Von_Lufuta
JF-Expert Member
- Mar 19, 2023
- 1,529
- 3,609
Habari za jumapili wakuu, hope mko vizuri. Nipo vizuri pia ingawa nipo njia panda kwa hili jambo.
Kuna jamaa zangu wawili mapacha wanyaturu huwa wana mdogo wao wa kike, ni mrembo Pro Max. Katika ile familia, naweza kumpa credit mama yao kwa kufyatua watoto wazuri kupita maelezo pale mtaani. Kuanzia dada zao wakubwa hadi kwa mtoto wa mwisho ambae ndio huyu binti ambae ndio lengo la huu uzi.
Kaka zake na huyo mrembo ni rika langu na tunaheshimiana sana. Nimekuwa nikienda kwao mara kwa mara lakini nilijikuta tu naanza kuvutiwa na mdogo wao. Sikuwaambia chochote na siwezi kuwaambia sababu najua hiyo inaweza kuwa chanzo cha kuvunjika kwa heshima tuliyoijenga kwa muda mrefu. Hivyo basi, nilipanga nitamuwinda mdogo wao pasipo wao kujua lolote.
Basi, katika kwenda kwao mara kwa mara, nilianza tu kuonyesha ishara za namna tofauti kwa binti kuonyesha kuwa nina jambo nae japo kwa kuibia sana isije kugundulika mambo yakaenda kombo. Jumamosi ya wiki jana nikiwa kwenye mizunguko ya kawaida tu, nilibahatika kukutana nae akiwa na rafiki yake. Kwanza sikuwa nimemuona, nilisikia naitwa tu, kugeuka sauti inapotokea nikakuta ni yeye. Moyo ulipasuka kwakuwa ni kweli binti nilikuwa nishaanza kumpenda. Nikamfuata tukajuliana hali pamoja na huyo rafiki yake. Akadai ameagizwa sehemu na mama yake hivyo ana haraka kidogo, kwahiyo nikachukua mawasiliano yake tu tukaachana..
Nilianza kumchatisha muda uleule, tukachat vingi ila alichonisisitiza ni kwamba sipaswi kuwaambia kaka zake kama ninawasiliana nae. Nikamwambia wala hilo halina shida, kisha nikamuomba appointment, akasema sawa. Ataangalia muda ataniambia. Muda wote huo sikuwa nimeingiza vocal, nilikuwa naisikilizia beat kwanza ili nijue naingiaje.. maana nilikuwa nasoma tu uelekeo kwanza ili nisije kuingiza vocal za blues wakati beat ni la Amapiano..
Kesho yake ambayo ilikuwa ni jumapili aliniambia jioni atakuwa na muda, nikawaza tu eneo tulivu la kumpeleka ambapo kaka zake hawatoweza kufika kwa urahisi. Jioni yake tukakutana kwenye eneo tulivu tu, tukaongea sana ndio nikapata wasaa wa kumtongoza. Haikuwa ngumu kwangu kama nilivyokuwa nikiwaza. Rasmi mrembo akasaini..
Nilifurahi sana, muda ukasogea hadi kagiza kakaingia. Nikampiga mate, akakubali. Nikajua tayari mhuri umegongwa kwenye mkataba aliosaini. Sasa ni mali yangu halali. Nikampa hela ya boda akarudi home.
Wiki hiyohiyo nikapata nafasi ya kukutana nae mara mbili na kupata uhondo kimya kimya, nilihakikisha hakuna atakaejua kati ya wale kaka zake. Aisee nina kila sababu ya kumsifia huyu mtoto.. kuanzia rangi, sura, shape na kila kitu chake..
Katika kukutana huko, nilipata wasaa wa kumpiga picha nyingi sana. Alinisisitiza tena zisionekane kwa kaka zake, hatamani kabisa iwe hivyo kwakuwa ananipenda sana, ikijulikana uhusiano utaharibiwa nikampa uhakika.
***************
Kuna rafiki yangu mwingine tofauti kabisa na kaka zake demu, ni mwanangu kitambo sana. Kutokana na majukumu mbalimbali tumekuwa tukikutana mara nyingi weekends tu. Jana nikiwa nae sehemu tumekaa aliniomba simu mara moja. Katika kupekua akakutana na picha za yule binti.. Ghafla nikaona kama jamaa kapaniki, ikabidi aniulize huyu demu unamjua? Nikamwambia ndio namjua. Akaniambia ni nani yako? Mie kimasikhara nikamwambia mbona picha zinajieleza kaka.. aisee jamaa mood yote ikakata kabisa. Akawa ananiambia huyu ni demu wangu kitambo sana.. nikawa siamini, ikabidi anionyeshe chatting zake na demu na picha alizokuwa nazo. Kuona haitoshi akampigia na simu kabisa kuthibitisha. Kweli aisee wakaongea kisha jamaa akakata simu.. Nilichoka hata mimi, binti ninaempenda kumbe tena na jamaa yangu anaishi hapo. Ikabidi nimwambie jamaa, mie sina muda sana tangu niingie nae kwenye mahusiano na wala sijawahi kukueleza kama nina mwanamke mwingine. Kibaya zaidi nawewe kwa muda wote huo hukuwahi hata kuniambia wala kunionyesha kama huyu ni mwanamke wako.. Jamaa hadi analia kabisa, nikaona hii ni serious kumbe.
Nilichomwambia jamaa ni kuwa mie nipo tayari kumpotezea kwakuwa wewe ulikuwa nae tangu zamani ili upate kuendelea nae wewe.. Lakini kiufupi binti nampenda zaidi ya sana na mimi sijui naamua vipi hapa. Kibaya zaidi binti kanipigia simu usiku wa jana wakati wa kulala, na leo asubuhi sana kujua nimeamkaje, so romantic call na inaonyesha kabisa hakuna anachojua hadi sasa.
Ushauri wenu tafadhali. Naamuaje hapa ili nisiumie? I love her deeply for sure
Kuna jamaa zangu wawili mapacha wanyaturu huwa wana mdogo wao wa kike, ni mrembo Pro Max. Katika ile familia, naweza kumpa credit mama yao kwa kufyatua watoto wazuri kupita maelezo pale mtaani. Kuanzia dada zao wakubwa hadi kwa mtoto wa mwisho ambae ndio huyu binti ambae ndio lengo la huu uzi.
Kaka zake na huyo mrembo ni rika langu na tunaheshimiana sana. Nimekuwa nikienda kwao mara kwa mara lakini nilijikuta tu naanza kuvutiwa na mdogo wao. Sikuwaambia chochote na siwezi kuwaambia sababu najua hiyo inaweza kuwa chanzo cha kuvunjika kwa heshima tuliyoijenga kwa muda mrefu. Hivyo basi, nilipanga nitamuwinda mdogo wao pasipo wao kujua lolote.
Basi, katika kwenda kwao mara kwa mara, nilianza tu kuonyesha ishara za namna tofauti kwa binti kuonyesha kuwa nina jambo nae japo kwa kuibia sana isije kugundulika mambo yakaenda kombo. Jumamosi ya wiki jana nikiwa kwenye mizunguko ya kawaida tu, nilibahatika kukutana nae akiwa na rafiki yake. Kwanza sikuwa nimemuona, nilisikia naitwa tu, kugeuka sauti inapotokea nikakuta ni yeye. Moyo ulipasuka kwakuwa ni kweli binti nilikuwa nishaanza kumpenda. Nikamfuata tukajuliana hali pamoja na huyo rafiki yake. Akadai ameagizwa sehemu na mama yake hivyo ana haraka kidogo, kwahiyo nikachukua mawasiliano yake tu tukaachana..
Nilianza kumchatisha muda uleule, tukachat vingi ila alichonisisitiza ni kwamba sipaswi kuwaambia kaka zake kama ninawasiliana nae. Nikamwambia wala hilo halina shida, kisha nikamuomba appointment, akasema sawa. Ataangalia muda ataniambia. Muda wote huo sikuwa nimeingiza vocal, nilikuwa naisikilizia beat kwanza ili nijue naingiaje.. maana nilikuwa nasoma tu uelekeo kwanza ili nisije kuingiza vocal za blues wakati beat ni la Amapiano..
Kesho yake ambayo ilikuwa ni jumapili aliniambia jioni atakuwa na muda, nikawaza tu eneo tulivu la kumpeleka ambapo kaka zake hawatoweza kufika kwa urahisi. Jioni yake tukakutana kwenye eneo tulivu tu, tukaongea sana ndio nikapata wasaa wa kumtongoza. Haikuwa ngumu kwangu kama nilivyokuwa nikiwaza. Rasmi mrembo akasaini..
Nilifurahi sana, muda ukasogea hadi kagiza kakaingia. Nikampiga mate, akakubali. Nikajua tayari mhuri umegongwa kwenye mkataba aliosaini. Sasa ni mali yangu halali. Nikampa hela ya boda akarudi home.
Wiki hiyohiyo nikapata nafasi ya kukutana nae mara mbili na kupata uhondo kimya kimya, nilihakikisha hakuna atakaejua kati ya wale kaka zake. Aisee nina kila sababu ya kumsifia huyu mtoto.. kuanzia rangi, sura, shape na kila kitu chake..
Katika kukutana huko, nilipata wasaa wa kumpiga picha nyingi sana. Alinisisitiza tena zisionekane kwa kaka zake, hatamani kabisa iwe hivyo kwakuwa ananipenda sana, ikijulikana uhusiano utaharibiwa nikampa uhakika.
***************
Kuna rafiki yangu mwingine tofauti kabisa na kaka zake demu, ni mwanangu kitambo sana. Kutokana na majukumu mbalimbali tumekuwa tukikutana mara nyingi weekends tu. Jana nikiwa nae sehemu tumekaa aliniomba simu mara moja. Katika kupekua akakutana na picha za yule binti.. Ghafla nikaona kama jamaa kapaniki, ikabidi aniulize huyu demu unamjua? Nikamwambia ndio namjua. Akaniambia ni nani yako? Mie kimasikhara nikamwambia mbona picha zinajieleza kaka.. aisee jamaa mood yote ikakata kabisa. Akawa ananiambia huyu ni demu wangu kitambo sana.. nikawa siamini, ikabidi anionyeshe chatting zake na demu na picha alizokuwa nazo. Kuona haitoshi akampigia na simu kabisa kuthibitisha. Kweli aisee wakaongea kisha jamaa akakata simu.. Nilichoka hata mimi, binti ninaempenda kumbe tena na jamaa yangu anaishi hapo. Ikabidi nimwambie jamaa, mie sina muda sana tangu niingie nae kwenye mahusiano na wala sijawahi kukueleza kama nina mwanamke mwingine. Kibaya zaidi nawewe kwa muda wote huo hukuwahi hata kuniambia wala kunionyesha kama huyu ni mwanamke wako.. Jamaa hadi analia kabisa, nikaona hii ni serious kumbe.
Nilichomwambia jamaa ni kuwa mie nipo tayari kumpotezea kwakuwa wewe ulikuwa nae tangu zamani ili upate kuendelea nae wewe.. Lakini kiufupi binti nampenda zaidi ya sana na mimi sijui naamua vipi hapa. Kibaya zaidi binti kanipigia simu usiku wa jana wakati wa kulala, na leo asubuhi sana kujua nimeamkaje, so romantic call na inaonyesha kabisa hakuna anachojua hadi sasa.
Ushauri wenu tafadhali. Naamuaje hapa ili nisiumie? I love her deeply for sure