Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Sijui naanzia wapi ila yalonikuta sitokaa kusahau maishani mwangu.
Mke kanitenda. Jamani kanitenda! Lol. Mimi ni mdau katika sekta ya utalii. Nimejibana saana mpaka nikamfungulia mke wang maduka mawili. Moja la nguo na lingine mini superket. Nikampa na gari ndogo ya kutembelea. Siku moja hivi majuzi mtoto akanambia kuna baba mmoja anaendeshaga gari ya mama pindi ninaposafiri. Nikaanza kufanya uchunguzi. Nikaja kugundua huyu jamaa alikuwa mchumbake kabla sijamuoa. Ikabidi siku moja niage naenda nje ya mji. Nilipoondoka tu jamaa naye akaja wakachkua gari yangu huyo wakaondoka! Mbaya sana alikuwa na mtoto wangu wa miaka sita. Akaenda na jamaa mpaka home. Jamaa akamsubiri wife wangu akabadilishe nguo akamwambia mtoto kuwa asjekuniambia kuwa alikuja na uncle...... Mtoto akajakunambia. Hakika iliniuma sana ukizingatia ni mtu ambaye nimejitahidi sana kuwasaidia yeye na familia yake (yaani wakwe zangu). Niliteseka sana rohoni. Juzi usiku kama saa nane hivi ilibidi nimuulize. Alichonambia kuwa huyo uncle ni kama kaka yake na wamekuwa pamoja mtaa mmoja. Nilipomuuliza iweje gari n iliyonunua mimi ampe mtu aendeshe bila idhini yangu? Akajibu aliwhi kumpa gari mara moja tu. Kuhusu kwenda nyumbani akajibu alimkuta njiani na mama yake akampa lifti. lakini yeye haishi mtaa ninaoishi. Nilipowauliza wafanyakazi wa pale dukani wakanambia aliondoka naye toka hapo dukani. Je kama ilikuwa kwa nia njema kwa nini aseme hakutoka naye? Kwa nini amwambie mtoto asinambie?
The next day alienda kazini kama kawida lakini aliaga kuwa anawahi nyumbani kufanya usafi. Lakini niligundua hali isiyo ya kawaida. Nilipomuuliza maelezo kamili kuhusu tuhuma zake alitoka chumbani na kukimbilia sebuleni. Nilipoamaka jana aliingia chumbani na kuchukua mkoba wake akauficha. Ilibidi tuanze kikao asubuhi baada ya watoto kuondoka. Niliyoyakuata ni mengi. Mi najua kuwa ana bank account 1 tu lakini ana akaunt nyingine 2 bank tofauti na zote zina hela. Slip zinaonyesha kuwa huwa anaweka pesa wakati mimi sipo. Wacha hirizi nilizozikuta ambazo zina jina langu na la mama yangu. Ana simcard zaidi ya 5 na zote zina fedha. Alilia sana, akaomboleza sana, akamwomba mtoto yule mdogo amwoombee radhi mtoto akamkataa.
Alipoona mambo yamezidi aliondoka kimya kimya tangu jana na sijui yuko wapi.
Mkiwa kama familia mnanishauri vipi?
Mke kanitenda. Jamani kanitenda! Lol. Mimi ni mdau katika sekta ya utalii. Nimejibana saana mpaka nikamfungulia mke wang maduka mawili. Moja la nguo na lingine mini superket. Nikampa na gari ndogo ya kutembelea. Siku moja hivi majuzi mtoto akanambia kuna baba mmoja anaendeshaga gari ya mama pindi ninaposafiri. Nikaanza kufanya uchunguzi. Nikaja kugundua huyu jamaa alikuwa mchumbake kabla sijamuoa. Ikabidi siku moja niage naenda nje ya mji. Nilipoondoka tu jamaa naye akaja wakachkua gari yangu huyo wakaondoka! Mbaya sana alikuwa na mtoto wangu wa miaka sita. Akaenda na jamaa mpaka home. Jamaa akamsubiri wife wangu akabadilishe nguo akamwambia mtoto kuwa asjekuniambia kuwa alikuja na uncle...... Mtoto akajakunambia. Hakika iliniuma sana ukizingatia ni mtu ambaye nimejitahidi sana kuwasaidia yeye na familia yake (yaani wakwe zangu). Niliteseka sana rohoni. Juzi usiku kama saa nane hivi ilibidi nimuulize. Alichonambia kuwa huyo uncle ni kama kaka yake na wamekuwa pamoja mtaa mmoja. Nilipomuuliza iweje gari n iliyonunua mimi ampe mtu aendeshe bila idhini yangu? Akajibu aliwhi kumpa gari mara moja tu. Kuhusu kwenda nyumbani akajibu alimkuta njiani na mama yake akampa lifti. lakini yeye haishi mtaa ninaoishi. Nilipowauliza wafanyakazi wa pale dukani wakanambia aliondoka naye toka hapo dukani. Je kama ilikuwa kwa nia njema kwa nini aseme hakutoka naye? Kwa nini amwambie mtoto asinambie?
The next day alienda kazini kama kawida lakini aliaga kuwa anawahi nyumbani kufanya usafi. Lakini niligundua hali isiyo ya kawaida. Nilipomuuliza maelezo kamili kuhusu tuhuma zake alitoka chumbani na kukimbilia sebuleni. Nilipoamaka jana aliingia chumbani na kuchukua mkoba wake akauficha. Ilibidi tuanze kikao asubuhi baada ya watoto kuondoka. Niliyoyakuata ni mengi. Mi najua kuwa ana bank account 1 tu lakini ana akaunt nyingine 2 bank tofauti na zote zina hela. Slip zinaonyesha kuwa huwa anaweka pesa wakati mimi sipo. Wacha hirizi nilizozikuta ambazo zina jina langu na la mama yangu. Ana simcard zaidi ya 5 na zote zina fedha. Alilia sana, akaomboleza sana, akamwomba mtoto yule mdogo amwoombee radhi mtoto akamkataa.
Alipoona mambo yamezidi aliondoka kimya kimya tangu jana na sijui yuko wapi.
Mkiwa kama familia mnanishauri vipi?