Nyerere: Salaam zenu mnaomkejeli!

Huwezi kusifia utawala wa Nyerere wakati vitu vidogo vidogo vya matumizi ya binadamu vilikuwa hakuna..
Wakati wa Nyerere watu tulikosa sabauni za kuongea na kufuria, dawa za meno, vyakula vibovu binadamu wanapewa..
Maduka ya ushirika unapangiwa vitu vya kununua unapewa maharage mabovu pamoja na magadi kwa ajili ya kuivisha wakati unayapika..
Unalazimishwa ununue vitu ambavyo utaki, lazima ununue panga, tube za baiskeli, sigara aina mbili Zakuchuja na Zaraha, mkuki, jembe, spoku za baiskeli za Swala..
Watu wanakwenda shule bila viatu, ukitaka radio mpaka ukanunue RTC..
Ukikutwa na dola 50 utajuta ukiweka akiba ndani ya chakula unaitwa muhujumu uchumi...ukitaka kupiga simu mpaka uende posta upange foleni..
Tumekula chakula cha farasi wa Texas, mahindi ya njano..
Watu walikuwa wanatembea nguo zimetoboka kwenye makalio, viraka kila sehemu..
Ngoja kwanza niishie apa kwanza...
Na mfano kama huu ndio wengi mnakosea sana sana. Yaani una pick up siku moja au mwaka mmoja na unaacha miaka 20.

Wakati wewe unasema hayo mwingine aliyeishi nyakati za mwalimu haswa na si kusimuliwa atasema hivi
1. Alikuwa tunakwenda shule bila ada na huko tunapewa vitabu na madaftari

2. Alikuwa tunasafiri kwenda shule kwa warrant na kama haukuchukuliwa akifika shule anadai nauli yake na inarudishwa.

3. Atakwambia mfanyakazi alikuwa anapewa warrant ya usafiri wa yeye na familia yake popote nchini kwa gharama yoyote

4 Atakwambia ukiumwa unaenda hospitali mambo yote unawaachia wao kuanzia vipimo hadi dawa
5. Atakwambia kama mlikuwa mahindi ya Texas, siku hizi mnakula kuku zilziooza kutoka South Africa na si kila mmoja ana afford

6 Zamani ulikuwa ukimaliza shule unapata ajira, ahh hayo ni mambo ya Nyerere na ujamaa. Siku hizi mambo safi unamaliza shule unatafuta bahasha za khaki 100 unaweka CV unaanza kuzunguka mtaani hadi soli iishe. Si tuna viatu bwana na si kama zamani!!

7. Atakwambia kutembea na dola 50 ilikuwa kosa lakini hiyo sh 10 ilikuwa inanua unga, sabuni, sukari na kitoweo.
Je sasa hivi kuna wangapi wana dola 1 mfukoni. Kama mtu hawezi kununua dozi ya peniciline ya sh 1200 yaani senti 90 dollar inamsaidia nini kumruhusu atembee na dola 2000. Huoni hapa ni akina fisadi wanaopaswa kushangilia na si Kibambara, Ng'onda au Zainabu.

8. Ukitaka radio lazima uende RTC, sasa siku hizi unapata kutoka china kesho unatupa. Tulikuwa na Matshusita iliyokuwa inatoa ajira na bidhaa bora sana , siku hizi ni faster faster unanunua sub standard haraka bila kwenda RTC. Hebu rejea post ya Mkandara hapo juu

Watu waangalie mambo in broad spectrum na si kutafuta kitu kimoja na kukifanya kama ndio mada. Mwaka 1974 kulikuwa na njaa kali sana iliyotokana na ukame. Sijui hapa mwalimu alaumiwe nini na ujamaa ulaumiwe vipi. Mbona nchi zote zinakumbwa na njaa kama tunavyoona Somalia na Kenya kwasasa. Mwaka 2006 watu wamekufa kwa kula ming'oko kule Rufiji, hapo je!

Ukiangalia kazi ya mwalimu kwa sabuni, tv na internet utapata shida kweli kumwelewa. Ukiangalia kazi ya mwalimu in terms of vision, execution and long term sustainable projects unaweza kukosa cha kumsumanga hata kwa bahati mbya tu.
 
Ukiangalia kazi ya mwalimu kwa sabuni, tv na internet utapata shida kweli kumwelewa. Ukiangalia kazi ya mwalimu in terms of vision, execution and long term sustainable projects unaweza kukosa cha kumsumanga hata kwa bahati mbya tu.

Tunatakiwa kuangalia kazi ya kila kiongozi on both "Micro and Macro" economics level

Chukulia taifa kama nyumba yako, wewe kama mzazi mlezi watu wa nyumbani wakikosa mlo wa siku na basics zingine hapo hakuna upungufu katika management ya nyumba??
 
Waberoya,
Mkuu sii umeona viongozi wa vyama wanavyoendesha watu wengine vyamani? Unafikiri ni Unyerere au Ndivyo Tulivyo..Wabunge hadi Ma mayor hujiona wao ni wao waheshimiwa! jambo ambalo Nyerere alitukataza kuwa na waheshimiwa lakini wapi... Mtu akikabidhiwa tu Unyapala basi yeye ndio Mungu mtu ilikuwepo toka utumwa na hadi magerezani kwa wafungwa, nyapala hujiona mkubwa kama Mungu.. Ni hulka ya mtu mweusi..

wengi hawalioni hiki kilema chetu....wengi hawataki kuukubali huu ukweli..tunawaambia Nyerere alikuwa na tabia hizi zauchifu watabisha mpaka mapovu yatatoka..tunasema Nyerere alikuwa hivyo bila ku-exclude tabia za waafrika wengine wengi tu kama si wote

u-chief wa viongozi wa ccm ni wa baba yao Nyerereni wa kiafrika pure-uafrika, ndio uchifu tunaouona NCCR sasa, CUF sasa na CDM ambao waliishalionyesha hilo mapema!

kama ulivyosema hakuna jipya tulilofundishwa na kuachiwa na mzee huyu, kinachonitatiza je Mkandara umetumia degree ipi na uwezo upi kujua tabia zetu mbaya na chafu za asili? leo ukipewa uongozi najua utafanya kinachotakiwa kufanya kwa sababu unajua hulka na tabia zetu! kiongozi anayejiita wa taifa , msomi na mwenye akili ya caliber ya Nyerere alitakiwa kujua hili far, far higher than you do! where should I place him?
 
Ukiangalia kazi ya mwalimu kwa sabuni, tv na internet utapata shida kweli kumwelewa. Ukiangalia kazi ya mwalimu in terms of vision, execution and long term sustainable projects unaweza kukosa cha kumsumanga hata kwa bahati mbya tu.

Uko sahihi kabisa, tunatofautiana ufahamu na hakuna aliyewahi kudadavua hili kwa undani, lengo lake lilikuwa ni nini?, inaonekana kwa wengi ilikuwa ni hadithi au ndoto fulani....bahati mbaya visions za mwalimu zilikuwa zake, alitumia ubabe mwingi kwa kudhani ana akili nyingi na yuko sahihi...same habit ambayo inaonyeshwa na pro-Nyerere wengi humu..ubabe na kuona wengine mazezeta au mambumbumbu! eti kisani visionary kuliko wengine wote..this is very wrong approach, poor leadership! ndio maana kule CCM leo ukiacha hawa wanaojiita watetezi wa mwalimu kwenye mitandao hakuna anaye-exercise tabia na siasa za mwalimu..they have long gone with him...ila eti anabaki visionary! guys strength are measured in the things we stand for, and weakness manifested in the things we have failed! Kinachobaki ni kuwa goli limefungwa tumeshindwa tunabaki kusema unajua tulipiga sana chenga, tukawapiga kanzu na kosa kosa nyingi...halafu formation yetu tuliyoicheza ya 4-4-2 was the best! yet we have failed

Mbaya zaidi waliofuata hawakutaka kujua tumefeli wapi , wakaanza maisha mapya kabisa, tunabaki Arusha declaration , ujamaa na kujitegemea...my foot! AD mababu zetu wali-support kwa nguvu zote! walitembea miles kwa ajili ya hiyo..leo wote hao wamesahau maumivu na uchungu wa maandamano yale! it seems they supoorted something they never believed! inauma!

kuna watu wako tayari kutukana yeyote wakimtetea Marehemu Nyerere.....kisa alikuwa na akili na hakuna moja leo tunaloringia la mwalimu!!!.......Mwalimu alisema EL hafai...Kikwete ambaye likuwa mtoto wa Nyerere akampa uwaziri mkuu!!!! what happened guys??


mimi mwalimu mwanafunzi akifeli sio tu anaangaliwa mwanafunzi bali na mwalimu wake!!
 
Hulka ya mtu mweusi ndio nini bana acha kutuchanganya wewe?? nyerere mweusi au mweupu? unasifia mweusi moja unadharau weusi wote ukiwemo wewe?? ipi ni ipi? Tabia haina rangi mkuu
Aaaah hata mimi nimo mkuu wangu napenda Unyapala wala siwezi kukataa lakini tofauti tu ni kwamba najua ni makosa na najitahidi kutokuwa Nyapala kujiona Mungu mtu...Nimekatazwa na vitabu lakini inferiority complex mkuu ni challenge kubwa sana kwa mtu mweusi utumwa umetufundisha mengi matamanio.. Waswahili wanasema - Maskini akipata makalio hulia Mbwataaa ... yaani kapumzika na kasahau alikotoka, Ndivyo Tulivyo...Ila sii vibaya kupeana tahadhali..
 
Uko sahihi kabisa, tunatofautiana ufahamu na hakuna aliyewahi kudadavua hili kwa undani, lengo lake lilikuwa ni nini?, inaonekana kwa wengi ilikuwa ni hadithi au ndoto fulani....bahati mbaya visions za mwalimu zilikuwa zake, alitumia ubabe mwingi kwa kudhani ana akili nyingi na yuko sahihi...same habit ambayo inaonyeshwa na pro-Nyerere wengi humu..ubabe na kuona wengine mazezeta au mambumbumbu! eti kisani visionary kuliko wengine wote..this is very wrong approach, poor leadership! ndio maana kule CCM leo ukiacha hawa wanaojiita watetezi wa mwalimu kwenye mitandao hakuna anaye-exercise tabia na siasa za mwalimu..they have long gone with him...ila eti anabaki visionary! guys strength are measured in the things we stand for, and weakness manifested in the things we have failed! Kinachobaki ni kuwa goli limefungwa tumeshindwa tunabaki kusema unajua tulipiga sana chenga, tukawapiga kanzu na kosa kosa nyingi...halafu formation yetu tuliyoicheza ya 4-4-2 was the best! yet we have failed

Mbaya zaidi waliofuata hawakutaka kujua tumefeli wapi , wakaanza maisha mapya kabisa, tunabaki Arusha declaration , ujamaa na kujitegemea...my foot! AD mababu zetu wali-support kwa nguvu zote! walitembea miles kwa ajili ya hiyo..leo wote hao wamesahau maumivu na uchungu wa maandamano yale! it seems they supoorted something they never believed! inauma!

kuna watu wako tayari kutukana yeyote wakimtetea Marehemu Nyerere.....kisa alikuwa na akili na hakuna moja leo tunaloringia la mwalimu!!!.......Mwalimu alisema EL hafai...Kikwete ambaye likuwa mtoto wa Nyerere akampa uwaziri mkuu!!!! what happened guys??


mimi mwalimu mwanafunzi akifeli sio tu anaangaliwa mwanafunzi bali na mwalimu wake!!
Mkuu wangu Hivi kweli ukicheza mpira na 4-4-2 ukashindwa ina maana mfumo huo haufai hata kama unajua fika kwamba refa hakuwa upande wenu, jamaa walicheza rafu mwanzo hadi mwisho.. Haya tumepata penalty dakika za mwisho mshambuliaji wetu akapiga juu kama walivyofungwa Ghana na Uruguay bado kosa ni la Kocha...halafu leo Suarez ndio kapewa sifa za kudaka mpira golini na kuwa mchezaji mzuri wa ku sign contract kubwa kubwa kumbe racist..Ama kweli kazi tunayo.
 
Waberoya;3022613]alitumia ubabe mwingi kwa kudhani ana akili nyingi na yuko sahihi...same habit ambayo inaonyeshwa na pro-Nyerere wengi humu..ubabe na kuona wengine mazezeta au mambumbumbu! eti kisani visionary kuliko wengine wote..this is very wrong approach, poor leadership!
Sio kwamba alijifanya ana akili, ni kweli alaikuwa na akili na uwezo wake unapimwa katika mizani ya kimataifa bila ya yeye kuwepo. Hata wapinzani wake wanakiri ana akili.
Kuhusu vision, nimeweke swali hapa halijibiwi na nashangaa! Waberoya, hebu niambie ni jambo gani lilifanyika miaka 25 iliyopita na miaka 10 baada ya kifo chake, na mipango gani ipo mbioni katika mipango ya miaka 25 ijayo ambayo haina maono(vision) ya mwalimu au haikuwahi kufanyiwa kazi na Nyerere.
Ndio maana kule CCM leo ukiacha hawa wanaojiita watetezi wa mwalimu kwenye mitandao hakuna anaye-exercise tabia na siasa za mwalimu..they have long gone with him...
Ni kweli mwalimu aliondoka na yake na hakuna anayefuata ndiyo maana kuna akian RA,EL, Jairo n.k. Wanaitafuna nchi.
Jiulize CCM ya Nyerere ndio hii ya leo ambayo hata kumwita mtu mwizi inahitaji vikao nenda rudi.

Halafu formation yetu tuliyoicheza ya 4-4-2 was the best! yet we have failed
Formation haina matatizo, tatizo ni kuwa wachezaji walilala makaburini wakigangwa na viongozi wanatafuta mchawi makaburini hata yule aliyefariki wanadhani ndiye sababu, mashabiki hawajui kwanini tumefungwa wanadhani mganga mzuri ni yule wa Tanga kwasababu anavaa kanzu, yule wa kisukuma alikuwa na madogori mengi ndio maana tumefungwa.


kuna watu wako tayari kutukana yeyote wakimtetea Marehemu Nyerere.....kisa alikuwa na akili na hakuna moja leo tunaloringia la mwalimu!!!.......Mwalimu alisema EL hafai...Kikwete ambaye likuwa mtoto wa Nyerere akampa uwaziri mkuu!!!! what happened guys??
Na kuna watu wapo tayari kusema uongo na uzushi kuhusu Nyerere hata kama hakufanya. Wapo wanaodhani angekuwa pagani nchi hii ingekuwa mbali sana.

Kumkataa EL, na kwa taarifa yako Kikwete pia ni moja kati ya vision za Nyerere! Kila mwenye akili timamu na asiyeongozwa na chuki za kuzaliwa au kufundishwa anakiri hili jambo. Wengi hawakuona hatari inayotukabili sasa wanagundua yule mzee aliona mbali.
 
Back
Top Bottom