Hodi humu ndani! Salamu wote wana Jamii Forum. Nianaomba msaada jamani.
MM nina Boyfriend wangu tumedumu kwa mwaka mmoja, tunapendana sana, na anaonyesha jitihada za kuwa na mm kama mke na mume, ameshanitambulisha kwa Mama yake, Dada zake na Kaka zake ila kwa kutumia simu kwan kwao ni mbali na tunapofanyia kazi kwahiyo umbali umechangia kuto onana face to face. Mara nyingi ndugu zake hao huwa wananipigia simu tunawasaliana na mm pia huwa nawapigia simu.
Mpaka hapo Mama yake anaonyesha upendo mkubwa sana wa mimi kuendelea kuwa na kijana wao. Ndugu wakinipigia simu wanakuwa wanani sihi sana kutulia na kumpenda kijana wao kwa moyo wote. Na mimi ki ukweli ninampenda sana kijana wao.
Week mbili zilizopita tulikutana kimwili na huyu Boyfriend wangu ambaye kwa sasa ni Mchumba mtarajiwa.. Baada ya siku kama tatu nikataka kumpima kama kweli anaupendo wa dhati kwangu au ni mambo ya ujana tu, nikamwambia nahisi kama nimepata ujauzito, kijana wa watu akaonyesha kufurahishwa sana na kauli ile akaniomba niende kupima ili niwe na uhakika kwan tupo wilaya tofauti hatuonani mara kwa mara, nikamwambia sawa nitaenda kupima, kesho yake nikampa majibu kuwa ni kweli nimepima na ninaujauzito. NILIKUWA NAMTANIA. Akaniambia sasa upendo wake kwangu umeongezeka mara dufu kwani anaamini nitakuwa mke wake.
Akampigia mama yake simu akamueleza juu ya jambo hilo na mama yake akamwambia basi hakuna shida atawaeleza baba zake wadogo ili wajiandae waje kwetu kutoa posa na taratibu nyingine za uchumba zifanyike ili tuoane mapema iwezekanavyo. Nikapigiwa simu na Mama yake akaniambia hongera mwanangu nimepewa taarifa zote na Mchumba wako kwa hiyo naomba usiogope sisi tunashughulikia swala la kuja huko kwenu.. Nilishtuka sana kwan Mchumba alikuwa ajaniambia kama amemwambia mama yake.
Na mimi nikamsikiliza mama yake mpaka mwisho. Swali langu je nimwambie mchumba kuwa nilikuwa namtania sina ujauzito? Na je atanichukuliaje? Na je wanaweza kusitisha zoezi la kwenda kujitambulisha nyumbani? Na mama yake atanionaje mimi? Nisaidieni mawazo ndugu yenu ntaumbuka mimi.
NB. Nilimtania ili kujua atachukua hatua gani baada yakujua mm ni mjamzito.
Ushauri wenu ndio silaha ya kuokoa ndoa hii itarajiwayo. Na Mungu atawabariki.
MM nina Boyfriend wangu tumedumu kwa mwaka mmoja, tunapendana sana, na anaonyesha jitihada za kuwa na mm kama mke na mume, ameshanitambulisha kwa Mama yake, Dada zake na Kaka zake ila kwa kutumia simu kwan kwao ni mbali na tunapofanyia kazi kwahiyo umbali umechangia kuto onana face to face. Mara nyingi ndugu zake hao huwa wananipigia simu tunawasaliana na mm pia huwa nawapigia simu.
Mpaka hapo Mama yake anaonyesha upendo mkubwa sana wa mimi kuendelea kuwa na kijana wao. Ndugu wakinipigia simu wanakuwa wanani sihi sana kutulia na kumpenda kijana wao kwa moyo wote. Na mimi ki ukweli ninampenda sana kijana wao.
Week mbili zilizopita tulikutana kimwili na huyu Boyfriend wangu ambaye kwa sasa ni Mchumba mtarajiwa.. Baada ya siku kama tatu nikataka kumpima kama kweli anaupendo wa dhati kwangu au ni mambo ya ujana tu, nikamwambia nahisi kama nimepata ujauzito, kijana wa watu akaonyesha kufurahishwa sana na kauli ile akaniomba niende kupima ili niwe na uhakika kwan tupo wilaya tofauti hatuonani mara kwa mara, nikamwambia sawa nitaenda kupima, kesho yake nikampa majibu kuwa ni kweli nimepima na ninaujauzito. NILIKUWA NAMTANIA. Akaniambia sasa upendo wake kwangu umeongezeka mara dufu kwani anaamini nitakuwa mke wake.
Akampigia mama yake simu akamueleza juu ya jambo hilo na mama yake akamwambia basi hakuna shida atawaeleza baba zake wadogo ili wajiandae waje kwetu kutoa posa na taratibu nyingine za uchumba zifanyike ili tuoane mapema iwezekanavyo. Nikapigiwa simu na Mama yake akaniambia hongera mwanangu nimepewa taarifa zote na Mchumba wako kwa hiyo naomba usiogope sisi tunashughulikia swala la kuja huko kwenu.. Nilishtuka sana kwan Mchumba alikuwa ajaniambia kama amemwambia mama yake.
Na mimi nikamsikiliza mama yake mpaka mwisho. Swali langu je nimwambie mchumba kuwa nilikuwa namtania sina ujauzito? Na je atanichukuliaje? Na je wanaweza kusitisha zoezi la kwenda kujitambulisha nyumbani? Na mama yake atanionaje mimi? Nisaidieni mawazo ndugu yenu ntaumbuka mimi.
NB. Nilimtania ili kujua atachukua hatua gani baada yakujua mm ni mjamzito.
Ushauri wenu ndio silaha ya kuokoa ndoa hii itarajiwayo. Na Mungu atawabariki.