Research Solutions TZ
Member
- Jul 11, 2020
- 64
- 139
Kila kitu kilikuwa kama maigizo kabla ya kuona rasmi napokea muamala kama mnavyoona hapo juu. Sina la kusema zaidi ya kuwashukuru JamiiForums kwa kunipatia hela hii ambayo sitahitaji ushauri wa jinsi ya kuitumia.
Nimefungua akaunti hii muda mrefu sana, nikawa napata vijisent vya hapa na pale kwa kuandika tafiti nikiwa na wenzangu ambao kwa sasa kila mtu ameajiriwa kimpango wake.
Nashukuru kwamba sijaacha suala la kuandika na kupitia Stories of Change nimepata hiki kiinua mgongo ambacho kinatosha kuanzisha walau kampuni tuliyowaza kuianzisha.
Naomba ieleweke kuwa bado naendelea kushauri wanafunzi wa post graduate kuhusu tafiti, aidha kama taasisi inahitaji kupata tafiti na pia nasaidia kufanya statistical analysis kwa software yoyote unayoihitaji. Ukitaka training ya matumizi ya software tafadhali nicheki Instagram au kwa namba yangu ya simu ambayo ipo kwenye posts zilizotangulia humu.
NB: Hela zina matumizi usije kukopa
Nitumie nafasi hii kuwashukuru sana JamiiForums. Kongole kwenu