Washawasha
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 16,652
- 13,077
Habari zenu wanajamvi ni hivi leo asubuhi nikiwa kituoni nasubiri 5 5 ili nielekee kazini,watu walikuwa wamesheheni kusubiri usafiri basi ghafla bin vuu akatokea chizi ana mshipa(bu sha) mkubwa na kuanza kutumwagia mchanga watu tuliokuwa tukisubiri usafiri,kwa kweli alituchafua na amani ilitoweka kwa watu kuanza kukimbia ovyo ovyo kwa kuhofia kumwagiwa michanga na yule chizi ,basi mie nikamvizia kwa nyuma yule chizi na nikaubutua ule mshipa wake kwa nguvu,yule chizi alikaa chini na kutulia mwenyewe,basi kwa kitendo changu kile wengine wakiniunga mkono wengine wakinikandia,je nimefanya makosa au nimepatia?Nalog off