St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,638
- 4,522
Kuna siku nilitokewa na ndoto nzuri na ya kupendeza.Usiku huo niliota nipo na msichana mrembo wa kuvutia ambaye kila kijana pale mtaani alikuwa akitamani kuwa naye.Na mimi katika ndoto hiyo nilimfaidi barabara,maana ilikuwa nikiamka na kujisafisha narudi tena kulala, naye anakuja tena na ndoto inaendelea na tuna do tena,hali hiyo ilijirudia mara tatu mpaka kulipokucha.Asubuhi yake nikajiona kuwa sitamtendea haki dada wa watu endapo sitamlipa ujira wake kwa kazi aliyonitendea ukizingatia kuwa mimi pia sipendi vya bure.Basi mtoto wa kiume nikatoka mpaka anapoishi yule dada na kutoa kitita cha noti na kumkabidhi,akaniuliza unanipa pesa ya nini?Nikamsimulia ndoto yangu,We!Nilikoma jinsi alivyonitoa mbio siku hiyo mpaka nikajiuliza kosa langu lilikuwa lipi?Kumlipa ujira wake?Kuota ninado naye?Au ujasiri wangu wa kwenda kumsimulia ndoto yangu.