MSAADA: Utukutu wa mtoto wa ndugu yangu unanishinda, anafanya matukio kila kukicha, nifanyaje?

plus_ix

JF-Expert Member
Jul 10, 2022
561
1,390
Habarini wana JF. Moja kwa moja kwenye mada kama kichwa hapo juu kinavyojieeleza.

Huyu ni mtoto wa jamaa angu nimeona niandike kwaajili yake, labda tutapata msaada humu ndani maana binafsi nimeshindwa.

Nina mtoto kwa sasa ana umri wa miaka kumi na nne (14) yupo kidato cha kwanza lakini kwa mwenendo wake naona hata kidato cha pili hatoboi, dogo ana matukio ya ajabu sana na tumejitahidi kwa kila njia lakini imeshindikana ntaweka matukio yake kiufupi.

Mwanzo kabisa wakati yupo darasa la tano alikimbia nyumbani hapa, alitoka Pugu mpaka kinyerezi kwa mguu kwa madai hakupendi. Tulijua ni kwa sababu ya utoto tulimtafuta kama siku mbili na kwa msaada wa polisi tulimpata tukapiga kidogo tukaacha.

Akakaa sawa akanza tutesa na tabia ya udokozi wa hela ndogondogo na anakopeleka ni kwenye play station tukamshika tena tukapiga kwa kuhofia ataanza kudokoa hela kubwa kubwa lakin nikama ndo tulikuw tunachochea moto.

Baada ya hapo matukio ni mengi sana hapa katikati ila kwa hili alilofanya kipindi hiki ni hatari zaidi. Ameanza kidato cha kwanza vizuri na kwa matokeo mazuri tu ya shule ya msingi kuanzia mwezi wa 1 mpaka mwezi wa sita matokeo yalikuja mabovu sijawahi ona. Somo alilofaulu sana alikuwa na arobaini nalo ni Kiswahili hayo mengine ni 14, 4.

Aisee ndio kuchukua maamuzi kwenda shuleni kukuta taarifa mtoto ni mtoro sugu, siku alizoingia darasani zinahesabika na kila siku anapewa hela ya shule. Ndio kufatili kwa makini kumbe anashinda chimbo na jamaa yake ambao wanaacha begi na nguo za shule kwa huyo jamaa, wanavaa nguo za nyumbani waneenda ps muda wa kurudi shule wanapitia kwa jamaa anavaa kama alivyoondoka asubuhi na kurudi nyumbani.

Basi hapa tulimkamata, tulipiga sana nusu kuua mpaka Mwalimu Mkuu aliingilia kati akasema hapa amenyoka. Tukampa mwalimu wa kumfatilia walivofungua shule kama wiki mbili tu hivi nikaitwa shuleni kwamba mwanao amekodi wahuni wa mtaani waje kumpiga mwalimu.

Aisee hapa nilipatwa na hasira sana, nilimpiga kiganja kimoja cha maana ndio nikamwambia jieeleze, ndio kuniambia wale wahuni aliwanunulia packet tatu za sigara akawapa na hela ya bangi ili waje kumpiga mwalimu!

Nilikuw najiuliza huyu ni mtoto wa namna gani licha ya mimi utotoni kuwa mtundu lakini kwa huyu mtoto ni zaidi. Mwezi wa 11 nilimpa hela apeleke shule, yeye akala ile hela na alivyogundua nimejua hajapeleka hela shuleni akaja nyumbani akaingia chumbani kwangu akapekenyua hela akabeba elfu hamsini akakimbia, hajalala nyumbani siku mbili, tukamtafuta tukampata.

Tulimpa kipigo kikali, nina jamaa angu polisi nikampigia simu aje amchimbe mikwara, jamaa kweli alikuja mpaka nyumbani na gari ya polisi na badhi ya askari na kule kwenye gari kulikuwa na waharifu waliopigwa na wananchi wamechakaa damu wanapelekwa hospitali nikasema mbebeni na huyu kwa lengo la dogo aogope ajue kichapo kilivyo huko njee na biti za polisi.

Walizunguka nae wakamrudisha jioni hapa alikuwa mpole balaa mpaka kilichotokea hiki sasa mpaka hapa naandika huu uzi huyu mtoto kaiba laki moja na kakimbia toka jana.

Naombeni mnisaidie mbinu gani ni itumie kwa huyu mafia ili akae sawa, kama ni kipigo nimepiga mnoo, ushauri kapewa mpaka na wachungaji lakini bado.

Naona hili nisikio la kufa.
 
Habarini wana JF. Moja kwa moja kwenye mada kama kichwa hapo juu kinavyojieeleza huyu ni mtoto wa jamaa angu nimeona niandike kwa jiri yake labda tutapata msaada humu ndani maan binafsi nimeshindwa

Nina mtoto kwa sasa ana umri wa miaka kumi na nne 14 yupo kidato cha kwanza lakin kwa mwenendo wake naona ata kidato cha pili hatoboi dg ana matukio ya ajabu sana na tumejitahidi kwa kila njia lakin imeshindikana ntaweka matukio yake kiufupi.

Mwanzo kabisa wakati yupo darasa la tano alikimbia nyumban hapa alitoka pugu mbaka kinyerezi kwa mguu kwa madai hakupendi tulijua ni kwa sababu ya utoto tulimtafuta kama siku mbili na kwa msaada wa polisi tulimpata tukapiga kidogo tukaacha aka kaa saw akanza tutesa na tabia ya udokozi wa ela ndogondogo na anakopeleka ni kwenye play station tukamshika tena tukapiga kwa ku ofia ataanza kudokoa ela kubwa kubwa lakin nikama ndo tulikuw tunachochea moto baada ya hapo matukio ni mengi sana hapa katikati ila kwa hili alilofinya kipindi iki ni hatari zaidi ameanza kidato cha kwanza vizuru na kwa matokeo mazuri tu ya shule ya msingi kuanzia mwezi wa 1 mbaka mwezi wa sita matokeo yalikuja mabovu sijawahi ona somo alilofaulu sana alikuwa na arobaini nalo ni kiswahili ayo mengine ni 14, 4 aisee ndo kuchukua maamuzi kwenda shuleni kukuta taarifa mtoto ni mtoro sugu siku alizoingia darasan zinahesabika na kila siku anapewa ela ya shule ndo kufatili kwa makini kumbe anashinda chimbo na jamaa yake ambao wanaacha begi na nguo za shule kwa uyo jamaa wanavaa nguo za nyumbani waneenda ps mdaa wa kurudi shule wanapitia kwa jamaa anavaa kama alivyoondoka asubuhi na kurudi nyumban basi hapa tulimkamata tulipiga sana nusu kuua mbaka mwalimu mkuu aliingilia kati akasema hapa amenyoka

Tukampa mwalimu wa kumfatilia walivofungua shule kama wiki mbili tu iv nikaitwa shuleni kwamba mwanao amekodi wauni wa mtaani waje kumpiga mwalimu aisee hapa nilipatwa na hasira sana nilimpiga kiganja kimoja cha maana ndo nikamwambia jieeleze ndo kuniambia wale wauni aliwanunulia packet tatu za sigara akawapa na ela ya bangi ili waje kumpiga mwalimu nilikuw najiuliza huyu ni mtoto wa namna gani licha ya mimi utotoni kuwa mtundu lakini kwa huyu mtoto ni zaidi mwezi wa 11 nilimpa ela apeleke shule yeye akala ile ela na alivyogundua nimejua ajapeleka ela shuleni akaja nyumbani akaingia chumbani kwangu akapekenyua ela aka beba elfu hamsini akakimbia ajalala nyumbani siku mbili tukamtafuta tukampata tulimpa kipigo kikali nina jamaa angu polisi nikampigia simu aje amchimbe mikwala jamaa kweli alikuj mbaka nyumbani na gari ya polisi na badhi ya askari nakule kwenye gari kulikuw na waarifu waliopigwa na wananchi wamchakaa damu wanapelekwa hospitali nikasema mbebeni na huyu kwa lengo la dogo aogope ajue kichapo kilivyo uko njee na biti za polisi walizunguka nae wakamrudisha jioni apa alikuwa mpole balaa mbaka kilichotokea hiki sas mdaa mbaka apa naandika huu uzi huyu mtoto kaiba laki moja na kakimbia toka jana.
Naombeni mnisaidie mbinu gani ni itumie kwa huyu mafia ili akae saw kama ni kipigo nimepiga mnoo ushauri kapewa mbaka na wachungaji lakini bado. Naona hili nisikio la kufa..

1: Huyu mtoto unaishi nae wewe? Anaetoa maelezo ni wewe ukiwa unaishi na mtoto wa jamaa yako au unatoa maelezo ya mzazi anaeishi na mwanae.

2: Huyu mtoto wazazi/familia yake unaifahamu vyema?

3: Mmejaribu kuitambua saikolojia ya mtoto na anachokihitaji maishani?
 
Huyo unafanya kumrelease tu aingie mtaani na kumpiga marufuku kabisa kukanyaga nyumbani nadhani hapo atapata uhuru wake wa kutosha. Vitu vingine siyo vya kulazimisha just let the nature to take its coarse bro......hawa madogo walioharibikiwa mitaani msidhani hawana wazazi waliowapigania ndo basi tu ilishindikana. Wewe kama mzazi kwa namna ulivoeleza ni tiyari ushafanya jukumu lako na jitihada zako zinaonekana ila ndiyo hvo imeshindikana.......Let him to the streets.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom