Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 67,119
- 173,952
Ugomvi usio na maana ni lack of maturityNatumai hamjambo wakuu.
Jana nikiwa nimerejea toka kazini tukawa tunapiga stori na wife aliniuliza "hivi mume tumewezaje kumaliza wiki ya 3 sasa bila kukwazana? wakati mara nyingi hata wiki hua hatumalizi? nikamuuliza umemiss kukwazana?
Akajibu hapana but nimeshangazwa na hili coz huko nyuma japo huwa tunaweka maazimio yakutokwazana na kujitahidi kujizuia but hutokea tu tena ndani ya mda mfupi" tukacheka kidogo then nikamwambia kukwazana pia ni sehemu ya maisha.
Sasa wakuu nachojiuliza je kwa nini ni ngumu sana kujizuia na kukwazana katika ndoa/mahusiano na unapopita mda mrefu kidogo bila kukwazana kila mtu hushangazwa na hali hiyo?