LA7
JF-Expert Member
- Aug 26, 2019
- 457
- 1,706
Sijajua ni Nini hasa inanifanya Mimi kuwa na hasira kupita kiasi mpaka kwa watu wangu wa karibu,
Kwani nimekuwa nikiwajibu majibu ya mkato mpaka wanakuwa wanashangaa
Wengine huishia kunyamaza na wengine huniambia kuwa nimewajibu vibaya,
Hii Hali imeanza mwezi huu wa kwanza, natamani Sana nirudi Kama mwanzoni ili nisiwapoteze hawa marafiki zangu kwani wamekuwa wakiniambia kuwa nimebadilika Sana, na ni kweli nimebadilika,
Naweza ulizwa tu vizuri najikuta nisharudisha jibu chapu Tena bila hata kufikiria, utafikiri nilikuwa nasubiri niulizwe tu niteme jibu,
Kuna vitu ambavyo nahisi labda ni sababu kuu ya mimi kuwa hivi.
1. Madeni
Hapa nilipo nadaiwa kodi ya nyumbani 40, ofisini 40, hospital 50, na uhakika wa kulipa umekuwa ni mdogo, kwani mpaka chakula nakopa.
2. Kuishi mbali na mke wangu kwa miezi karibia 3
Toka mke wangu ajifungue Sasa umeisha mwezi ili bidi nimpeleke kwao kwasababu nyumbani kwao ni mkoa wa karibu na tunapoishi, kuliko mkoani kwetu.
3. Toka ajifungue sijaona hata sura ya mtoto
Ukweli ni kwamba simu yake imezingua kwenye mambo ya internet hivo ameshindwa hata kunitumia picha ya mtoto na amekosa hata ya kuazima, Ni muoga.
4.Nimekosa nauli ya kwenda kuwasalimia
Yaani kule kwao nimeendaga tu maramoja, na mahari bado sijapeleka na huyo mtoto ni wa pili, hivo nilipanga nikienda kuwasalimia nijipange hata na laki na nusu ili hata ya kuwapelekea zawadi ukweni.
Sijafanya mapenzi zaidi ya miezi 3
Jua kuwa Kali na joto kuongezeka.
Kuchelewa kulala bila sababu maalumu, yaani wastani nimekuwa nalala kuanzia saa 7 usiku naamka saa2 asubuhi
Je, Hizi yaweza Kuwa sababu mm kuwa na hasira?
Na nitumie mbinu gani ili nirudi Kama mwanzoni kwani siku hizi nagombana mpaka mitandaoni.
Nawasilisha by fundi simu
Kwani nimekuwa nikiwajibu majibu ya mkato mpaka wanakuwa wanashangaa
Wengine huishia kunyamaza na wengine huniambia kuwa nimewajibu vibaya,
Hii Hali imeanza mwezi huu wa kwanza, natamani Sana nirudi Kama mwanzoni ili nisiwapoteze hawa marafiki zangu kwani wamekuwa wakiniambia kuwa nimebadilika Sana, na ni kweli nimebadilika,
Naweza ulizwa tu vizuri najikuta nisharudisha jibu chapu Tena bila hata kufikiria, utafikiri nilikuwa nasubiri niulizwe tu niteme jibu,
Kuna vitu ambavyo nahisi labda ni sababu kuu ya mimi kuwa hivi.
1. Madeni
Hapa nilipo nadaiwa kodi ya nyumbani 40, ofisini 40, hospital 50, na uhakika wa kulipa umekuwa ni mdogo, kwani mpaka chakula nakopa.
2. Kuishi mbali na mke wangu kwa miezi karibia 3
Toka mke wangu ajifungue Sasa umeisha mwezi ili bidi nimpeleke kwao kwasababu nyumbani kwao ni mkoa wa karibu na tunapoishi, kuliko mkoani kwetu.
3. Toka ajifungue sijaona hata sura ya mtoto
Ukweli ni kwamba simu yake imezingua kwenye mambo ya internet hivo ameshindwa hata kunitumia picha ya mtoto na amekosa hata ya kuazima, Ni muoga.
4.Nimekosa nauli ya kwenda kuwasalimia
Yaani kule kwao nimeendaga tu maramoja, na mahari bado sijapeleka na huyo mtoto ni wa pili, hivo nilipanga nikienda kuwasalimia nijipange hata na laki na nusu ili hata ya kuwapelekea zawadi ukweni.
Sijafanya mapenzi zaidi ya miezi 3
Jua kuwa Kali na joto kuongezeka.
Kuchelewa kulala bila sababu maalumu, yaani wastani nimekuwa nalala kuanzia saa 7 usiku naamka saa2 asubuhi
Je, Hizi yaweza Kuwa sababu mm kuwa na hasira?
Na nitumie mbinu gani ili nirudi Kama mwanzoni kwani siku hizi nagombana mpaka mitandaoni.
Nawasilisha by fundi simu