Nimechanganyikiwa !!!

Pole dada, nenda kapime hata kama umeambukizwa what you need ni kutulia na kufuata masherti ya wataalamu kwani ukimwi sio kifo wangapi wanao wanishi up to 20 years, lakini wasiokuwa nao wanakufa na vifo vingine. Kisukari sasa hivi ndo kinafuatia baada ya malaria na ukimwi unakuja nafasi ya tatu lakini wenye kisukari wala hawaogopi na wala dawa zao haziitwi dawa za kuongeza maisha.

Usiogope nenda kapime ujijue na ubadili tabia. Huyo mtu ni mshenzi sana wanasambaza makusudi watu wa aina yake.
 
Pole sana Della. Kama wengi walivyokushauri, nenda kwanza ukapime ujue status ya afya yako na hata kama umeathirika ujue sio mwisho wa maisha!Wapo watu wengi sana ambao wameathirika na wanaishi kama watu wengine!Usikate tamaa kabisa, muombe Mungu wako naye kamwe hatokuacha.
 
pole mwayego, si vizuri kukata tamaa ya maisha kwani wewe bado unahitajika kujenga taifa letu, sio vibaya ukaenda kupima ili ujue uishi maisha ya namna gani!! Ni hayo tu.
 
Ardhi yenye afya imebeba watu wadhaifu.... Na watu dhaifu wamebeba utukufu.... Bora ukapime, uwe huru.... Nenda kapime ujue uwe huru..!!! Shija alipopima alijisihi katua mzigo mkubwa sana Ingawa alikutwa navyo...!!! Kapime dada HIV siyo mwisho wa maisha! Pointi ya msingi, usitumie hasira za kutendwa kumkomoa mtu, utakua unajidhuru mwenyewe..! "UKIkuingia MWIlini" ni sehemu ya matatizo ya taifa letu kama ufisadi tu
 
Pole sana kwa hayo yote; kwa kifupi ni kwamba umechanganyikiwa kwasababu umejua kinachoendelea. Ni vema ujue kwamba kuna wengi wa aina yako isipokuwa hawajapata kujua kinachoendelea hence they are happy with their life. Ni vizuri ujue kuwa HIV feeds on our ignorance na sio ugonjwa wa kutisha kama watu tunavyoubeba. Na pia siyo kweli kwamba sex without condom is always lead to HIV infection....hiyo iko kitaalamu zaidi, so nenda ukapime maana nahisi unadevelop pressure na siyo HIV.
 
kama walivyokushaur nami pia nakushaur nenda kapime ili ujijue then mengine yatafuta nahicho kibwana kaanacho mbali xana
 
Nawashukuru kwa kunipokea katika JF.
Naamini kabisa ni mahali pa watu kupata msaada wa kimawazo,n.k.Nilikuwa natafuta ni wapi pa kusemea ,naona labda nianzie hapa naombeni ushauri.. sijui nianzeje.

Mimi nina mtoto mmoja.namtaunza mwenyewe tu kwa kila kitu, baba yake yupo ila anajifanya kama haoni na ana uwezo ,na mara ingine akikutana na marafiki zake anaanza kujisifia ..kwangu sioni tatizo ila niliamua baada ya kukaa muda mrefu sina mtu wa karibu wa kuongea nae nikapata boyfriend,mimi kwa kweli sielewi huyu (naweza kusema sio type yangu)sijui kanitokea wapi? najiuliza,Approach yake,utanashati kwa kweli nikaona nimepata mtu na anaongea kwa busara,
Nimekuwa na uhusiano nae kwa muda wa miezi kama 3 tu ila nimegundua tabia na mwenendo wake si mzuri hata kidogo,makucha yake yalianza kujitokeza pale nilipogundua ana mke anaishi nae,mke alinipigia na kuniambia tuonane mimi ni mke wa jamaa.Jamaa akanikatalia sana nisionane na mkewe nimegundua pia kwamba kwa mkewe yeye amejiweka ni mlokole pai amebadilisha kabila ,simjui ndugu yake hata mmoja ila ni marafiki tu .Jamani najuta mimi!!!
watu husema za mwizi ni arubaini ,tabia ingine ya huyu jamaa ni dhuluma sasa kaenda kumdhulumu mke wa mtu mwingine ndio yakaja mambo yote ya huyu jamani ni kwamba ameathirika siku nyingi sana! kuna mwanamke alifiwa na mume yeye alikuwa anatembea nae maana anapenda sana dezzo.haikutosha yupo mwingine amefariki mwisho wa mwezi wa tatu 2008 nae alizaa nae mtoto alifikisha umri wa 8 months.akafariki,(sio kwamb natunga jamani ni ya kweli na aliesimulia ni rafiki yake mpenzi na one of the inlaws wa huyu mwanamke aliefariki mwisho wa mwezi wa tatu),nilijiona mdogo kama piriton nilihisi kama moyo umeruka mapigo yake ,sio hayo tuu hapo anapoishi jamaa an mwanamke mwenye mtoto mchanga wa umri wa miezi 4,pia ametelekeza mke na watoto 4 wanateseka kweli,jamaa anchukua watoto wa shule tena wachafu wachafu akiwahonga sana ni 500.00!!akishavuruga anakutema anachukua mwengine ,jamani nimfanyeje ?sasa iv anaishi kam digidigi, kwa kuniogopa labda nitamshataki au chochote, anavyodai,mimi jamani ntaenda wapi nahisi nimeukwaa ntawaambiaje ndugu zangu??wazazi je? jamii ndio kabisa sijui nitaitazamaje ..nisaidieni naogopa kwenda kupima maana mpaka sasa sio siri naona mapigo ya moyo yanasimama kila saa.kazi naharibu,siwezi hata kula ,,jamani naombeni uashauri wenu, Najuta mimi.

Pole sana my dear,Mungu yuko upande wako.Nina rafiki yangu alikuwa anaishi na mume wake wa ndoa,ila mume alikuwa hajatulia,mume akaukwaa akaugua sana,mke akashauri wapime jamaa akagoma,mke akaenda kupima akakuta negative,mume akaona yes tuko safi,ndio akapata nguvu ya kwenda kupima ila bila kumwambia mkewe,looh akajikuta positive akapanic sana na akawa mpole sana kwa mkewe,mke akapima 3 times yuko fit,jamaa akahamua kuwa anaambukiza makusudi na akamwambia mkewe kama kweli huna virus hongera na naomba ulee watoto vizuri mimi naendelea kuwarudishie wanawake virusi vyao,kawa malaya wa kutupwa,na rafiki angu alimkimbia maana alikuwa akija amelewa anataka wa du bila condom.
FUNDISHO
Sio lazima ukitembea na mwenye virusi basi utaupata na wewe,big no,nenda kujipime na upate ushauri kwanza.Rafiki angu alifanyiwa canseling na aliendele kusex na mumewe kwa condom,yani unashauriwa unapewa na mifano hai mpaka unaona ni normal tu,yani mi nilikuwa namshangaa kweli best anasex na mwadhirika,ila anaupendo sana na adabu nafikiri ndio maana Mungu alimnusuru,looh kama sio kutaka kubakwa na mumewe nahisi wangekuwa wanaendelea,ana two years sasa tangu waachane na hana virusi,sema jamaa anachapa balaa,nahisi wanafunzi wa IFM wameshapigana sana juu yake ila hawajui ni mgonjwa,poor ladies.Kapime shost virusi sio mwisho wa maisha,ila achana nae kabisa maana sio mume wako na sio mwaminifu.
 
Pole sana...kwanza tambua kuwa hayo yote ni majaribu tu, na huwa yanakuja na kuisha vilevile. Pia tambua kwamba hauko peke yako katika majaribu, kuna matatizo mbalimbali mengi tu na makubwa ambayo binadamu huyapata lakini kumbuka kuna siku yataisha tu.
Tulia tu na uendelee na shuguli zako kama kawaida ili utulize akili yako, halafu jaribu kupanga kuanza maisha mapya na baada ya muda kidogo ukisha tulia ni vizuri kwenda kucheki afya...am sure majibu yoyote utakayoyapata uwezo wa kuyapokea utakua nao kwa sababu ushaamua kuishi maisha mapya! ila naamini hauna ngoma na mambo yako yataenda vizuri ile mbaya.
 
Pole sana...kwanza tambua kuwa hayo yote ni majaribu tu, na huwa yanakuja na kuisha vilevile. Pia tambua kwamba hauko peke yako katika majaribu, kuna matatizo mbalimbali mengi tu na makubwa ambayo binadamu huyapata lakini kumbuka kuna siku yataisha tu.
Tulia tu na uendelee na shuguli zako kama kawaida ili utulize akili yako, halafu jaribu kupanga kuanza maisha mapya na baada ya muda kidogo ukisha tulia ni vizuri kwenda kucheki afya...am sure majibu yoyote utakayoyapata uwezo wa kuyapokea utakua nao kwa sababu ushaamua kuishi maisha mapya! ila naamini hauna ngoma na mambo yako yataenda vizuri ile mbaya.

kiongozi?avatar yako ni picha ya kitu gani?ninachokiona ndio chenyewe au macho yangu?
 
Daah ila pipo ndo tujifunze pindi 2napoanzisha mahusiano mapya kwa ulimwengu wa leo bora mpime mapeeeema othrwize kinga ndo iwe mpango mzima cz kwa hii case ya bidada hapa wangekuwa wamepima frm the beginin or wangekuwa wana2mia kinga hata asingekuwa na hizi stress alizonazo hapa bt anyway pole nyingi mwaya,kapime ili uwe na amani otherwize hofu will kill you softly kwakwel
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom