Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,305
- 33,924
Rais wa nchi anayetokana na CCM kuwa mwenyekiti wa CCM Taifa ni utamaduni tu ndani ya CCM na wala si takwa la kikatiba la chama hicho.
Kwa sasa Mwenyekiti wa CCM ni Samia Suluhu Hassan kutokana na mwana CCM huyo kuwa Rais wa Tanzania. Lakini kabla ya kuwa Rais, Samia alikuwa ni mjumbe tu wa Kamati Kuu ya CCM na sidhani kama asingekuwa Rais angeweza hata kupendekezwa kuwa Makamu wa mwenyekiti wa chama hicho.
Nape Nnauye ni mwanasiasa mzowefu ndani ya CCM na ni mwanasiasa maarufu kuliko wanasiasa wengi sana ndani ya CCM, na imani yake kwa chama hicho inazidi imani ya wanazi wengi tu walio kwenye madaraka ya juu CCM. Ni wakati sasa bila ya kujali tamaduni ya kumfanya Rais wa nchi kuwa mwenyekiti wa CCM, Nape awe Mwenyekiti wa Taifa CCM sasa
Nape amepambana sana kwa niaba ya CCM. Hata yale mambo ya goli la mkono kwenye chaguzi yeye ndiye muasisi wa falsafa hiyo.
Kwa sasa Mwenyekiti wa CCM ni Samia Suluhu Hassan kutokana na mwana CCM huyo kuwa Rais wa Tanzania. Lakini kabla ya kuwa Rais, Samia alikuwa ni mjumbe tu wa Kamati Kuu ya CCM na sidhani kama asingekuwa Rais angeweza hata kupendekezwa kuwa Makamu wa mwenyekiti wa chama hicho.
Nape Nnauye ni mwanasiasa mzowefu ndani ya CCM na ni mwanasiasa maarufu kuliko wanasiasa wengi sana ndani ya CCM, na imani yake kwa chama hicho inazidi imani ya wanazi wengi tu walio kwenye madaraka ya juu CCM. Ni wakati sasa bila ya kujali tamaduni ya kumfanya Rais wa nchi kuwa mwenyekiti wa CCM, Nape awe Mwenyekiti wa Taifa CCM sasa
Nape amepambana sana kwa niaba ya CCM. Hata yale mambo ya goli la mkono kwenye chaguzi yeye ndiye muasisi wa falsafa hiyo.