Elections 2010 Nikimpa Slaa kura yangu atatawala vipi?

Diana-DaboDiff

JF-Expert Member
Jul 13, 2009
376
19
Mimi Diana na watanzania wengi tunataka kumpa kura Dr. Slaa oct.2010 lakini najiuliza nikimpa atatawala vipi huku wabunge wengi watatoka CCM? sitaki kuichezea kura yangu na watu wengi wanajiuliza swali hili naomba watu wa Chadema watueleze tukimchagua atavunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine au atapitisha vipi miswada yake bungeni.Hii mbio ya kuingia ikulu cannot be an end by itself.
 
Kila kona maofisini na mitaani Dr.Slaa ndio gumzo,nilimpa kura yangu Mrema 95,Lipumba 2000,Mbowe 2005.Kwakifupi toka vyama vingi vianze CCM hawajapata kura yangu Chadema tutoeni gizani kuhusu suali hili ili tuweze kuwaelimisha na wengine.
 
nani alikuambia kuwa Chadema watapata wabunge wachache? wabunge watakuwa wengi na wasipotosha wataunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kujumuisha wabunge wa cuf na ccm.
Piga kura kwa Dk wa ukweli, hatudanganyiki tena kuchagua ccm
 
nani alikuambia kuwa Chadema watapata wabunge wachache? wabunge watakuwa wengi na wasipotosha wataunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kujumuisha wabunge wa cuf na ccm.
Piga kura kwa Dk wa ukweli, hatudanganyiki tena kuchagua ccm[/QUOTE

Tayari ishirini na wamepita bila kupingwa ukiongeza viti maalum wanakaribia mia hata oct. bado,nina wasiwasi.
 
Ni bora kura yangu mara mia ipotee kuliko kuipatia CCM inayonuka rushwa na kila aina ya maovu, nafsi yangu nitakuwa nimeitendea haki kwa kupigia mtetezi wa kweli anayeweza kupinga maovu! Tena siwezi kujipendekeza na kujigongagonga kwa mtu aliyesema hataki kura za wafanyakazi! Hata kama hashindi lakini Dr Slaa anawakilisha wanyonge na ana rekodi safi kabisa, sasa sioni kwanini niipigie CCM ya mafisadi ambayo juzi tu tumeona ilivyojiaibisha kwa rushwa na ubabe wa kuwaondoa watu waliostahili kwenye kura za maoni. Kweli ntakuwa sijatumia busara nikiichagua CCM ya waovu kwasababu tu wana possibility kubwa ya kushinda na hivyo kura yangu haitapotea (labda na mimi niwe natetea maovu)!
 
Mimi Diana na watanzania wengi tunataka kumpa kura Dr. Slaa oct.2010 lakini najiuliza nikimpa atatawala vipi huku wabunge wengi watatoka CCM? sitaki kuichezea kura yangu na watu wengi wanajiuliza swali hili naomba watu wa Chadema watueleze tukimchagua atavunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine au atapitisha vipi miswada yake bungeni.Hii mbio ya kuingia ikulu cannot be an end by itself.

wewe hujui unachoongea soma kwanza katiba ya nchi uielewe na ndio uje hapa ..sio unakuja na arguments zako za kitoto hapa
 
Tayari ishirini na wamepita bila kupingwa ukiongeza viti maalum wanakaribia mia hata oct. bado,nina wasiwasi .
Ishirini ni nini kati ya 400 weye?
Msianzishe unncessary-woga!
Muda bado, usitishwe na kelele za Makamba wewe! zile ni mbinu za vitisho!..Hujui kuwa kati yao hao 20, kuna petition kadha tayari za pingamizi?..huh!
 
Wabunge ishirini kati ya wabunge 300 na zaidi ndio wengi we dada au umetumwa? Kama kweli umenuia kutoa kura yako kwa Chadema twaiomba.
 
Msaidieni huyu Dada! Ni mmoja kati ya mamilioni wasiofahamu hilo. Na mwisho wake ni maamuzi asiyoyajua!
 
Mimi Diana na watanzania wengi tunataka kumpa kura Dr. Slaa oct.2010 lakini najiuliza nikimpa atatawala vipi huku wabunge wengi watatoka CCM? sitaki kuichezea kura yangu na watu wengi wanajiuliza swali hili naomba watu wa Chadema watueleze tukimchagua atavunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine au atapitisha vipi miswada yake bungeni.Hii mbio ya kuingia ikulu cannot be an end by itself.

Dr Slaa kawa gumzo maofisini, je ni ofisi ngapi unazozingungumzia, kwako, kwa rafiki yako au ofisi zote? Kuna Ofisi ambazo hatuzungumzii Slaa achia mbali siasa kwa ujumla.

Kiujumla Slaa hatoshinda, usipige kura au ukipiga usimpigie rais.

Kwani lazima uchaguzi mwaka huu kama hakuna mgombea anayeonekana kufaa? Uahirishwe hadi hapo tutakapokuwa tayari.
 
Mimi Diana na watanzania wengi tunataka kumpa kura Dr. Slaa oct.2010 lakini najiuliza nikimpa atatawala vipi huku wabunge wengi watatoka CCM? sitaki kuichezea kura yangu na watu wengi wanajiuliza swali hili naomba watu wa Chadema watueleze tukimchagua atavunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine au atapitisha vipi miswada yake bungeni.Hii mbio ya kuingia ikulu cannot be an end by itself.

Pole Diana, swala ulilouliza ni la msingi, na kweli watu wanataka kufahamu haya mambo. Kama majibu yenyewe ndio hayo.....Wangapi wanamuda wakusoma hiyo katiba?? Wewe uliyeisoma basi ingikua vizuri kumueleza Diana badala ya kumshabulia.

Every vote counts, so kila jimbo kushinda ni muhimu, huwezi kutabiri yatakayotekea mpaka baada ya uchaguzi....majimbo waliyopoteza Chadema sio kitu cha kuzarau. Mnataka kushika nchi lakini mkiambiwa ukweli mnanuna kwa!!
 
Mimi Diana na watanzania wengi tunataka kumpa kura Dr. Slaa oct.2010 lakini najiuliza nikimpa atatawala vipi huku wabunge wengi watatoka CCM? sitaki kuichezea kura yangu na watu wengi wanajiuliza swali hili naomba watu wa Chadema watueleze tukimchagua atavunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine au atapitisha vipi miswada yake bungeni.Hii mbio ya kuingia ikulu cannot be an end by itself.


Kwani wewe unampigia mtu kura kwa kuwa unahisi atapita? Au ni kwa sababu unaamini kuwa ndio atatetea haki, amani na maendeleo yako....! Tafadhali sana, hiyo ni kukaribisha udhaifu, na si vinginevyo...! Hata wabunge wa CCM wakiwa wengi, hawataweza kupitisha mswada wenyewe...! Hata hivyo tunamwihitaji mtu wa kuweza kuwashughulikia mafisadi wa nchi hii...! Please, change your mind, and do not get disappointed....!
 
Kila mmoja anasema anapinga UFISADI, CHADEMA na CCM...I think this fisadi thing is over rated!! Haiwezi kuwa ndio sababu ya kukuchangua, hao hao unawaita mafisadi leo hii wamehamia kwenye chama chenu. Hii vita kubwa mnayotaka kupigana, vita ndogo ndogo mnashindwa kuonyesha uwezo wenu..
 
:glasses-nerdy:KWA KUWA UMEJITAMBULISHA KUWA NI CHADEMA DAMU BASI NA KURA YANGU HUIPATI NG'O !!
Kura yako ni muhimu kwetu. Tafadhali naiomba.

Mwisho wa yote utaona mabadiliko ambayo yatakuwa yetu sote na si ya Chadema pekee. Watanzania twahitaji mabadiliko. Twahitaji siasa safi na uongozi bora.
 
nani alikuambia kuwa Chadema watapata wabunge wachache? wabunge watakuwa wengi na wasipotosha wataunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kujumuisha wabunge wa cuf na ccm.
Piga kura kwa Dk wa ukweli, hatudanganyiki tena kuchagua ccm

Si mpaka CCm wakubali?

wewe hujui unachoongea soma kwanza katiba ya nchi uielewe na ndio uje hapa ..sio unakuja na arguments zako za kitoto hapa

Si mpaka uwe na wabunge wa kutosha ndio upitishe miswaada bungeni?

Wabunge ishirini kati ya wabunge 300 na zaidi ndio wengi we dada au umetumwa? Kama kweli umenuia kutoa kura yako kwa Chadema twaiomba.

Nimetumwa na nani? nilitegemea wewe mwenye bendera ungejibu swali langu la msingi kwa unyenyekevu kupata kura yangu.
 
Msaidieni huyu Dada! Ni mmoja kati ya mamilioni wasiofahamu hilo. Na mwisho wake ni maamuzi asiyoyajua!

Pole Diana, swala ulilouliza ni la msingi, na kweli watu wanataka kufahamu haya mambo. Kama majibu yenyewe ndio hayo.....Wangapi wanamuda wakusoma hiyo katiba?? Wewe uliyeisoma basi ingikua vizuri kumueleza Diana badala ya kumshabulia.

Every vote counts, so kila jimbo kushinda ni muhimu, huwezi kutabiri yatakayotekea mpaka baada ya uchaguzi....majimbo waliyopoteza Chadema sio kitu cha kuzarau. Mnataka kushika nchi lakini mkiambiwa ukweli mnanuna kwa!!

Asanteni Dreamliner na Mapambano.
 
In fact hata kama asipopata wabunge wengi, atakuwa na wabunge wa kutosha kuendesha serikali yake kwa vile ataruhusiwa kuteua wengine 10. Sasa unapokuwa na rais anayetoka chama kingine na bunge linaongozwa na chama kingine, hapo ndipo wananchi tutakapoanza kuonja utamu wa kuwa na serikali kwani taasisi zote mbili zitawajibika sana kwetu. Sasa hivi bunge na serikali ya CCM vinalindana na inapotokea Bunge kuikaba sana serikali utasikia wabunge wanakaa kama kamati ya CHAMA, lakini katika mazingira ya hapo juu, bunge na serikali watakuwa wanachungana kwa karibu sana wasifanye madudu kila mmja akiwa tayari kula nyama ya mwenziwe.
 
Back
Top Bottom