Nilichojifunza Kenya: Madaktari Tanzania Mnaandika Dawa za Kiwango cha Chini

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,246
4,467
Kenya kuna makampuni mengi makubwa ya madawa, ambayo mengi yao ni innovators wa dawa mbalimbali (brands), ambazo nchi nyingine hususani India huja kuzalisha baadaye kama generic.

Kwa wasiojua brands huuzwa ghali, ila ni bora zaidi, wakati ni generic huuzwa kwa bei ya kutupwa, nyingi zikiwa na ubora unaopungua zaidi ya 80% ya brand yake.

Kampuni kubwa kama Novartis, Merck, Johnson & Johnson, Roche, Sanofi, Bristol Myers, Lilly, AstraZeneca, Gilead, Novo Nordisk, Bayer, GSK, Takeda n.k zote zipo kwenye soko la Kenya. Madaktari wa Kenya, wanaandika dawa kwa kutumia brands, tanzania wanatumia zaidi Generic.

Mwisho wa siku mtanzania atapata dawa za kiwango cha chini, hususani toka India na mara nyingi zitafanya kazi kwa kiwango duni na zimejaa maudhi lukuki. Najua kuna watu watapinga, ila ni sawa na kutumia Iphone au Samsung Galaxy vs Tecno Phantom.

Kuna mfamasia mwenzangu hapa Nairobi, aliniuliza kulikoni Tanzania mnauziwa dawa za kiwango duni za Kihindi? Mbona kampuni kubwa za madawa zinawakimbia? Nikamwambia sisi Tanzania kitu cha kwanza tunaangalia price, issue za quality sisi hatuzijui. Akaniuliza wewe uko radhi kutibiwa na Ceftriaxone ya kihindi inayouzwa Ksh 100, au kutibiwa na Rocephin, ambayo ni Ceftriaxone original iliyovumbuliwa na Roche, inayouzwa kwa KSh 1,500?

Nilimjibu ningetumia Rocephin. Akaniuliza mbona watanzania mnatumia zaidi dawa za kihindi kwa wagonjwa wenu? Sikuwa na jibu, maana mimi siandiki prescriptiom. Mimi natoa dawa iliyoandikwa na daktari.

Madaktari wa Tanzania, mjitafakari. Hayo mambo ya cheap cheap, kuna wakati wagonjwa wenu hawaponi.
 
ni kweli , ila sababu mojawapo ni upatikanaji wa hizo BRANDS , dealers wengi wa madawa ndio hao wanaoangalia price over quality, kuna brand unaandika mtu hapati famasi zote mji mzima mzima, unabidi ubadili tu achukue alternative, so hizo brands pia kama zingekuwa available dr angekuwa na machaguzi mengi, unakuta hata ma hospital makubwa bado vidawa ni poor hvyohvyo.
nadhani pia taasisi kama bima haziko tayari kulipia hizo BRANDS inawezekana ndio maana hata haziagizwi.
sababu ya pili ni umaskini wa watu, so hizo brands zikija hazitauzika so kibiashara wanaona mzunguko mdogo.
cha mwisho ni serikali yetu, wadhibiti ubora ni bure kabis, tungekuwa na standards zetu ingewashape mpaka na raia, sasa tuna mamlaka za udhibiti ikiwemo tbs, tmda lakn vidawa very low vinasambazwa nchini.

wa tz ni maskini wa kiuchumi ila viongozi wetu ni maskini ki fikra, weupe pee
 
Watanzania wengi wamefanywa maskini na mfumo wa utawala ambao unajali maslahi binafsi huku wakiwaamisha watanzania kwamba nchi yao ni maskini, hiki ndo alichokuwa anapambana nacho Magufuli kuwaondolea watanzania imani ya muda mrefu kwamba nchi yao ni maskini, yeye akisema wazi kabisa kwamba Tanzania ni nchi tajiri.

Kwa hiyo si ajabu kuona dawa za kiwango duni na bidhaa nyingine substandard zikiwa zimefurika kwenye soko la Tanzania huku kwa wenzetu hapo Kenya hali ikiwa ni tofauti kabisa......mostly ni kwamba umaskini wa watanzania umejengwa pia kwenye fikra na mfumo wa utawala uliokuja baada ya wazungu kuondoka.

Kwa nchi kama Kenya na hata Marekani ambazo ziliwakumbatia wakoloni waingereza baada ya kupata uhuru wao utaona hali ilivyo tofauti na kwetu hapa.​
 
watz ni maskini kupitiliza
Viongozi wanasababisha kwa makusudi ili wapate kututawala kirahisi milele maana mtu ukiwa lofa hata akili huwezi kuwa nazo ndiyo maana leo hii hata serikali inapotimiza wajibu wake wa kupeleka huduma kwa wananchi utasikia mazuzu wakimshukuru "mtu fulani" kwa kuwasaidia wakati ni haki yao na wala sio msaada uliotolewa na kenge yeyote.
 
Daktari anagawa dawa zilizopo sokoni, unanishangaza kulaumu daktari kwa hoja yako hii wakati umedai unafanya kazi sekta ya afya tena no Mtanzania. Daktari ndio anaaagiza dawa nje? Unawezaji kumlaumu mpishi wa shule kwanini hajapika pilau nyama wakati store kapewa unga dona na dagaa.

MSD kwa dawa za serikali wanatoa hizo generic. Kwa baadhi ya hospitali private ndio wanatoa mchanganyiko. Niliwahi pewa painkillers za Pfizer kwa shilingi laki moja wakati ningenunua za mitaani kina Panadol, Aspirin, Dawa Tatu zote hazizidi elfu tatu.
Zile Pfizer nilitumia ghafla maumivu ya mgongo yakaisha haraka sana, nilishangaa.
 
Mkuu naomb kujua tofauti kati brand na generic name maana nimegoogle hiyo Rocephin nikaandikiwa ceftriaxone ila wakaandika Rocephin is given in generic name sasa sijaelewa kwamba contents zao ndio tofauti au?
 
Back
Top Bottom