HOMOSAPIEN
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 745
- 271
Umeyakuza mwenyewe hilo bifu halitaisha labda ubadili kazi au ofisi,pole kwa masaibu yaliyokukuta ila ni kazi ndogo sana kubali yaishe mridhishe,ila usikubali kujenga kibanda ukifanya hivyo umekwisha!ukimridhisha atanyamaza na kutunza siri ila ukimkorofisha anaweza kukuzushia ulitaka kumbaka,yote ni maisha na haya siyo mageni katika haya maofisi tena bora huyo ni mhudumu angekuwa bosi wako hata kazi ungesimamishwa,mwanamke akidhamiria jambo lazima alitimize,asipolitimiza yupo tayari kufanya chochote ilimradi atimize ndoto yake,masaibu kama haya yanawasibu wengi katika haya maofisi yetu ila yanakamilika kwa siri na hali inabakia shwari,sasa ni juu yako kusuka au kunyoa ila ukumbuke ulilolifanya siyo jema kwa mwanamke anayekufuata kwa jinsi hiyo huyo yuko tayari kwa lolote liwe la mvua au la jua, yaani liwalo na liwe kazi kwako