Nimeamua kusimamisha masomo ya PhD nje ya nchi ili nijitayarishe kwaajili ya kugombea ubunge 2025 katika jimbo la Mbozi Mashariki

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,331
8,254
Habari za leo watanzania wenzangu,

Mimi rafiki yenu na kijana mwenzenu nilishafungua moyo wangu kuwatumikia watanzania katika kiti cha ubunge. Kama kuna wabunge humu naomba watanishauri zaidi ila ni jambo ambalo nalipenda na nina uzoefu nalo kidogo.

Muda wangu sahihi wa kujitokeza hadharani utakua 2025 ila bado sijaweka wazi nitagombea ubunge kupitia chama gani.

Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya nisitishe masomo yangu haraka sana ili niweze kujipanga katika hili. Nilipata kuchaguliwa kuendelea na masomo ya PhD katika chuo kimoja huko nje ya nchi. Ilinipasa mwezi wa tisa mwaka jana niwe nimeshaingia chuoni na kuanza masomo yangu.

Naombeni kuungwa mkono katika hili. Najua muda ukiwadia ipo siku nitamalizia elimu yangu. Lakini kwasasa nijapange ili kutimiza adhima yangu.

Ahsanteni jamani.

VISA2.JPG


VISA.JPG
 
Hatuna Jimbo linaloitwa Mbozi mashariki katika mkoa wa Songwe, masuala ya Mbozi mashariki na magharibi yalikwishaga na kuishia kwa akina Zambi na Silinde, ambapo Jimbo la Mbozi mashariki lilitoa Jimbo la Mbozi linaloongozwa kwa Sasa na mh GEORGE RAINWELL MWENISONGOLE pamoja na Jimbo la Vwawa linaloongozwa na mh Hasunga, wakati Mbozi magharibi lilitoa majimbo ya Tunduma ambalo kwa Sasa linaongozwa na mh Silinde, pamoja na la Momba.

Kutokujua tu majimbo katika eneo unapokwenda kugombea kunakuondolea sifa ya kupewa nafasi ya kugombea maana Kama hata majimbo huyajuwi bila Shaka hata kero za wananchi huwezi ukazijua iwe Ni kata ya Mlowo, Igamba, Shiwinga, Mahenje, Itaka, Bara, Nambizo, Magamba,n.k

Hata hivyo majimbo Yana watu tayari na kwa kanuni zetu wanaccm hupaswi kuanza vurugu za kampeni wakati huu bali unapaswa kumsaidia aliyopo labda Kama unagombea kupitia huko kwa wababaishaji wa chadema wasio na Sera Wala ajenda Wala Dira.

Pia kutokujuwa hata chama Cha kugombea pia huo Ni ubabaishaji mwingine maana huo Ni usaka tonge tu na kuangalia mahali kwenye fursa badala ya kuangalia itikadi ya chama.

Ushauri Wangu Ni kuwa Kama unataka kugombea kupitia chama changu Cha CCM nakushauri ungeendelea tu na masomo yako maana naona upo bado Sana kuiva kisiasa na badala yake ungejikita katika fani yako ya mafuta ili ulisaidie Taifa kuliko kuja kupoteza muda wako wakati hadi Sasa hujui hata chama kipi ugombee na Wala huna chama, Sasa Kama huna chama Ni mjinga gani atakupigia Kura wakati anaona wewe Ni msaka fursa?

Pili lazima uwe na misimamo katika maisha maana mpaka Sasa haieleweki unasimamia Nini na unataka Nini, pia wapiga kura ambao Ni wajumbe Ni waelewa Sana kwa Sasa hivyo usije kujipa majibu yako ya kubuni.
 
Hatuna Jimbo linaloitwa Mbozi mashariki katika mkoa wa Songwe,masuala ya Mbozi mashariki na magharibi yalikwishaga na kuishia kwa akina Zambia na silinde,ambapo Jimbo la Mbozi mashariki lilitoa Jimbo la Mbozi linaloongozwa kwa Sasa na mh GEORGE RAINWELL MWENISONGOLE ,Pamoja na Jimbo la Vwawa linaloongozwa na mh Hasunga, wakati Mbozi maghalibi lilitoa majimbo ya Tunduma ambalo kwa Sasa linaongozwa na mh silinde, pamoja na la Momba.

Kutokujuwa tu majimbo katika eneo unapokwenda kugombea kunakuondolea sifa ya kupewa nafasi ya kugombea maana Kama hata majimbo huyajuwa bila Shaka hata kero za wananchi huwezi ukazijuwa iwe Ni kata ya mlowo,igamba,shiwinga, mahenje,itaka,Bara,nambizo,magamba,n.k

Hata hivyo majimbo Yana watu tayari na kwa kanuni zetu wanaccm hupaswi kuanza vurugu za kampeni wakati huu bali unapaswa kumsaidia aliyopo labda Kama unagombea kupitia huko kwa wababaishaji wa chadema wasio na Sera Wala ajenda Wala Dira.

Pia kutokujuwa hata chama Cha kugombea pia huo Ni ubabaishaji mwingine maana huo Ni usaka tonge tu na kuangalia mahali kwenye fursa badala ya kuangalia itikadi ya chama.

Ushauri Wangu Ni kuwa Kama unataka kugombea kupitia chama changu Cha ccm nakushauri unaendelea tu na masomo yako maana naona upo bado Sana kuiva kisiasa na badala take ungejikita katika fani yako ya mafuta ili ulisaidiebTaifa kuliko kuja kupoteza muda wako wakati Hadi Sasa hujuwi hata chama kipi ugombee na Wala huna chama,Sasa Kama huna chama Ni mjinga gani atakupigia Kura wakati anaona wewe Ni msaka fursa?

Pili lazima uwe na misimamo katika maisha maana mpaka Sasa haieleweki unasimamia Nini na unataka Nini,pia wapiga kura ambao Ni wajumbe Ni waelewa Sana kwa Sasa hivyo usije kujipa majibu yako ya kubuni
Ahsante sana kwa ushauri mzuri. Ushauri huu nitaanza kuufanyia kazi kwa uharaka sana rafiki.
 
Hatuna Jimbo linaloitwa Mbozi mashariki katika mkoa wa Songwe,masuala ya Mbozi mashariki na magharibi yalikwishaga na kuishia kwa akina Zambia na silinde,ambapo Jimbo la Mbozi mashariki lilitoa Jimbo la Mbozi linaloongozwa kwa Sasa na mh GEORGE RAINWELL MWENISONGOLE ,Pamoja na Jimbo la Vwawa linaloongozwa na mh Hasunga, wakati Mbozi maghalibi lilitoa majimbo ya Tunduma ambalo kwa Sasa linaongozwa na mh silinde, pamoja na la Momba.

Kutokujuwa tu majimbo katika eneo unapokwenda kugombea kunakuondolea sifa ya kupewa nafasi ya kugombea maana Kama hata majimbo huyajuwa bila Shaka hata kero za wananchi huwezi ukazijuwa iwe Ni kata ya mlowo,igamba,shiwinga, mahenje,itaka,Bara,nambizo,magamba,n.k

Hata hivyo majimbo Yana watu tayari na kwa kanuni zetu wanaccm hupaswi kuanza vurugu za kampeni wakati huu bali unapaswa kumsaidia aliyopo labda Kama unagombea kupitia huko kwa wababaishaji wa chadema wasio na Sera Wala ajenda Wala Dira.

Pia kutokujuwa hata chama Cha kugombea pia huo Ni ubabaishaji mwingine maana huo Ni usaka tonge tu na kuangalia mahali kwenye fursa badala ya kuangalia itikadi ya chama.

Ushauri Wangu Ni kuwa Kama unataka kugombea kupitia chama changu Cha ccm nakushauri unaendelea tu na masomo yako maana naona upo bado Sana kuiva kisiasa na badala take ungejikita katika fani yako ya mafuta ili ulisaidiebTaifa kuliko kuja kupoteza muda wako wakati Hadi Sasa hujuwi hata chama kipi ugombee na Wala huna chama,Sasa Kama huna chama Ni mjinga gani atakupigia Kura wakati anaona wewe Ni msaka fursa?

Pili lazima uwe na misimamo katika maisha maana mpaka Sasa haieleweki unasimamia Nini na unataka Nini,pia wapiga kura ambao Ni wajumbe Ni waelewa Sana kwa Sasa hivyo usije kujipa majibu yako ya kubuni
Lucas mwashambwa
😇😇😇

Erythrocyte amenukuliwa akisema jamaa hapo juu hajalamba uteuzi........
 
Ulifanya homework yako vizuri lakini mkuu? Usije ukaikumbuka hii nafasi uliyoiacha ya kumaliza PHD.

Ubunge una mambo mengi Sana. Sio kitu rahisi Sana, unaweza kuwa na uwezo wa kuwa mbunge ila siasa zikakukataa plus wajumbe.

Hata hivyo unaweza kuwatumikia Wa Tanzania kwa namna nyingi zaidi ya kuwa Mbunge, na kusema kweli kabisa kwa nature ya bunge letu, huwatumikii waTanzania kwa kuwa mbunge, unaitumikia Serekali na kukinufaisha Chama chako.

Sema ubunge una maslahi. Kama hii ndio target yako well and good.
 
Habari za leo watanzania wenzangu,

Mimi rafiki yenu na kijana mwenzenu nilishafungua moyo wangu kuwatumikia watanzania katika kiti cha ubunge. Kama kuna wabunge humu naomba watanishauri zaidi ila ni jambo ambalo nalipenda na nina uzoefu nalo kidogo.

Muda wangu sahihi wakujitokeza hadharani utakua 2025 ila bado sijaweka wazi nitagombea ubunge kupitia chama gani.

Hii ndio sababu kubwa iliyonifanya nisitishe masomo yangu haraka sana ili niweze kujipanga katika hili. Nilipata kuchaguliwa kuendelea na masomo ya PhD katika chuo kimoja huko nje ya nchi. Ilinipasa mwezi wa tisa mwaka jana niwe nimeshaingia chuoni na kuanza masomo yangu.

Naombeni kuungwa mkono katika hili. Najua muda ukiwadia ipo siku nitamalizia elimu yangu. Lakini kwasasa nijapange ili kutimiza adhima yangu.

Ahsanteni jamani.

View attachment 2495736

View attachment 2495735
Umejipanga kwa masuala ya uganga na uchawi. Siasa ya Tanzania inategemea pesa na uwezo wako wa kuroga.
Angalau wakati wa Magufuli hakukuwa na uwezekano wa kupata Ubunge kwa pesa na ndumba ila kwa sasa tumerudi siasa za awamu ya nne. Wewe unadhani yule Mbunge alikuwa anaweza kumng'oa Chenge, hapana!
alipita kwa msuli wa Magufuli!

Ungeomba ushauri mapema, tungekushauri uende shule kuliko kugombea nafasi ambayo sharti ujue kusoma na kuandika!
 
Back
Top Bottom