Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,882
- 2,762
Wadau nimeota ndoto. Ni kama tarehe 1 nov hivi ambapo zoezi la kuhesabu kura za urais linaelekea kukamilika. Taarifa zisizo rasmi ni kuwa Dr Slaa anaongoza kwa kura kwa %85 hivi. Nchi nzima imeshikwa ganzi kwa yanayoendelea. Ukimya umetawala kila kona huku wana wa nchi wakitafakari hili. NEC wanasita kutoa matokeo na ccm wapo kimya mno! Tupo na Dr. Slaa sehemu fulani akiwa na wapambe wake tunampa moyo na matumaini mapya. Hatimaye Kikwete anatoa kitabu fulani kidogo hivi ambacho Slaa anatakiwa kusaini tayari kwa taratibu za kutangazwa mshindi wa uchaguzi mkuu 2010! Oh Lord, grant my dear dream a potential reality, AMEN!