Kutokana Yote Tunayafahamu Mpaka Sasa, Sharif Alipanga Kurudi CCM kwa Kupitia Njia ya Uchaguzi. Kawaida Wapinzani Dhaifu Wanarudi CCM kwa Njia ya Kutangaza Habari Maalumu Ila Sharif Ametumia Tactic Mpya ya Kukiua Chama Chake. Wananchi Tunajua Jinsi Gani Sharif Alikuwa Tayari Kupigana Alipoambiwa Kashindwa 2005 Leo Hii Tunaona Tofauti. Huu Uchaguzi wa Visiwani Unaonekana Kabisa CCM Walishindwa Sana na CUF Ila Kilichoshangaza Sharif Alikubali Haraka Sana Kupata Ofisi ya Makamu wa Raisi. Hii ni Tamaa Yake ya Madaraka na Visiwani Watajuta. Lipumba Mwenyewe Kapatwa Butwaa Aliposikia Kwenye Habari Sharif Kakubali Matokeo. Kwa Kifupi Bara, CUF Imekufa na Tunaona Wabunge Wao Hawana la Kufanya Ila Kuingia Kwenye Vikao vya CCM na Kukubali Kila Hoja ya CCM. CUF Imeingizwa Kwenye Vitabu vya Malipo vya CCM Hata CCM Wenyewe Hawakuamini Ingekuwa Raisi Hivi, the Strategy Work. Hizi Ndio Siasa za Visiwani, Hakuna Jipya Huko Issue Yao Kubwa ni Kujitenga. Wananchi Bara Mpaka Leo Hatujui Malengo ya CUF na Upinzani Wao Hauleweki Inchini. Kwa Wale Mnaotaka Kupeleka Mijadala Kwenye Udini, Hii Sio Nafasi Yenu Jitete na Hoja Yako Mwananchi... Kitu cha Kuuliza Wananchi Bara, Kuna Haja ya Tujali Sana Hatua za CUF Visiwani? Wanatupa Faida Yeyote