Nimfanye nini huyu Mwanamke?

Tegelezeni

JF-Expert Member
Dec 31, 2009
268
124
Mke wangu nimedumu naye kwa miaka minne sasa, katika ndoa yetu tumebahatika kupata mtoto wa kiume mmoja, na baada ya mtoto kutimiza miaka mitatu, tuliamua tupate mtoto mwingine. Tumefanya majaribio kadhaa kwa takriban miezi tisa lakini mke wangu hakushika mimba. Tukaenda kwa wataalamu na baada ya kushauriwa na kupewa tiba, ndipo mimba ikashika, lakini ilianza na matatizo na akahitajiwa akae Bed Rest.

Wakati ujauzito wa mke wangu ulipotimiza miezi miwili, hivi karibuni akapata msiba wa kaka yake aliyemlea. Mimi sikuwepo mjini kwa sababu nilisafiri kikazi mikoani. Alinipigia simu kunipa taarifa za msiba na akanijulisha kwamba mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda kijijini kwao kwa mazishi. aliniaga kwamba na yeye atasafiri na mwili wa marehemu kwenda kuzika. Nilimshauri asisafiri kutokana na hali yake, na nilimuhakikishia kwamba nitakaporudi nitafanya utaratibu ili twende tukahani msiba. Alikataa katakata na akanioana mimi ni mbaya kwa sababu nimemkatalia kwenda kumzika kaka yake aliyemlea na kumsomesha. Nikamwambia aende lakini sitahusika na lolote litakalotokea akipata matatizo.

Ni kweli aliamua kwenda lakini akiwa njiani alipata matatizo na ikabidi akimbizwe hospitai ya karibu na ule ujauzito ukatoka. Hakumudu kuendelea na safari na wala hakuhudhuria mazishi ya kaka yake. Nimezipokea taarifa hizi kwa uchungu sana. Sasa najiuliza nikirejea nimfanye nini huyu mwanamke?
 
ssa wewe hujui kwenye habari za msiba wanawake huwa wanafanya maamuzi ambayo siyo rational??????
 
msamehe tu ujue mtu ukifiwa na mtu ambaye alikusaidia katika maisha yako lazima akili itachange ila pole sana mkuu then saikolojikali ameshaharibika wewe mtie moyo then maisha yenu yatakuwa na furaha tena
 
Asiyesikia la mkuu,msamehe tu,naamini hakutegemea kama ujauzito ungetoka.Akili yote iliishia kwenda kumzika kaka yake.BIBLIA INASEMA "ENYI WAUME ISHINI NA WAKE ZENU KWA AKILI MAANA NI VIUMBE DHAIFU"

Unajua swala la yeye kushika ujauzito lilitusumbua sana na lilitugharimu pia, inashangaza anachukua maamuzi ambayo sio kwamba yalikuwa yanahatarisha maisha ya hicho kiumbe, bali pia hata maisha yake! hivi alikuwa anatumia akili au matope?
 
ssa wewe hujui kwenye habari za msiba wanawake huwa wanafanya maamuzi ambayo siyo rational??????


The Boss nakubaliana na wewe, lakini pale ambapo mume anatoa ushauri tena wa msingi halafu ukapuuzwa, basi hapo kuna walakini. Na huyu amekuwa mtovu wa nidhamu, kushindwa kumtii mumewe wa ndoa.
 
Unajua swala la yeye kushika ujauzito lilitusumbua sana na lilitugharimu pia, inashangaza anachukua maamuzi ambayo sio kwamba yalikuwa yanahatarisha maisha ya hicho kiumbe, bali pia hata maisha yake! hivi alikuwa anatumia akili au matope?

Inaonekana una hasira sana mkuu.. just relax ndio yameshatokea hayo msamehe mkeo mkae pamoja mjaribu tena
 
Unajua swala la yeye kushika ujauzito lilitusumbua sana na lilitugharimu pia, inashangaza anachukua maamuzi ambayo sio kwamba yalikuwa yanahatarisha maisha ya hicho kiumbe, bali pia hata maisha yake! hivi alikuwa anatumia akili au matope?
Hujawahi kufiwa na mtu aliekuwa wa muhimu sana maishani mwako?Mimba itashika nyingine tu.
 
Mkuu mpaka dakika hii mkeo ameshapata fundisho, unachopaswa kufanya kwa wakati huu ni kukubali yaliyotokea, kumsamehe kisha kuwa upande wake na kumpa moyo ili arejee katika hali yake ya kawaida..!

Mapendo.
 
Yaani mi nakuona wewe ni bonge la kilaza, hujui kama hiyo mimba ingetoka kama haikupangwa mtoto kuzaliwa bila kujalisha kama ingetoka akiwa safarini au amekaa?.
 
The Boss nakubaliana na wewe, lakini pale ambapo mume anatoa ushauri tena wa msingi halafu ukapuuzwa, basi hapo kuna walakini. Na huyu amekuwa mtovu wa nidhamu, kushindwa kumtii mumewe wa ndoa.

wakati mwingine ukiwafuata sana kina ananilea nkya ndio matatizo kama hayo yanatokea..

kwani angewaambia nduguze wangemtenga wakati wanafahamu anatatizo. mwambie aache kujistukia itamcost zaidi ya hapo.
 
Hujawahi kufiwa na mtu aliekuwa wa muhimu sana maishani mwako?Mimba itashika nyingine tu.

Nimefiwa na mama, when I was young, na nilifiwa na baba ambaye nilimuuguza mwenyewe na akarudi nyumbani akiwa amepona lakini akazidiwa ghafla na kufariki, but I didin't panic, nilijipanga na kwenda nyumbani kuzika. so what is abig dill kufiwa na kaka! All of us we will die one day, none of us wil live forever!
 
Sasa utajuaje kuwa haikupangwa mtoto asizaliwe. Kusema kuwa ni kilaza siyo sahihi.
 
Kwani wewe ndo Mungu, hakuna lolote la kumfanya Mungu ndo kajalia mtoto asizaliwe wewe hata ukienda kwa waganga kama mungu hataki upate mtoto hutapata.

Hata ukiowa wanawake wengine kama mungu hataki wewe kupata mtoto utaishia kwenda kujitubu kwa waganga au madaktari wa kila aina katika hospital za dunia nzima na hupati kitu, tulia kijana na mke wako...Wacha hasira kama mungu kajalia kupata watoto utapata tu siku za mbele.

FYI mimi najua kuna mwanamke mmoja alikuwa akitaka kutoa mimba-alikunywa madawa ya kila aina na mimba haikutoka....Hapo lazima uweke akili Mungu akisema yes ni Yes tu hakuna No.
 
Mi nadhani ukifika nyumbani wala husimgombeze mkeo,kwanza mpe pole kwa msiba wa kaka yake na yaliyotokea. Ameshajifunza na hakupenda yatokee hayo,pia usifanye mchezo na kufiwa na kaka especially aliyekuleya.....Mungu atawapa mtoto mwingine!!!
 
Mi nadhani ukifika nyumbani wala husimgombeze mkeo,kwanza mpe pole kwa msiba wa kaka yake na yaliyotokea. Ameshajifunza na hakupenda yatokee hayo,pia usifanye mchezo na kufiwa na kaka especially aliyekuleya.....Mungu atawapa mtoto mwingine!!!


Mbona mimi nilifiwa na aliyenizaa kabisa na wala siku-panic!
 
wanawake hata wao hawajielewi
tena wakikatazwa ndo hutaka kufanya
hasa wanapokuwa na uhakika wa Love and protection.

Wala usimgombeze
ana machungu ya kufiwa na mimba
ni fundisho kwa leo na siku zijazo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom