habari zenu wana jamvi.mimi nipo ughaibuni huku nasoma,sasa kuna msichana mmoja tuna uhusiano wa karibu miezi kumi sasa.kabla yangu mimi huyu msichana kashawahi kuwa na relationships mbili,wa kwanza waliachana kwa ugomvi sana na mpaka sasa ata wakikutana njiani ni kama maadui vile,ila huyu wa pili jamaa alikuja kusoma kwa semester moja then walikuwa wapenzi kwa karibu miezi miwili na nusu kisha jamaa akarudi kwao.ila kinachonitatiza mimi ni kwamba bado wana mawasiliano kwenye internet especially in facebook.miezi kama mitatu hivi iliyopita jamaa alimwambia msichana kwamba anataka kuja tena kusoma kwa summer time pekee ila alimwambia demu kuwa je akija wataweza kufanya mapenzi tena au la?basi msichana akawa amechanganyikiwa kweli ikabidi aje aniambie mimi maana anadai yeye jamaa anamchulia kama rafiki yake,mimi nikamwambia yeye uamuzi wake ukoje? demu akasema itabidi afikilie maana kachanganyikiwa hajui afanye nini ila mimi nikamwambia kwa kipindi hicho anachofikilia itabidi tuwe just friends na sio wapenzi demu akakubali japo kwa shingo upande.baada ya wiki moja na nusu demu akataka tukutane tuongee mimi sikuwa na kinyongo tukakutana then demu akasema kwamba anavyoona yeye jamaa anataka kumchezea tu then atamuacha kama alivyomuacha mwanzo then akaomba msamaa ili tuwe pamoja maana mimi ndio anaona mtu ninayemfaa sana kuja kuwa baba wa familia yake,mimi nikamsamehe japo kwa shingo upande,basi tukaendeleza uhusiano wetu kwa karibu miezi minne tunafurahi na kusahau yote yaliyopita.sasa tatizo linakuja yeye bado sometimes anaendelea kuchati na huyo jamaa yake japo huyu msichana ananiheshimu sana hana mambo ya kipuuzi,sasa last week alikuja kwangu kulala tukafanya mapenzi kama kawaida then kulala sasa katikati ya usiku demu akamuota jamaa yake huyo anaechati nae sometimes,asubuhi kuamka akaniambia ameota ndoto mbaya sana nikajaribu kumdadisi ila akusema kitu then next day akaja akniambia kuhusu hiyo ndoto ila imemchanganya sana kwa sababu yeye yuko na mimi tumelala pamoja sasa kwa nini amuote jamaa basi demu akawa kachanganyikiwa tena, mimi nikamuambia ile ni ndoto tu na si kweli demu akakomaa anadai inabidi afikilie ile ndoto inamaanisha nini maana ataki kuja kunibetray baadae maana ananipenda sana na mimi ni mwema sana kwake.akaenda kujadiliana na rafiki zake huko then akaja anasema eti ile ni ndoto tu na sasa hivi haipi sana uzito then tuendelee tu na uhusiano wetu kama kawaida.mimi ikabidi nisafiri kwa siku tatu kwenda kula bata then nikirudi nifikilie nini nitafanya,sasa leo ndio tunakutana tena sasa wadau mnanishauri nimwambie nini huyu msichana?nimuache au niendelee nae tu? ila demu mwenyewe ni mzungu ana 22 years old