kutusaidia zaidi hapa
 
tatizo wanawake wengi au wanaume wakishaoa/ kuolewa wanajisahau yale mambo mazuri waliyokuwa wanafanya those days wanayaacha wanajisahau. ndo mana unakuta mtu wa nje anapojua una ndoa halafu umetoka anajua lazima kuna kitu unakikosa, kwa hiyo anatumia utaalamu wake wote na heshima ya hali ya juu ili akuteke ndo mana unakuta watu wengine wanakimbia ndoa zao kwa sababu huko nje wamenogeshwa.
 
Msanii natega vipi? mie nashindwa kuelewa mpaka umrate nyumba ndogo aas better in fulfilling your love desire ina maana mkeo hujamwambia kuwa akikufanyia hivi vile unaridhika?

Iweje nyumba ndogo ajue your weak point na mkeo asijue? au wanatumia uchawi?
kama umeshamwambia mke na hajaonesha dalili za kubadilika au kukuelewa unadhani nini hutokea? ni kumtafuta msaidizi wake ili uendelee kumpenda mkeo au la utamchukia moja kwa moja.
Raha ya nyumba ndogo ni kwamba inajituma ipasavyo maana inakula kwa jasho lake. Halafu kwenye nyumba ndogo hata ukitaka kujiexpress yourself unapita bila kupingwa
 
Wakati mwingine hakuna kipya unachokipata huko ila ni ile kubadilisha mboga,si unajua hata maharage uwa matamu kwa sharti ufululize nyama na samaki.
Wengi wetu tunapokuwa ndani ya ndoa ujisahau sana hivyo tukawa si wabunifu,unachoka maana hakuna kipya.Sasa unapoonjeshwa kisamvu tena hata nazi hakina,unabaki ukijiramba midomo.Na kwa kuwa hauendi kwa nyumba ndogo mara kwa mara,siku zote unakuwa na hamu nae.
Kitu kingine,ni heshima isiyokuwa na maana tunayojifanya kuwa nayo ndani ya ndoa,wakati kwa nyumba ndogo kule unakuwa free,unajiachia unavyotaka.Sasa wewe kila siku kifo cha mende,usichoke.Wewe unategemea siku ukipigiwa mbuzi kagoma kwenda,utabaki hapo.

Mbaya zaidi wanawake katika sita kwa sita uwa kama bendera,sasa ukikuta na mwanaume mwenyewe ndo kama mie,anajua kuvamia tuu kwa staili ile ya kifo cha mende tuu,lazima utaibiwa tuu.

Ishuuu inakuja siku umepita katika jukwaa la kikubwa,una mastaili kibao.
Mama naniii leo geukia huko,au kaaa hivi,wewee majibu yako

"Hayo kawafanyiege hao hao hawala zako sio mimi"
Kwa nini usigande kwa nyumba ndogo
 
kama umeshamwambia mke na hajaonesha dalili za kubadilika au kukuelewa unadhani nini hutokea? ni kumtafuta msaidizi wake ili uendelee kumpenda mkeo au la utamchukia moja kwa moja.
Raha ya nyumba ndogo ni kwamba inajituma ipasavyo maana inakula kwa jasho lake. Halafu kwenye nyumba ndogo hata ukitaka kujiexpress yourself unapita bila kupingwa

jamani hii si slogan ya tigo hiyo niliyoihighlight hapo juu.!!!? mizee ya NSSF utaijua tu bila kuchafua kiv*zi haisikii raha.
 
kama Joy alivyosema, wengi wetu 2kishaingia ndani tunajisahau sana, kuna ndoa ya ma colleague ilifungwa last yr oct but anasema ndoa imeshakuwa ndoano mana mke hana time tena na chochote kinachohusu ndoa, akiguswa hivi nimechoka, akiambiwa mami leo nina hamu ya matembele oohh ctaweza kupika leo twende kukachukue take away, anajuta kuoa na mpaka kashampata king'asti na anasema anajuta kwanini alifunga ndoa haraka mana king'asti ndio aliefaa kuwa mke! na hapo hapo kwa upande mwingine kuna wanaume hata uwape kitu gani/ufanye nini bado watatoka tu(kunguru hafugiki).
 
Mara nyingi nimeshasikia watu wakishangaa kwa bwana fulani kutembea (sex) nje ya ndoa yake na mwanamke ambaye pengine havutii kihiiiivyo kama mkewe wa ndoa. Au mwanamke kutembea na kijibwana ambacho hakina A wala B compared na Mr wake.

Na mara nyingi wote ukiwauliza wanatoa sababu nzuri tu za kuwafanya wao wakubaliwe huo udhaifu wao...

...dah, Mwj'1 hapo ulipoandika "wanatoa sababu nzuri tu" ndipo uliponimaliza, kwani bado sijawahi sikia sababu yeyote nzuri ya kutembea nje ya ndoa.
 
Kusema ukweli nyumba ndogo haina lolote na wala haina hicho kinachoitwa ubunifu. Huwa ni frustrations tu zinazotokana na kuzoeleka kwa ndoa kiasi cha mtu kuanza kumchukulia mwenzie kama 'as usual'.

Huo ubunifu unaozungumziwa kwenye nyumba ndogo hauna zaidi ya kile waswahili wanita kipya kinyemi. Mifano mingi ya watu walio hamia nyumba ndogo (yaani kuioa kabisa) zimeishia na kushindwa kubaya, watu wakitamani kurudi kule walikotokea (kuwarudia wenzi wao wa zamani).

Performance ya nyumba ndogo iko kwenye ubongo wa yule anayeitafuta. Kushindwa kuhimili mikiki mikiki ya ndoa ndio chanzo kikubwa cha watu kutafuta relief katika nyumba ndogo. Kwa hiyo hata ikiwa nyumba ndogo ni chovu kuliko nyumba kubwa, basi anayeitafuta hufurahia cho chote kile na huo uchovu atauona ni bidhaa adimu. Atagundua tu kuwa huo ni uchovu tu pale nyumba kubwa inapoota mbawa.

Kwa hiyo ni ka-ugonjwa tu au tunaweza sema ni hickups katika ndoa. Ukweli with time, nyumba ndogo ni chanzo cha frustrations nyingi kwa watu wanaozifuata kwa kusikiliza stori kama hizi na kuamini kuwa nyumba ndogo zitamaliza matatizo yao.

Ndoa ikikushinda,........ Jaribu kutafuta amani ndani ya nafsi yako mwenyewe. Ikiwa mwanandoa mwenzio unahisi hakupendi au hakuheshimu kihivyo, we jiheshimu mwenyewe na jipende mwenyewe. Utamaliza matatizo. Kukimbilia upendo wa nyumba ndogo ni kujaribu kuzima moto wa petroli kwa kuupuliza.
 
teh teh teh
karibu one the world mkuu
ahahahahahahahahahaha, nimepakumbuka sana mwananyamala. kule NSSF kila mtaa mpaka mvua hazinyeshi kule. watoto wanajua kuchafua kidesh-desh ile mbaya.
nimekupata mkuu, ila inabidi tuache sasa maana humu JF kuna wachungaji na maustaadh wengi kwelikweli. wakati mwingine huwa nahisi kama niko jangwani kwenye maombezi
 
hahahaha
endelea kuombewa mpaka uache kisha utuachie uwanja mpana zaidi kwani tukiwa wawindaji wengu tunapoteza mawindo kinoma
 
Kusema la ukweli sisi wanawake huwa tunachangia waume zetu kwenda nyumba ndogo. Tukisha olewa na kuweka ndani ndio tunaona tumefika. Tunasahau wakati tukiwa wachumba tuliokuwa tunayafanya hata mkitoka kazini wote ile jioni mzee akiitaji kula matembele mbio unakwenda kuandaa, tena wafanya kumbembeleza " Honey leo njoo ule kwangu bwana.... akimaliza ugali na tembele unaachia viwili vya nguvu akha mtu anaende kwake kulala akiwa mweepeeesiii.
leo uko ndani akitaka unadai umechoka kwani mwanzoni ulikuwa huchoki ana hukujua unahitaji kuwahi kwenda kazini asubui. Wakati style zote ulikuwa unampatia uwe umechoka au hujachoka ulikuwa radhi kumtimizia ilimradi tu asiende nje kwa mrembo mwingine. Leo ati umechoka kilicho kuchosha ni nini?
Wanawake tubadilike. Tuliwazoeshe wenyewe hawa waumezetu kipindi cha kuchumbiana.!

Sio nawasema wanawake tu nanyi wanaume pia ukisha amua kuowa basi wale uliokuwa nao nyuma waache, eti mmnakamsemo kenu " PENZI LA HAWARA HALIFI" ukiwa unapewa huduma zote hadi kubebwa mgongoni kinachokupeleka nje kipi? Tulieni na wake zenu.
Kumbuka yale uliokuwa unamfanyia mkeo kipindi cha uchumba utakapo acha kumfanyia basi nae kwasababu anakosa ile huduma ya mwanzo ndipo anapokwenda kwa mlizi,shamba boy, dereva hata house boy pia. Utakuta mwanaume akisharudi mkewe yuko moto jamaa anagusa tu alafu anakoroma unategeme nini kama mkeo haendi kupindwana wafanyakazi wako.
 
mmesahau kuwa sisi ni waafrika halisi?
ukichunguza sana utakuja kugundua babu za wazazi wetu walidumisha mila ktk ndoa. seuse sisi
 
Simpo. Dawa ni kupeana sana, mno, kabisa, every time, mpaka hamu za kwenda huko nje zinakuwa hazipo. Kama huwezi hivyo, utajiju...Huwezi kwenda nje kama huna hamu.
 
Msanii natega vipi? mie nashindwa kuelewa mpaka umrate nyumba ndogo aas better in fulfilling your love desire ina maana mkeo hujamwambia kuwa akikufanyia hivi vile unaridhika?

Iweje nyumba ndogo ajue your weak point na mkeo asijue? au wanatumia uchawi?

MJ1, haya ni maoni yangu, labda huko nyumba ndogo wanawake wa huko wanauliza maswali mbali mbali ili kujua wanaume wanapenda nini latika tendo la ndoa, nini wanapenda kufanyiwa ili wasuuzike roho zao na kipi wanachopenda kuwafanyia wapenzi wao ambacho na wao pia wanaenjoy kukifanya.

Tukirudi nyumbani labda mazungumzo kama hayo hayapo kabisa. Halafu ujue nyumba ndogo wanajua tayari wana competition wakizembea tu katika 'kazi zao' basi kibarua kitaota majani, hivyo ni lazima wajitahidi kadri ya uwezo wao ili kuhakikisha njembas zinachanganyikiwa na kurudi at least kila siku :) au baada ya siku chache.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom