Nimeyapenda maoni ya mhariri katika gazeti hili kuhusu Rais kushusha mishahara

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
"RAIS AONGEZE, ASIPUNGUZE MISHAHARA

SAKATA la mishahara minono ya vigogo katika mashirika ya umma, limekuwa sehemu ya mazungumzo kila mahali, hasa kwenye vyombo vya habari.

Mazungumzo hayo ambayo yamebeba mawazo tofauti, yametokana na kauli ya rais kwamba, amekusudia kupunguza mishahara ya baadhi ya eatendaji wakuu katika mashirika ya umma.

Rais hakutumia maneno mepesi,. Alisema, kwa mishahara yao minono , watendaji hao wamekuwa wanaishi kama malaika na kwamba ataishusha ili waishi kama shetani.

Haya ni maneno yasiyotarajiwa kutamkwa hadharani na kiongozi mkuu wa nchi.Hayapaswi kutoka Ikulu.

Kwa rais kutamka haya ni dalili kwamba anatumia ushauri wa watu wasiojua jinsi mishahara ya watendaji hao inavyopangwa, au uvumi wa wananchi masikini wanaodhani kwamba watendaji hao wanalipwa kiasi kikubwa mno wasichostahili.

Kumwambia masikini anayebangaiza mlo wa siku kwamba kuna watendaji wanaolipwa Sh. 36 milioni kwa mwezi, ni kujaribu kujenga uhasama kwa jamii.

Ni njia ya kuchochea masikini kuchukia mafanikio au watu waliofanikiwa.

Hata kauli yake kwamba anatamani watu waishi kama shetani , sio kauli inayopaswa kutolewa na kiongozi mkuu wa nchi, hata kama kuna baadhi ya wasikilizaji wake wanapigia makofi kauli hiyo.

Kupunguza mishahara ya watu ambayo imepangwa kwa mujibu wa taratibu zisizotegemea kauli yake, ni ubabe tu.

Taasisi zinazosimamia zina viwango vya mishahara ambavyo huwekwa na bodi kwa vigezo rasmi vinavyoongoza taasisi hizo.

Lakini kwa kauli za rais, ni wazi kuwa anawajengea wananchi hisia kwamba wakuu wa taasisi hizi “wanajipa mamilioni”.Anataka jamii iwaone kama wezi.

Sisi tunaamini kwamba wananchi makini hawawezi kubabaikia kauli za kibabe za rais ambazo zinachochea, zinaenzi na kutukuza ubabe.

Hatuwezi kuingia katika mkumbo wa kutukuza kila kauli anayotoa rais, huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo, tunajenga uhasama kati ya wenyenacho na wasionacho.

Na tunadhani kuwa rais angekuwa amelitendea haki taifa , angejibisha kuinua uchumi , ili mishahara ya wafanyakazi wote ipande badala ya kupunguza mikubwa iliyopo.

Hao wenye mishahara mikubwa siyo wezi. Ni watu waliowekeza katika elimu, ujuzi, uzoefu na stadi mbalimbali zilizowafikisha katika ngazi za juu kiuongozi."

S
ource: MwanaHalisi 04/04/2016
 
Hii nchi tulipofikia tunahitaji Raisi wa aina hii, kwani watz pamoja na mwandishi ni watu wa majungu tu, na majungu kama haya ndo yameifikisha hii nchi hapa, wakati wa JK pia walisema ni mpole sana na ndo maana Tz imekuwa kama shamba la bibi, ss leo tumepata kiongozi ambaye anatuonyesha mafanikio na kutuondoa ujinga wa majungu na kutokufanya, tunamwona kama ni mbabe, huu mm nasema ni upumbavu.
 
tukitaka rushwa kubwa isiwepo mishahara mikubwa kwa mabosi sharti iwepo. pia kumbuka wenye fani za pekee wanaolipwa vizuri zaidi ktk taasisi binafc na za kimataifa hawatajiynga na taasisi za serikali. tutawakosa jamani. angalia kwa uchache. Gavana wa BOT alikuwa workd bank, mcheck Mchechu wa NHC alikuwa sekta binafc. check maendeleo yao halafu unakomaa wapunguziwe salary!
 
tukitaka rushwa kubwa isiwepo mishahara mikubwa kwa mabosi sharti iwepo. pia kumbuka wenye fani za pekee wanaolipwa vizuri zaidi ktk taasisi binafc na za kimataifa hawatajiynga na taasisi za serikali. tutawakosa jamani. angalia kwa uchache. Gavana wa BOT alikuwa workd bank, mcheck Mchechu wa NHC alikuwa sekta binafc. check maendeleo yao halafu unakomaa wapunguziwe salary!
Si kweli , wawekee watch dogs
Kila MTU alipwe anachostahili
 
"RAIS AONGEZE, ASIPUNGUZE MISHAHARA

SAKATA la mishahara minono ya vigogo katika mashirika ya umma, limekuwa sehemu ya mazungumzo kila mahali, hasa kwenye vyombo vya habari.

Mazungumzo hayo ambayo yamebeba mawazo tofauti, yametokana na kauli ya rais kwamba, amekusudia kupunguza mishahara ya baadhi ya eatendaji wakuu katika mashirika ya umma.

Rais hakutumia maneno mepesi,. Alisema, kwa mishahara yao minono , watendaji hao wamekuwa wanaishi kama malaika na kwamba ataishusha ili waishi kama shetani.

Haya ni maneno yasiyotarajiwa kutamkwa hadharani na kiongozi mkuu wa nchi.Hayapaswi kutoka Ikulu.

Kwa rais kutamka haya ni dalili kwamba anatumia ushauri wa watu wasiojua jinsi mishahara ya watendaji hao inavyopangwa, au uvumi wa wananchi masikini wanaodhani kwamba watendaji hao wanalipwa kiasi kikubwa mno wasichostahili.

Kumwambia masikini anayebangaiza mlo wa siku kwamba kuna watendaji wanaolipwa Sh. 36 milioni kwa mwezi, ni kujaribu kujenga uhasama kwa jamii.

Ni njia ya kuchochea masikini kuchukia mafanikio au watu waliofanikiwa.

Hata kauli yake kwamba anatamani watu waishi kama shetani , sio kauli inayopaswa kutolewa na kiongozi mkuu wa nchi, hata kama kuna baadhi ya wasikilizaji wake wanapigia makofi kauli hiyo.

Kupunguza mishahara ya watu ambayo imepangwa kwa mujibu wa taratibu zisizotegemea kauli yake, ni ubabe tu.

Taasisi zinazosimamia zina viwango vya mishahara ambavyo huwekwa na bodi kwa vigezo rasmi vinavyoongoza taasisi hizo.

Lakini kwa kauli za rais, ni wazi kuwa anawajengea wananchi hisia kwamba wakuu wa taasisi hizi “wanajipa mamilioni”.Anataka jamii iwaone kama wezi.

Sisi tunaamini kwamba wananchi makini hawawezi kubabaikia kauli za kibabe za rais ambazo zinachochea, zinaenzi na kutukuza ubabe.

Hatuwezi kuingia katika mkumbo wa kutukuza kila kauli anayotoa rais, huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo, tunajenga uhasama kati ya wenyenacho na wasionacho.

Na tunadhani kuwa rais angekuwa amelitendea haki taifa , angejibisha kuinua uchumi , ili mishahara ya wafanyakazi wote ipande badala ya kupunguza mikubwa iliyopo.

Hao wenye mishahara mikubwa siyo wezi. Ni watu waliowekeza katika elimu, ujuzi, uzoefu na stadi mbalimbali zilizowafikisha katika ngazi za juu kiuongozi."

S
ource: MwanaHalisi 04/04/2016
Nakubaliana na wewe mwandishi kwa asilimia nyingi isipokua aya ya 6 na 7 hukupaswa kukosoa kwan naona Magu yuko sahihi na wananchi wajue nin kinachofanyika serilalin ili pale panapobid wahoji dhid ya kod zao
 
Hii nchi tulipofikia tunahitaji Raisi wa aina hii, kwani watz pamoja na mwandishi ni watu wa majungu tu, na majungu kama haya ndo yameifikisha hii nchi hapa, wakati wa JK pia walisema ni mpole sana na ndo maana Tz imekuwa kama shamba la bibi, ss leo tumepata kiongozi ambaye anatuonyesha mafanikio na kutuondoa ujinga wa majungu na kutokufanya, tunamwona kama ni mbabe, huu mm nasema ni upumbavu.
Rais anatakiwa achuje maneno ya kinywa chake. Rais ni role model. Siyo busara kuwaambia watu anaowaongoza atawafanya waishe kama shetani. Kwanza tujue shetani anaishije? Biblia yangu inasema shetani ni mwuaji na tena ni mwongo (Yonana 8:44)
 
Mishahara minono ingekuwa inazuia tamaa hapo wanaotuhumiwa humu Jamii forums wangekuwa na hizi makashfa? Wapewe mishahara reasonable na wafanye kazi kwa uaminifu. Mwingine spate laki Tatu kwa mwezi mwingine M40 ni sasa? Kazi ya DG na kazi ya Mwalimu zote zona umuhimu sasa. Hata kama una PHD ni lazima ukumbuke kuwa uneitia kwa Mwalimu akieanza na wewe ukiwa hujui hata Ba Be Bi Bo By. Mishahara ya serikali isitofautiane kwa Kiwango hicho Si vyema. Ni unyonyaji tena mkubwa.
 
Lengo la mr president si baya japo kwa upande wa pili ningemuomba kuboost wale walioko chini kbs wanaolipwa kima cha chini kabisa...
Mwenye kima kidogo cha mshahaka ktk kodi yake angepunguziwa na yule mweny kulipwa million 30 aongezewe kodi
 
"RAIS AONGEZE, ASIPUNGUZE MISHAHARA

SAKATA la mishahara minono ya vigogo katika mashirika ya umma, limekuwa sehemu ya mazungumzo kila mahali, hasa kwenye vyombo vya habari.

Mazungumzo hayo ambayo yamebeba mawazo tofauti, yametokana na kauli ya rais kwamba, amekusudia kupunguza mishahara ya baadhi ya eatendaji wakuu katika mashirika ya umma.

Rais hakutumia maneno mepesi,. Alisema, kwa mishahara yao minono , watendaji hao wamekuwa wanaishi kama malaika na kwamba ataishusha ili waishi kama shetani.

Haya ni maneno yasiyotarajiwa kutamkwa hadharani na kiongozi mkuu wa nchi.Hayapaswi kutoka Ikulu.

Kwa rais kutamka haya ni dalili kwamba anatumia ushauri wa watu wasiojua jinsi mishahara ya watendaji hao inavyopangwa, au uvumi wa wananchi masikini wanaodhani kwamba watendaji hao wanalipwa kiasi kikubwa mno wasichostahili.

Kumwambia masikini anayebangaiza mlo wa siku kwamba kuna watendaji wanaolipwa Sh. 36 milioni kwa mwezi, ni kujaribu kujenga uhasama kwa jamii.

Ni njia ya kuchochea masikini kuchukia mafanikio au watu waliofanikiwa.

Hata kauli yake kwamba anatamani watu waishi kama shetani , sio kauli inayopaswa kutolewa na kiongozi mkuu wa nchi, hata kama kuna baadhi ya wasikilizaji wake wanapigia makofi kauli hiyo.

Kupunguza mishahara ya watu ambayo imepangwa kwa mujibu wa taratibu zisizotegemea kauli yake, ni ubabe tu.

Taasisi zinazosimamia zina viwango vya mishahara ambavyo huwekwa na bodi kwa vigezo rasmi vinavyoongoza taasisi hizo.

Lakini kwa kauli za rais, ni wazi kuwa anawajengea wananchi hisia kwamba wakuu wa taasisi hizi “wanajipa mamilioni”.Anataka jamii iwaone kama wezi.

Sisi tunaamini kwamba wananchi makini hawawezi kubabaikia kauli za kibabe za rais ambazo zinachochea, zinaenzi na kutukuza ubabe.

Hatuwezi kuingia katika mkumbo wa kutukuza kila kauli anayotoa rais, huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo, tunajenga uhasama kati ya wenyenacho na wasionacho.

Na tunadhani kuwa rais angekuwa amelitendea haki taifa , angejibisha kuinua uchumi , ili mishahara ya wafanyakazi wote ipande badala ya kupunguza mikubwa iliyopo.

Hao wenye mishahara mikubwa siyo wezi. Ni watu waliowekeza katika elimu, ujuzi, uzoefu na stadi mbalimbali zilizowafikisha katika ngazi za juu kiuongozi."

S
ource: MwanaHalisi 04/04/2016
Pole; mhariri hajui anachokiandika; nani alimwambia bodi in mamlaka ya kuwaibia wananchi? Bodi hizi zilizoruhusu flow meter zifungwe kwa miaka mitano? Bodi kama ya nssf inayonunua ardhi ekari moja kwa shs milioni 800? Bodi zinazosafiri nje ya nchi kufanya vikao?! Bs
 
Duh ati waishi kama shetani hii kweli kauli inatoka kwa kiongozi mkuu wa nchi? sijui Makonda atatoa kauli ipi mmhh
 
Back
Top Bottom