Jerry001
Member
- Apr 29, 2020
- 21
- 57
Wazee wa jukwaa nawasalimu.
Sitosahau kisa hiki kilichonikuta skonga miaka ya 2003 wakati nipo sekondari moja huko nyanda za juu kusini.
Ilikuwa Ijumaa mishale ya saa 2 usiku, ambapo mimi na jamaa zangu watukutu tulikuwa tunajiandaa na paper za NECTA tukaona sio mbaya twende kijiji jirani kutafuta bangi kama kawaida yetu.
Tulikuwa na kundi letu la watukutu, yaani masela uchwala ila wazee wa kukesha na kupopoa msuli mpaka majogoo.
Sasa hiyo siku tukatoka mimi, wanangu Chino, Buga na Chopa haaoo mpaka karibu na kilabu kimoja cha gongo ambapo ndio pusha wetu ilikuwa maskani yake.
Kufika pale hatukumkuta, tukaelekezwa kuwa atakuwa kwenye disko vumbi ambapo sio mbali sana na pale.
Tukaona fresh ngoja tutimbe mpaka eneo husika, wakati huo Chino na Buga walishanunua sigara kali wakipiga pafu mdogo mdogo.
Kufika disko vumbi, Chopa akatinga ndani kumtafuta pusha, wakati huo mimi na jamaa wengine tupo nje tunasikilizia. Zikapita kama dakika 10 Chopa hajarudi, ikabidi mimi niende kumfuatilia ili kujua nini tatizo.
Kuingia ndani, moja kwa moja nikatimba mpaka kwa msaidizi wa dj nikamuuliza kama amemuona pusha. Yule jamaa akanijibu kifupi kuwa hayupo. Nikamuuliza tena kama alikuwepo pande zile akasema hajamuona. Nikamuona jamaa chenga. Kumcheki vizuri kumbe jicho nyanya, hivyo hatuelewani.
Kurudi nje sikumkuta Chino wala Buga. Nikaanza kuwafuatilia walipoenda, nikajua tu watakuwa wamerudi kule kilabuni kwa mwanzo na Chopa.
Nikachukua njia moja kwa moja mpaka kilabuni. Cha kushangaza sikuwakuta ila nilimkuta Chopa ambaye alidai ametutafuta sana maana baada ya kumpata pusha alidai mzigo kauacha maskani kwake. Tukaona sio shida tukanunua bangi ya mia tano hao tukasepa mdogo mdogo kurudi disko vumbi kuwatafuta Chino na Buga.
Tukiwa njiani tukasokota vijiti viwili vya msuba tukawasha nyasi na kula moshi mdogo mdogo kisha kuucheulia puani kama gari moshi. Basi baada ya kuvuta pafu kama nne za haja nikaanza kusikia kichwa kizito na njaa kiasi. Kadri muda ulivyoenda nikaanza kusikia njaa kali na kichwa kizito kama nimebeba zile ndoo za maji za chuma (wahenga mnazimanya fresh).
Kwa mbali nikawaona Chino na Buga, ila cha ajabu walikuwa wamebadilisha nguo. Chino amevaa koti kama la daktari na Buga koti kama la fundi makenika. Nikafikicha macho kuona kama yananidanganya sababu ya bangi au ndivyo ilivyo. Kuangalia vizuri kumbe Chino kavaa vazi la wauza bucha maana lilikuwa na damu damu kiasi.
Kuwafikia, nikasikia Chopa anawauliza walikuwa wapi, ndipo Buga akajibu walifuata vifaa vya kazi.Wakati huo mdomo wangu umekuwa mzito mbaya siwezi hata kuunyanyua kuongea chochote ukizingatia na ile njaa kali iliyonikumba ghafla.
Sijakaa sawa nikasikia Buga anamuuliza Chopa kama kazi waliyompatia ameshaifanya. Chopa akatikisa kichwa kama kuwapa ishara fulani. Basi tukawa tunaongozana kwenda njia panda ya kuelekea shule. Kufika mbele karibu na vichaka vya mianzi Chopa akawaambia tuingie pori kumalizia Bangi aliyokuwa nayo. Hapo ndio machale yakanicheza
itaendelea...
Sitosahau kisa hiki kilichonikuta skonga miaka ya 2003 wakati nipo sekondari moja huko nyanda za juu kusini.
Ilikuwa Ijumaa mishale ya saa 2 usiku, ambapo mimi na jamaa zangu watukutu tulikuwa tunajiandaa na paper za NECTA tukaona sio mbaya twende kijiji jirani kutafuta bangi kama kawaida yetu.
Tulikuwa na kundi letu la watukutu, yaani masela uchwala ila wazee wa kukesha na kupopoa msuli mpaka majogoo.
Sasa hiyo siku tukatoka mimi, wanangu Chino, Buga na Chopa haaoo mpaka karibu na kilabu kimoja cha gongo ambapo ndio pusha wetu ilikuwa maskani yake.
Kufika pale hatukumkuta, tukaelekezwa kuwa atakuwa kwenye disko vumbi ambapo sio mbali sana na pale.
Tukaona fresh ngoja tutimbe mpaka eneo husika, wakati huo Chino na Buga walishanunua sigara kali wakipiga pafu mdogo mdogo.
Kufika disko vumbi, Chopa akatinga ndani kumtafuta pusha, wakati huo mimi na jamaa wengine tupo nje tunasikilizia. Zikapita kama dakika 10 Chopa hajarudi, ikabidi mimi niende kumfuatilia ili kujua nini tatizo.
Kuingia ndani, moja kwa moja nikatimba mpaka kwa msaidizi wa dj nikamuuliza kama amemuona pusha. Yule jamaa akanijibu kifupi kuwa hayupo. Nikamuuliza tena kama alikuwepo pande zile akasema hajamuona. Nikamuona jamaa chenga. Kumcheki vizuri kumbe jicho nyanya, hivyo hatuelewani.
Kurudi nje sikumkuta Chino wala Buga. Nikaanza kuwafuatilia walipoenda, nikajua tu watakuwa wamerudi kule kilabuni kwa mwanzo na Chopa.
Nikachukua njia moja kwa moja mpaka kilabuni. Cha kushangaza sikuwakuta ila nilimkuta Chopa ambaye alidai ametutafuta sana maana baada ya kumpata pusha alidai mzigo kauacha maskani kwake. Tukaona sio shida tukanunua bangi ya mia tano hao tukasepa mdogo mdogo kurudi disko vumbi kuwatafuta Chino na Buga.
Tukiwa njiani tukasokota vijiti viwili vya msuba tukawasha nyasi na kula moshi mdogo mdogo kisha kuucheulia puani kama gari moshi. Basi baada ya kuvuta pafu kama nne za haja nikaanza kusikia kichwa kizito na njaa kiasi. Kadri muda ulivyoenda nikaanza kusikia njaa kali na kichwa kizito kama nimebeba zile ndoo za maji za chuma (wahenga mnazimanya fresh).
Kwa mbali nikawaona Chino na Buga, ila cha ajabu walikuwa wamebadilisha nguo. Chino amevaa koti kama la daktari na Buga koti kama la fundi makenika. Nikafikicha macho kuona kama yananidanganya sababu ya bangi au ndivyo ilivyo. Kuangalia vizuri kumbe Chino kavaa vazi la wauza bucha maana lilikuwa na damu damu kiasi.
Kuwafikia, nikasikia Chopa anawauliza walikuwa wapi, ndipo Buga akajibu walifuata vifaa vya kazi.Wakati huo mdomo wangu umekuwa mzito mbaya siwezi hata kuunyanyua kuongea chochote ukizingatia na ile njaa kali iliyonikumba ghafla.
Sijakaa sawa nikasikia Buga anamuuliza Chopa kama kazi waliyompatia ameshaifanya. Chopa akatikisa kichwa kama kuwapa ishara fulani. Basi tukawa tunaongozana kwenda njia panda ya kuelekea shule. Kufika mbele karibu na vichaka vya mianzi Chopa akawaambia tuingie pori kumalizia Bangi aliyokuwa nayo. Hapo ndio machale yakanicheza
itaendelea...