Nimempa akili huyu, "bila kula siku tatu!"

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
May 15, 2009
7,323
6,810
Juzi nilikuta ugumvi wa majirani wangu, kaka mkubwa na mdogo wake, kaka ni mkubwa kwa miaka 15 hivi. Kaka mtu anasema mdogo wake hamjali kabisa ingawa yeye ndiye aliemsomesha hadi darasa la saba alipofaulu na kuendelea na masomo hadi sasa kamaliza mavyuo na maisha yameanza kukaa vizuri.
Kaka mtu akasema "nilikuwa nakulaza njaa wewe siku tatu, hamna kula kitu chochote, na kukupiga nilikupuga! si unaona ulivyo na akili? tofauti na wenzio waliokulia raha." "mimi najua kulea bwana, angalia kina.........(akawataja ndugu zake) watoto wote waliokulia kwao hakuna aliyefanikiwa kama wewe!"
Sasa baadae mimi nikajiuliza hivi kumyima mtoto wa shule chakula siku tatu ni kujua kulea??
Kama ni kujua kulea yule bwana mkubwa itatakiwa awe anawanyima watoto wake wakuwazaa chakula kwa siku 6 hivi ili wawe na mafanikio maradufu, kwani hawezi kumlea vizuri mdogo wake kuliko watoto wake.
Mwisho, hivi jamani ni kweli ukimpa mtoto shuruba kama hizo za kumyima msosi atakuja kuwa na akili??
!
Yule mdogo mtu baadae akanifuata akaniambia kaka yake huwa anamkera sana kwa tabia yake hiyo...ya kumdhalilisha hata mbele ya mkewe na watoto akaniomba ushauri nikamwambia ntapa jibu, asubiri kwanza.. Jamani naomba ushauri wenu kwa niaba yake, please!
 
Kwanza kabisa, kwa machache yaliyosemwa hapa naweza kuona huyu kaka ana matatizo mengi, kuanzia hayo ya ukwasi wa roho mpaka kushindwa maisha.

Ukimsaidia mtu siyo basis ya kumsimanga akipata maendeleo baadaye.Huyo kaka anaonekana si mstaarabu na pia kashindwa maisha sasa anabaki kudandia kwa mdogo wake eti tu kwa sababu "alimsaidia".tenda wema uende zako, usingoje shukurani, na wala usitake kujitapa.
 
hilo jamaa ningekuwa mimi ningemtoa nduki kabisa asikanyage kwangu **** dush mkubwa
 
kama walizaliwa tumbo moja, wakalelewa na wazazi hao hao, huyo kaka mkubwa kwa......anini hana akili na anasema hivyo kum...funza mtu akili ni kum...nyima msosi ili kumaaa....anisha nini?

Na kama aaliweza kumpa akili wenzake kwa staili hiyo ya kunyima chakula ili afanikiwe, kwa...anainai sasa hakujinyima nae awe na akili? Au Nae kaka hiyo akili aliyoweza kumfundisha mdogo wake aliitoa wapi au wazazi wao ndo.......oooo walimfunza hivyo stailli??.


Kama shida ni mafanikio tu labda mdogo mtu amweleze ukweli kuwa hata asingenyimwa msosi au fedha za shule, kama shuleni hakuweza kuelewa au hana mipango ya masiha, bado hiy akili ambayo kaka anadai kamfundisha haina maana kwake..

Daima, hakuna mtu ambaye amefanikiwa hapa duniani kwa lolote pasipo kuwa na msaada wa hali na mali toka kwa mwingine. Hivyo, ukim....saaiadia mtu, haina maana umsimange.
 
mi nadhani ni bora walkae chini wazungumze kati yao ajue hasa haya maneno ya kaka yanatokana na nini? shida yake hasa aiweke wazi hapo patakuwa pazuri manake dogo naye atapata nafasi ya kujua kilichomo katika nafsi ya kaka yake kisha kupata suluhisho la matatizo yake kwani uamuzi anao yeye kujua chanzo ni nini na kutafuta suluhisho la kudumu.
 
ampigie hesabu ya gharama alizotumia, amlipe watemane!

Hii imenikumbusha ya rafiki yangu mmoja msomali alikua hapatani na baba yake kiasi cha kusema atapiga nyeto amrudishie mbegu baba yake watemane.
 
Siri ya mafanikio anayo mdogo mtu mpaka amefika hapo alipo, na kama hayo mafanikio yake bro alikuwa anamchango, mdogo mtu anajua alichosaidiwa. Kama udhalili unaendelea awatafute wazazi, ndugu, walezi, wenye busara kupata suluhu, ikishindikana bro ampigie maheasabu na alipwe mbele ya mashahidi na kwa maandishi ili mambo yaishe. Na amini undugu ni hazina, kufaana katu si kufanana.
 
Back
Top Bottom