Ni wapi naweza kupata mkopo usio na RIBA ndani ya Tanzania hii?

Amani iwe nanyi.

Moja kwa moja naomba nijitambulishe kwa imani mimi ni muumini wa dini ya Kiislam.Katika maandiko matakatifu ya kitabu cha Quran naona kuwa Suala la RIBA limekemewa sana ,kifupi ni haramu kula au kutumia RIBA!

Principle kuu ni kuwa RIBA ni haramu, yaani ongezeko lolote la pesa juu ya mkopo ni RIBA na haifai kudeal na jambo hilo. Hivyo inaniwia vigumu kukopa katika taasisi za kifedha kama vile benki maana system ya mikopo yao ni RIBA.

Ukikopa mfano shilingi milioni 1 basi utatakiwa kurudisha milioni 1.2 au ukikopa milioni 10 basi utatakiwa kurudisha milioni 12-13. Hilo ongezeko katika pesa ya mkopo ndio RIBA na ni haram.

Naombeni mnijuze ni wapi naweza kupata mkopo usio na riba!!

Asanteni
Torati 23:19-20
 
Kwahiyo ni haram kwa muislam kuwekeza pesa zake katika Mifuko kama UTT amis au kununua shares?

Hebu tufafanulie ndugu kwa faida ya wote
Quote kwenye post hiyo

"Muislam hapaswi kuwekeza (invest) kwenye kitu chochote, kuna utararibu wake na tathmini lazima ifanyike kujua kama maeneo hayo yanakubalika kisheria (sharia compliant)"
 
Mkuu unasoma hizo "aya" bila uelewa wake..........ikiwa wataka hivyo ulazimishavyo iwe basi Waislamu wote haitowafaa biashara yoyote

Uislamu juu ya suala la Riba..umetoa njia ambazo waislamu wataweza kuepuka "Riba" hiyo isiyotakiwa

Yasiofaa
1.haifai kuomba riba
2.haifai kuomba mkopo wenye riba

Ifaavyo
3. Musharakah - mwenye pesa na mwenye biashara wanakuwa washirika, wanafanya pamoja na kugawana faida
4.Murabaha-Benki inanuua bidhaa unayotaka,halafu inakuuzia kwa faida (Cost-plus financing)
5..Ijarah-benki inakukodisha kifaa na unanua baada ya muda wa kukodi (Lease)
6.Bay Salam - Mfano, mkulima analipwa kabisa kwa ajili ya mazao yake, na aleta mazao baada ya kuvuna bdae
7.Mudharaba-Benki inawekeza kwako na kuchukua asilimia ya faida ya shughuli husika (e.g 60:40) (Profit n risk sharing)

ziada
Muislam hapaswi kuwekeza (invest) kwenye kitu chochote, kuna utararibu wake na tathmini lazima ifanyike kujua kama maeneo hayo yanakubalika kisheria (sharia compliant).
Tunajua kuwa huwezi ku invest kwenye pombe, kamali, riba, n.k, lakini sio hivyo tu. Kampuni inaweza kuwa kwenye biashara halali, mfano kilimo, lakini ikakosa vigezo vingine vya uwiano wa ki-fedha (financial ratios).
Vigezo hivi vya ki-fedha vinaangalia;
1. Kiasi cha mkopo wa riba kinachangia kiasi gani katika mali zote za kampuni (interest-bearing debt/total assets shuld not exceed 30%)
2. Kiasi cha amana (interest-earning) kampuni ilichoweka benki na mali zote (interest-bearing deposits/total assets) kisizidi 30%
3. Kiasi cha mapato yanayotakana na maeneo yaliyokatazwa yasizidi 5% (non-permissible income)
4. Na “accounts receivables” zisizidi 49% ya mali za kampuni
Kama unataka kununua hisa (shares), kampuni lazima ikidhi vigezo hivyo juu.
Na hii sio kwa waislam tu, ni kwa mtu yoyote, kwa kuwa vigezo hivyo vinaiweka kampuni katika nafasi nzuri ya kuwa na maendeleo makubwa (high growth potential)

Mwisho
Watu wengi wanalalamika kuwa ni ngumu kuepuka riba, baadhi ya sababu wanazotoa ni hizi;
1. Wanatia shaka huduma za kibenki za kiislam na kusema kuwa ni ujanja tu kubadili riba na kuiita faida. Matokeo yake wanaendelea kutumia huduma za kibenki za kawaida (conventional banking)
2. Hawana hufahamu wa utararibu wa huduma za kibenki za kiislam
3. Wanasema benki za kiislam zinatoa masharti magumu ya mikopo, haswa like suala ka kutotoa mikopo ya fedha taslim (cash loans). Hali hii inapelekea thamani ya benki za kiislam (total assets) kuendelea kuwa chini ya assets za conventional banks.
Ukiangalia total assets za 50 top conventional banks only ni USD 69.6 trillion, wakati za islamic banks total globally ni USD 2.2 trillion, ila ukuaji unaendelea vizuri.
JE, NI VIP TWAWEZA KUEPEKANA NA RIBA?
KI-Iman (Religiously)
1. Kuamini kuwa rizki inapangwa na Mwenyezi Mungu, waweza acha riba na Yeye akakupa rizki yako kama kawaida (tawakkul)
2. Kumbuka kuwa kuna adhabu kubwa ya kujihusisha na riba (punishment). Financially
1. Fungua akaunti katika benki zenye utararibu usio na riba
2. Wekeza pesa zako katika mifumo isiyo na riba. Usiweke pesa zako kwenye government bonds, government bills, stocks (hisa) za makampuni yenye kufanya biashara haramu, speculation, n.k
3. Fungua akaunti za akiba (savings) ili uepukana na haja za kuomba mikopo
4. Usiingie mikataba yenye masharti ya kulipa penalties za riba
Socially (ki-jamii)
1. Ishi kwa mujibu wa kipato chako (live below your means) ili kuepuka vishawishi vya kutaka kukopa
2. Jiunge na utaratibu wa vikundi vya kupeana mikopo isiyo na riba, kama vile islamic saccos
Kumbuka kuwa madhara ya riba ni mabaya hapa duniani, na mibaya zaidi kesho akhera.
Surah Al-Baqara, Verse 276:
يَمْحَقُ اللَّهُ الرِّبَا وَيُرْبِي الصَّدَقَاتِ وَاللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ
Allah does not bless usury, and He causes charitable deeds to prosper, and Allah does not love any ungrateful sinner.

Some Credit ziende kwa: Salum Awadh

cc.Partner in business Mshana Jr
Ndugu mfano nataka nikope pesa kwa ajili ya kufanya biashara yangu ya ununuzi wa mazao vijijini huko, lets say 10M ...halafu naenda ktk benki ya kiislam mfano amana bank wanawezaje kunisaidia kupata kiasi hicho cha fedha ilihali wanasema hawatoi pesa taslim?!
 
Amani iwe nanyi.

Moja kwa moja naomba nijitambulishe kwa imani mimi ni muumini wa dini ya Kiislam.Katika maandiko matakatifu ya kitabu cha Quran naona kuwa Suala la RIBA limekemewa sana ,kifupi ni haramu kula au kutumia RIBA!

Principle kuu ni kuwa RIBA ni haramu, yaani ongezeko lolote la pesa juu ya mkopo ni RIBA na haifai kudeal na jambo hilo. Hivyo inaniwia vigumu kukopa katika taasisi za kifedha kama vile benki maana system ya mikopo yao ni RIBA.

Ukikopa mfano shilingi milioni 1 basi utatakiwa kurudisha milioni 1.2 au ukikopa milioni 10 basi utatakiwa kurudisha milioni 12-13. Hilo ongezeko katika pesa ya mkopo ndio RIBA na ni haram.

Naombeni mnijuze ni wapi naweza kupata mkopo usio na riba!!

Asanteni
Hapa Tanzania huwezi kupata nenda Burundi uko unaweza kupata
 
Ndugu mfano nataka nikope pesa kwa ajili ya kufanya biashara yangu ya ununuzi wa mazao vijijini huko, lets say 10M ...halafu naenda ktk benki ya kiislam mfano amana bank wanawezaje kunisaidia kupata kiasi hicho cha fedha ilihali wanasema hawatoi pesa taslim?!

Njia pekee nikuingia partnership na wewe...mtaifanya hiyo biashara pamoja mkigawana faida ama hasara
aidha kwa makubaliano ya kimlinganyo wa shares au mnakuwa washirika mkifanya biashara pamoja nakugawana faida
 
Mkuu usiendekeze Sana dini!
Au muombe Mungu huo mkpo wa bila riba.

Mambo mengine ni outdated! Kwaiyo wanafunzi wasipokee pesa(helbs) kwa Sababu ya riba??!

Fanya Kama dharula.
#nakopesha laki Moja kwa laki na nusu
10m kwa 15m
Karibu
Unaweza nikopesha mil 200 narudisha mil300
 
wao watanunua na kukuzia kwa faida......hii yafaa japo tu "haijuzu ikiwa watatafuta faida kubwa exceed 30%"

kwa hiyo gari la 10M wakilinunua na kukuuzia kwa 10M upto 13M ni sahihi na yajuzu

nimekuongezea nyama kwe post namba 30


Na Allah awe nawe kwenye njia njema
Ameen..shukran ndugu
 

Kumbukumbu la Torati 23:19-20 SRUV​

Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu chochote kikopeshwacho kwa riba; mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili BWANA, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki.
 
njia pekee nikuingia partnership na wewe...mtaifanya hiyo biashara pamoja mkigawana faida ama hasara
aidha kwa makubaliano ya kimlinganyo wa shares au mnakuwa washirika mkifanya biashara pamoja nakugawana faida
Kwahiyo kinachotakiwa ni kuwaeleza mategemeo ya faida unayoweza kuipata katika biashara n.k then wao ndio wanapanga uwagawie faida kiasi gani ? Vp kuhusu ile principle wanayokupa (10M)?? Unawarudishiaje?
 
Mungu anaruhusu riba

Na ndo maana wale waliopewa Taranta, aliyezifukia alimtoa na kusema bora ni yule aliyepeleka kwa watoza riba na taranta kuongezeka
 
Nenda BRANCH huko unaweza ukaamua usirudishe. Pesa ziko nje nje. Shusha application Yao kwenye simu yako ndani ya dakika kumi utapata mkopo wa bure. Utarudisha siku ukijisikia. Nadhani wale ndugu zao TALA hawapo Tena nchini. Nao walikua wanakopesha mpaka wapiga debe vituo vya daladala.
 
Mungu anaruhusu riba

Na ndo maana wale waliopewa Taranta, aliyezifukia alimtoa na kusema bora ni yule aliyepeleka kwa watoza riba na taranta kuongezeka
Kwa imani yako ila kwenye uislam hilo jambo ni HARAM
 
Hawakopeshi fedha , wanakopesha vitu ambapo ni mfumo ule ule wa riba tu sema umezungushwa.

Mfano unataka milioni 10 ununue gari, wao wanasema tunalinunua hilo gari kwa 10m halafu tunakuuzia wewe kwa milioni 13. Then unalipa kidogo kidogo.

Ila ukiwafata wakupe fedha hawatoi.
Ehh kumbe
Japo faida yake ni kwamba watu watatimiza malengo husika
 
Amani iwe nanyi.

Moja kwa moja naomba nijitambulishe kwa imani mimi ni muumini wa dini ya Kiislam.Katika maandiko matakatifu ya kitabu cha Quran naona kuwa Suala la RIBA limekemewa sana ,kifupi ni haramu kula au kutumia RIBA!

Principle kuu ni kuwa RIBA ni haramu, yaani ongezeko lolote la pesa juu ya mkopo ni RIBA na haifai kudeal na jambo hilo. Hivyo inaniwia vigumu kukopa katika taasisi za kifedha kama vile benki maana system ya mikopo yao ni RIBA.

Ukikopa mfano shilingi milioni 1 basi utatakiwa kurudisha milioni 1.2 au ukikopa milioni 10 basi utatakiwa kurudisha milioni 12-13. Hilo ongezeko katika pesa ya mkopo ndio RIBA na ni haram.

Naombeni mnijuze ni wapi naweza kupata mkopo usio na riba!!

Asanteni
Kuna ile bank ya Kiislamu inatwa AMAN kama sikosei hawana riba
 
Nenda BRANCH huko unaweza ukaamua usirudishe. Pesa ziko nje nje. Shusha application Yao kwenye simu yako ndani ya dakika kumi utapata mkopo wa bure. Utarudisha siku ukijisikia.
Nadhani wale ndugu zao TALA hawapo Tena nchini. Nao walikua wanakopesha mpaka wapiga debe vituo vya daladala.
Tupiamo link yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amani iwe nanyi.

kifupi ni haramu kula au kutumia RIBA!

Asanteni

Amini nakuambia, tofauti na muislamu mwenzako, hakuna mkopeshaji asiyependa riba. Kwa andiko lako maana yake ni kwamba, hata akikupa sehemu ya pesa yake bila kukutoza riba (asiye muislamu) lazima kuwemo na riba aliyowatoza wengine.

Nachelea kusema, MKOPO NI HARAMU KWAKO
 
Back
Top Bottom