ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Hali ya sasa kwa Babu ipo shwari ukifika inakuchukua muda mchache kupata kikombe kisha unageuza. Safari ya magari mengi kutoka Arusha Mjini ni usiku na kunako alfajiri upo kwa Babu..ukiweza unasikilza mawaidha yake kabla ya kujimiminia kikombe.
Msafara mrefu kwa sasa unasababishwa na wafuata huduma toka nchi za jirani hasa Kenya, Matatu toka Kericho, Nairobi Naivasha nk yanafika Samunge sasa. Fedha alizotoa Magufuri zimewezesha kukarabati barabara toka mto wa Mbu mpaka kwa babu japo vumbi ni jingi sana barabarani hasa kwa magari madogo kama saloon na Noah zinaweza kukwama kwenye vumbi.