The Don
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 3,499
- 1,163
Mimi nina girlfriend ambaye nimedumu nae katika mahusiano kwa miaka kama minne na sasa yupo masomoni,kiukweli nampenda sana ila sijui upande wake japo anajitahidi kwa kiasi chake kuonyesha mapenzi ya dhati,tumepitia mengi yani shida na raha na mitafaruku ya hapa na pale,yani nilimjali kwa kila kitu mf. Pesa,msaada wa kimawazo nk,kutokana na kwamba bahati mbaya wazazi wake walikwishaaga dunia mda mrefu kidogo na kuwaacha ktk hali ngumu ya maisha kidogo,nilikuwa nachat nae km kawaida na alinambia anakuja tarehe moja mwezi huu wa sita,ila jana nimewasiliana na rafiki zake wawili kuwajulia hali walichonijibu sikuamini,wapo likizo yani wamerudi nyumbani jana wakiwa wote ila mpaka sasa hapatikani na hajanitafuta,naona jini kisirani kaingia kwa kasi sana kwani mimi kila nikisafiri nikirudi lazima nimtaarifu,je ananipima au ndo naibiwa? Msaada tafadhali kwani nashindwa kufanya chochote nifanyeje