GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,738
- 109,177
Baba yake Mzazi ni Rafiki yangu mkubwa sana tu na tunaheshimiana halafu hata Kiumri ni kama Mdogo wangu ila tatizo ni kwamba Mwanamke wake wa sasa sijui keshamroga au hapana kwani ( Jamaa ) hapindui kwa huyo Mwanamke ( yaani Mkewe )
Sasa ni mwezi wa tatu unakatika tokea huyu Mtoto atoke kwa Mama yake na kuja kuishi na Baba yake ambaye ni Jirani yangu ila tokea aje / ahamie kwa Baba yake na kukutana na Mama yake wa Kambo ambaye pia ana Mtoto wake wa Kike sijawahi kuona siku yoyote ile huyu Mtoto akakosa ' Kupigwa ' na ' Kunyanyasika ' na huyu Mama yake wa Kambo anayeishi nae sasa.
GENTAMYCINE huwa nina huruma mno na uchungu na niliamua kuvumilia kunyamaza sasa naona yamenifika shingoni hivyo natafuta namna ya kumwambia Baba yake kuwa Mwanae anateswa na kupigwa mno na Mkewe tena kuna muda bila hata sababu za msingi.
Ila changamoto kubwa Kwangu ni jinsi tu ya kumuingia huyu Baba yake na aniamini kwani kwa huyu Mkewe Jamaa hapindui kabisa hivyo nimekimbilia Kwenu humu muweze kunisaidia kusudi nimuokoe huyu Mtoto kwani kwa dalili ambazo naziona kwa ' mateso ' anayoyapata huyu Mtoto kuna Siku Turubai la Msiba litawekwa pale Kwao na kwenda Kumzika huyu Mtoto wa Watu.
Je nifanyeje? Nimvae huyu Mama Yeye kama Yeye nimpe ' makavu ' yake au nimwambie Baba Mtoto ambaye kuna kila dalili ' Limbwata ' limeshamkolea au nijenge Urafiki wa Kimkakati na huyu Mtoto nimfundishe ' Ujeuri ' na ' Ubabe ' ili awe anamdindia Mama yake na ikibidi awe anampiga hata na Matofa / Mawe?
Dada zangu Wapendwa ( Wanawake ) mtanisamehe ila mna roho mbaya sana. Badilikeni tafadhali. Hivi mnawezaje kumchukia Mtoto wa Mwanamke mwenzako ambaye na Yeye pia aliutumikia ' Mkuyenge ' vilivyo kama ulivyoutumikia Wewe na akajifungua kama ulivyojifungua Wewe?
Najua wengi wenu humu mmeshazoea kuwa GENTAMYCINE ni Mtu wa Utani ila kwa hili nisiwaficheni limeniumiza na limenikera mno na hadi hasira kunipanda na natamani hata siku moja huyu Mama akosee tu anijibu hovyo ili nimpe ' Kipondo ' cha kulipizia Hasira zangu Kwake kwa jinsi anavyomtesa huyu Mtoto wa Watu. Imeniuma sana!
Nawasilisha.
Sasa ni mwezi wa tatu unakatika tokea huyu Mtoto atoke kwa Mama yake na kuja kuishi na Baba yake ambaye ni Jirani yangu ila tokea aje / ahamie kwa Baba yake na kukutana na Mama yake wa Kambo ambaye pia ana Mtoto wake wa Kike sijawahi kuona siku yoyote ile huyu Mtoto akakosa ' Kupigwa ' na ' Kunyanyasika ' na huyu Mama yake wa Kambo anayeishi nae sasa.
GENTAMYCINE huwa nina huruma mno na uchungu na niliamua kuvumilia kunyamaza sasa naona yamenifika shingoni hivyo natafuta namna ya kumwambia Baba yake kuwa Mwanae anateswa na kupigwa mno na Mkewe tena kuna muda bila hata sababu za msingi.
Ila changamoto kubwa Kwangu ni jinsi tu ya kumuingia huyu Baba yake na aniamini kwani kwa huyu Mkewe Jamaa hapindui kabisa hivyo nimekimbilia Kwenu humu muweze kunisaidia kusudi nimuokoe huyu Mtoto kwani kwa dalili ambazo naziona kwa ' mateso ' anayoyapata huyu Mtoto kuna Siku Turubai la Msiba litawekwa pale Kwao na kwenda Kumzika huyu Mtoto wa Watu.
Je nifanyeje? Nimvae huyu Mama Yeye kama Yeye nimpe ' makavu ' yake au nimwambie Baba Mtoto ambaye kuna kila dalili ' Limbwata ' limeshamkolea au nijenge Urafiki wa Kimkakati na huyu Mtoto nimfundishe ' Ujeuri ' na ' Ubabe ' ili awe anamdindia Mama yake na ikibidi awe anampiga hata na Matofa / Mawe?
Dada zangu Wapendwa ( Wanawake ) mtanisamehe ila mna roho mbaya sana. Badilikeni tafadhali. Hivi mnawezaje kumchukia Mtoto wa Mwanamke mwenzako ambaye na Yeye pia aliutumikia ' Mkuyenge ' vilivyo kama ulivyoutumikia Wewe na akajifungua kama ulivyojifungua Wewe?
Najua wengi wenu humu mmeshazoea kuwa GENTAMYCINE ni Mtu wa Utani ila kwa hili nisiwaficheni limeniumiza na limenikera mno na hadi hasira kunipanda na natamani hata siku moja huyu Mama akosee tu anijibu hovyo ili nimpe ' Kipondo ' cha kulipizia Hasira zangu Kwake kwa jinsi anavyomtesa huyu Mtoto wa Watu. Imeniuma sana!
Nawasilisha.